EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, September 25, 2014

UNESCO YAWAFUA WATENDAJI WA REDIO JAMII‏

DSC_0014
Meneja wa Kituo cha Habari na Mawasiliano cha Redio Sengerema mkoani Mwanza Bw. Felician Ncheye, akiwakaribisha na kuwatambulisha wawezeshaji kwa washiriki wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku tano ya kuwajengea uwezo katika masuala ya masoko na Tehama kwa mameneja na waandishi wa habari takribani 60 kutoka Redio jamii mbalimbali nchini, yanayoendelea kwenye kituo cha habari na mawasiliano cha Redio Sengerema mkoani Mwanza.
Na Mwandishi wetu, Sengerema
SHIRIKA la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) limesema litaendelea kusaidia kuimarika kwa redio za jamii nchini kwa kuwa ndio nyenzo muhimu za maendeleo ya wananchi kwa kuwapa sauti katika huduma na shughuli zao.
Kauli hiyo imetolewa na Afisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa UNESCO, Bw. Al Amin Yusuph, wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa mameneja na watendaji takribani 60 kutoka Redio jamii mbalimbali nchini, mafunzo yanayofanyika kwenye kituo cha Redio Sengerema FM.
Katika mafunzo hayo watendaji hao watafunzwa masuala ya Tehama na utafutaji wa soko kwa lengo la kufanya redio hizo kuwa endelevu na kujiendesha zenyewe kwa kuweza kutekeleza miradi yake na kuendelea kushirikiana na wananchi.
Mafunzo hayo ni utekelezaji wa mradi wa miaka mitatu wa kuwezesha redio za jamii nchini unaoendeshwa na UNESCO baada ya redio hizo nyingi kusaidiwa kuanzishwa katika miaka ya karibuni.
DSC_0045
Afisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa UNESCO, Bw. Al Amin Yusuph akizungumza na Mameneja na waandishi wa habari kutoka redio tisa za jamii wanaohudhuria mafunzo ya siku tano ya kuwajengea uwezo katika masuala ya masoko na matumizi ya Tehama yanayofadhiliwa na mradi wa SIDA na kuratibiwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sayansi na Utamaduni (UNESCO). Kushoto mgeni rasmi Ofisa mdhani kutoka Wizara ya Habari Utamaduni Utalii na Michezo Zanzibar na Mjumbe wa bodi ya usimamizi Redio Jamii Micheweni, Ali Mohamed.

Kwa mujbu wa Yusuph mradi wa SIDA ambao umekuwa ukitekelezwa kwa kipindi cha miaka mitatu umeshughulika na uboreshaji wa redio hizo ili kuzipatia uwiano na pia kuziwezesha kutumia Tehama kuhabarisha wananchi pia kutokana na mafanikio yaliyopatikana mradi huo utaendelea kwa miaka mingine mitatu.
Ametaja mafanikio hayo kuwa yamepatikana kwa ushirikiano wa Redio za jamii pamoja na shirika hilo hali iliyofanya kuyavuta mataifa mengine kuchangia kwa ajili ya kuendelea kuzijengea uwezo redio za jamii kupitia shirika hilo.
Ameongeza kuwa kufanikiwa kwa redio za jamii nchini Tanzania katika mradi huu wa SIDA kumefanya mashirika mengi yanayotaka kufanyakazi na wananchi wa kawaida kukimbilia UNESCO kutambua redio za jamii ambazo zinaweza kufanyakazi nayo.
Mradi huo wa Tehama unaofadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Sweden (SIDA) na kuratibiwa na UNESCO ni sehemu ya mradi wa UNESCO katika nchi saba za Afrika , Tanzania ikiwamo.
DSC_0036
Baadhi ya Mameneja na waandishi wa habari kutoka redio mbalimbali za jamii wakimsikiliza Bw. Al Amin Yusuph kwenye ufunguzi wa mafunzo hayo yanayoendelea kwenye kituo cha habari na mawasiliano Sengerema Telecentre mkoani Mwanza.
Katika mafunzo hayo yanayofanyika mjini Sengerema, elimu inatolewa kwa wakuu wa vituo na waandishi wa habari kutoka redio Micheweni FM, Orkonerei FM, Pambazuko FM, Mtegani FM, Kahama FM, Redio FM, Kyela FM, Fadeco Radio na Pangani FM.
"Kuna mambo mengi yamefanikiwa.. kikubwa zaidi kumpa nafasi mwananchi kujieleza na kueleza matumaini yake.." alisema Yusuph ambapo aliongeza kwamba kutokana na mradi huo kufanikiwa zipo nchi na mashirika ambayo yapo tayari kuchangia uimarishaji wa redio za jamii nchini.Hakuzitaja nchi hizo
Alisema kutokana na mafanikio yaliyopo ya redio hizo kuwa karibu na jamii, SIDA kwa kushirikiana na UNESCO wametengeneza programu hiyo ili kuwezesha kuwepo kwa matumizi ya mtandao katika kukusanya habari, kuziboresha na kuzitumia kwa manufaa ya wananchi.
DSC_0005
DSC_0060
Ofisa mdhamini kutoka Wizara ya Habari Utamaduni Utalii na Michezo Zanzibar na Mjumbe wa bodi ya usimamizi Redio Jamii Micheweni, Ali Mohamed, akitoa baraka zake tayari kuanza mafunzo ya siku tano ya kuwajengea uwezo katika masuala ya masoko na Tehama mameneja na waandishi wa habari takribani 60 kutoka redio za jamii mbalimbali nchini, yanayoendelea kwenye kituo cha habari na mawasiliano Sengerema Telecentre mkoani Mwanza.
Alisema kutekelezwa kwa mradi huo ni utekelezaji wa azimio la Windhoek la mwaka 1991 linalohimiza matumizi ya redio jamii katika kuboresha maisha ya wananchi kutokana na kuonekana dhahiri kwamba wananchi wanapokuwa na nafasi ya kujieleza wanaweza kufanya makubwa zaidi.
Akifungua mafunzo hayo Ofisa mdhamini kutoka Wizara ya Habari Utamaduni Utalii na Michezo Zanzibar na Mjumbe wa bodi ya usimamizi redio jamii Micheweni, Ali Mohamed aliwataka mameneja na watendaji wa radio hizo kutekeleza ushauri wa UNESCO ikiwa na pamoja na kutekeleza maagizo ya utengenezaji wa vipindi vya vijana ili kupata nafasi ya kushindania nafasi moja ya upendeleo kwenda Paris , Ufaransa mwakani kwa tamasha la redio za jamii.
Aidha aliwataka watendaji kuwa makini katika kazi zao kutokana na serikali kuweka mazingira sahihi ya uendeshaji wa radio hizo kwa manufaa ya umma.
DSC_0092
Mkufunzi wa darasa la mameneja wa redio mbalimbali za jamii Mkurugenzi Mtendaji wa ASMET, Bw. Ramadhan Ahungu akiendesha mafunzo ya siku tano ya namna ya kuingiza kipato pamoja na kutafuta masoko kwa ajili ya kuendeleza vituo vyao yanayofadhiliwa na mradi wa SIDA na kuratibiwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sayansi na Utamaduni (UNESCO) yanayoendelea kwenye kituo cha habari na mawasiliano Sengerema Telecentre mkoani Mwanza.
DSC_0079
Baadhi ya mameneja wa redio mbalimbali za jamii wanaohudhuria mafunzo ya siku tano ya masoko na ujasiriamali yanayofadhiliwa na mradi wa SIDA na kuratibiwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sayansi na Utamaduni (UNESCO).
DSC_0120
Meneja wa kituo cha redio Orkonerei FM, Bw. Lucas Kariongi akihoji swali kwa mkufunzi wakati wa mafunzo hayo.
DSC_0101
Mhasibu wa kituo cha habari na mawasiliano Sengerema Telecentre, Bw. George Tumbo akiongaza washiriki wenzake katika kazi za vikundi wakati wa mafunzo hayo.
DSC_0171
Afisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa UNESCO, Bw. Al Amin Yusuph akiendesha mafunzo ya matumizi ya Tehama kuwajengea uwezo wa kuweka kumbukumbu za vipindi na kukusanya vyanzo vya habari kwa kutumia "Tablet" kwa waandishi wa habari wa redio mbalimbali za jamii yanayofadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Sweden (SIDA) na kuratibiwa na shirika la UNESCO yanayoendelea kwenye kituo cha Redio Sengerema mkoani Mwanza.
DSC_0156
Afisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa UNESCO, Bw. Al Amin Yusuph akitoa maelekezo ya matumizi ya "TABLET" katika kuhifadhi na kuandaa habari kwa kutumia kifaa hicho.
DSC_0142
Pichani juu na chini ni washiriki wa mafunzo hayo wakifanya mafunzo kwa vitendo kwa kutumia Teknolojia mpya ya "TABLET".
DSC_0136

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate