EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, October 28, 2014

BINTI ATEKWA NA WACHUNA NGOZI


Stori: Chande Abdallah na Deogratius Mongela
MBONA
majanga! Mrembo aliyejitambulisha kwa jina la Latifa Abdallah (19), mkazi wa Kinondoni –Mkwajuni, Dar amesimulia alivyotekwa na watu aliodai ni wachuna ngozi wakiwa na mwanamke aliyevalia kininja ndani ya gari jeusi.

Binti anayetambulika kwa jina la Latifa Abdallah (wa pili kushoto) akiwa na ndugu zake.
Akizungumza na Uwazi jijini Dar, juzi, Latifa alidai Oktoba 19, mwaka huu akiwa anatoka kumsindikiza dada yake aliyekuwa akienda Kibaha, Pwani ghafla msichana aliyevalia kininja akajigonga kwenye mwamvuli alioushika na kumwambia alimgonga kwa makusudi.
“Nilimwomba msamaha na kumwambia ni bahati mbaya lakini alinikamata na kuniingiza ndani ya gari jeusi lililopaki kando ya barabara ambapo kuna mtu alifungua mlango yule mwanamke akanisukumia ndani,” alisema Latifa.
Akizidi kusimulia, binti huyo alisema kuwa, ndani ya gari hilo alimkuta msichana mmoja kama yeye na mtoto kama wa miaka miwili wakiwa wamefungwa vitambaa vyeusi machoni na yeye akafungwa kama wenzake.
“Tulikwenda kushushwa kwenye nyumba moja sijui ni wapi, tukaingizwa katika  chumba kidogo na kufunguliwa vitambaa. Ndipo nilipogundua kuwa, watekaji wote walivaa kininja. Mmoja alikuwa mwanaume, mwingine ndiyo yule aliyenisukumia ndani ya gari pale kwenye Kituo cha Daladala cha Vijana Kinondoni (Dar).
Fomu ya PF3 ya Latifa Abdalla aliyopewa kituo cha Polisi Oysterbay.
“Yule mwanaume alisema lazima tufanye  naye mapenzi la sivyo atatufanya kama watakavyomfanyia yule mtoto. Wakamchukua yule mtoto na kumchoma sindano, alilia sana kisha akanyamza ghafla huku ngozi yake ikiumuka kama puto. Yule mwanaume alitoa kisu na kuanza kumchuna ngozi yule mtoto akianzia shingoni.
“Nikiwa katika hali ya kutetemeka kwa woga, yule mwanamke alisema tujiandae na kifo kama cha yule mtoto. Nilimwomba Mungu sana atuepushie kifo hicho.
“Siku ya Jumanne asubuhi wale watu walikuja kutuangalia kidogo na kuondoka. Baadaye jioni walirudi na kutupa maji ambayo hatukuelewa ndani yake yalikuwa na nini, walitunywesha na kutuambia kesho yake wangeturudisha makwetu, wakachukua namba za simu za ndugu zetu, sikuamini nikawatajia namba ya mwalimu wangu wa cherehani ambaye waliniambia akipokea nimwambie kuwa mimi ni mzima nitafika nyumbani kesho kutokea Kawe  jambo ambalo nililifanya.
“Kuanzia hapo yule mwanamke akawa anachati naye. Wakati huo yule mwenzangu kwao ni Mbezi naye aliwataarifu ndugu zake na tukawa tunasubiri kesho ifike. Kweli, kesho yake wakatuchukua, mimi nikashushwa pale Kituo cha Daladala Kinondoni–Studio (Dar), wakanipa shilingi 1,000 wakasema nipande bodaboda nirudi nyumbani,” alisema Latifa.
Mwalimu wa cherehani wa Latifa, Celestine ‘Baba Mkanji’ alisema tangu Latifa atoweke nyumbani amekuwa akipigiwa simu na kutumiwa meseji zinazoonesha Latifa alikuwa kwenye hali ya hatari jambo lililomshtua na kuwashirikisha ndugu zake nao wakaripoti Kituo cha Polisi cha Mzambarauni, baadaye Kituo cha Polisi cha Oysterbay jijini Dar.
Baada ya kurudishwa nyumbani, Latifa alipelekwa Oysterbay Polisi kwa ajili ya kupata PF3 na baadaye kwenda Hospitali ya Mwananyamala kwa ajili ya vipimo zaidi.
Naye mama mzazi wa Latifa, Habiba Saidi (56) alisema  amesikitishwa na kitendo alichofanyiwa mwanaye na kuomba watu wa haki za binadamu na wanasheria wamsaidie ili waliomfanyia mambo hayo mwanaye wakamatwe.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate