Stori: Mwandishi Wetu HUKU
 mwenyewe akikanusha vikali kwamba hatumii, nyota wa muziki wa Injili 
Bongo, Rose Muhando bado anaandamwa na madai mazito kwamba anatumia 
madawa ya kulevya ‘unga’ yanayomfanya kuwa hoi kiasi cha kushindwa 
kutokea kwenye matamasha mbalimbali anayolipwa fedha, Risasi Jumatano 
linateremka nayo.
Kwa mujibu wa vyanzo, Rose anadaiwa kutumia unga kiasi kwamba, baada 
ya matumizi hujikuta akishindwa kufanya jambo lolote lile la kujitafutia
 mkate wake wa kila siku na ndiyo maana amekuwa akikwaa skendo za 
kupokea fedha za shoo halafu hatokei tu!
WATOA MADAI
Hivi karibuni, akina mama watatu walifika kwenye Ofisi za Global Publisheers na kumtolea madai Rose kuhusu tuhuma zanazomwandama kwamba amekuwa akiingia mitini na fedha za watu wanaomwita kwenye matamasha ya nyimbo za Injili.
Hivi karibuni, akina mama watatu walifika kwenye Ofisi za Global Publisheers na kumtolea madai Rose kuhusu tuhuma zanazomwandama kwamba amekuwa akiingia mitini na fedha za watu wanaomwita kwenye matamasha ya nyimbo za Injili.
“Sisi
 tunavyojua, Rose anatumia madawa, wengine wanasema unga wengine 
wanasema sijui nini huko. Sasa akishatumia hayo madawa huwa yanamfanya 
awe kama amelewa na kushindwa kufanya lolote.
“Huwa anafika hatua anashinda kitandani amelala tu na hawezi kutoka, ndiyo maana mtu anaweza kumpa pesa asitokee kuimba kwa sababu anashindwa kutoka ndani kwake.
“Kwa hiyo jamani, si suala la kumwandika tu
 kwamba anaingia mitini na fedha za watu bali mumsaidie Rose kama kweli 
mnampenda, sisi wenyewe tunamwombea kwa Mungu kila siku,” alisema mama 
mmoja kati ya hao waliofika lakini bila kutaja majina yao.
MADAI SUGU
Madai ya kwamba, Rose anatumia madawa ni ya siku nyingi, wengi wamekuwa wakisema wana uhakika, wengine wanasema wanasikiasikia tu lakini hawana uhakika.
Madai ya kwamba, Rose anatumia madawa ni ya siku nyingi, wengi wamekuwa wakisema wana uhakika, wengine wanasema wanasikiasikia tu lakini hawana uhakika.
Magazeti ya Global (Ijumaa Wikienda, Uwazi, Risasi Jumatano, Amani, 
Ijumaa na Risasi Jumamosi) yameshapokea madai hayo kwa muda mrefu lakini
 kilichokuwa kikifanyika ni kuendelea kumchunguza msanii huyo kuhusu 
madai hayo.
RISASI LAINGIA KAZINI KUCHUNGUZA
Kufuatia madai ya akina mama hao waliojitambulisha ni waumini wa kutoka katika kanisa moja la kilokole jijini Dar, gazeti hili liliamua kuingia kazini kufanya uchunguzi ili kubaini ukweli au uongo wa madai hayo.
Kufuatia madai ya akina mama hao waliojitambulisha ni waumini wa kutoka katika kanisa moja la kilokole jijini Dar, gazeti hili liliamua kuingia kazini kufanya uchunguzi ili kubaini ukweli au uongo wa madai hayo.
WATU WA KARIBU NA ROSE
Mtu wa kwanza kumtafuta ambaye gazeti hili liliamini kwamba anaweza kujua chochote kuhusu madai hayo ni mratibu wa Tamasha la Pasaka linalofanyika kila mwaka kwenye baadhi ya mikoa, Alex Msama.
Msama: “Mimi siwezi kusema ni kweli kwani sijawahi kumwona akitumia wala sijui kama ameathirika.”
Mtu wa kwanza kumtafuta ambaye gazeti hili liliamini kwamba anaweza kujua chochote kuhusu madai hayo ni mratibu wa Tamasha la Pasaka linalofanyika kila mwaka kwenye baadhi ya mikoa, Alex Msama.
Msama: “Mimi siwezi kusema ni kweli kwani sijawahi kumwona akitumia wala sijui kama ameathirika.”
Risasi Jumatano likamsaka Katibu wa Chama cha Waimba
 Injili Tanzania (Chawaita), Stela Joel: “Mimi sijui, kama unasema kuna 
watu wamekuja ofisini kwenu na kutoa madai hayo, basi wamwombee. Lakini 
tutachunguza.”
MCHUNGAJI
Risasi Jumatano pia lilibahatika kuzungumza na mchungaji mmoja (jina tunalo) ambaye alisema ameshawahi kusikia taarifa hizo akamuuliza Rose lakini alimkatalia kuwa si madai ya kweli.
Risasi Jumatano pia lilibahatika kuzungumza na mchungaji mmoja (jina tunalo) ambaye alisema ameshawahi kusikia taarifa hizo akamuuliza Rose lakini alimkatalia kuwa si madai ya kweli.
“Ila ninachojua mimi ni kwamba, Rose amekuwa akitumia dawa f’lani 
(akazitaja jina). Hizi ni dawa zinazopatikana kwa njia ya sindano. Mara 
nyingi mtu akiwa hajiwezi kwa maana ya kushindwa kufanya kazi anachomwa 
hizi zinampa nguvu.
“Niliwahi kusikia kwamba, kuna daktari mmoja katika Hospitali ya Mkoa
 wa Dodoma (akamtaja jina). Huyu ndiye aliyekuwa akimchoma sindano zenye
 dawa hizo Rose pale mwili unapokuwa dhaifu.
“Ila madhara yake sasa, dawa ikiwa imekwisha mwilini, mtu anakuwa 
mlegevu, anahisi kizunguzungu au kulalalala, kutokwa jasho jingi na 
kuhisi anaumwa kiasi kwamba ukimwona unaweza kusema ni teja. Ni dawa 
ghali sana kwa dozi moja, nadhani ni shilingi laki sita,” alisema 
mchungaji huyo.
Akaongeza: “Nasikia Rose amefika mahali huwa anajichoma mwenyewe akipata dozi. Kwa hiyo kwa suala la kubwia unga nadhani alilikanusha.”
ROSE MWENYEWE SASA Risasi Jumatano, juzi lilimpigia simu Rose lakini hakupokea hata baada ya kurudia kumpigia mara kadhaa. Likamtumia meseji na kumsomea mashitaka yote, akajibu:
Akaongeza: “Nasikia Rose amefika mahali huwa anajichoma mwenyewe akipata dozi. Kwa hiyo kwa suala la kubwia unga nadhani alilikanusha.”
ROSE MWENYEWE SASA Risasi Jumatano, juzi lilimpigia simu Rose lakini hakupokea hata baada ya kurudia kumpigia mara kadhaa. Likamtumia meseji na kumsomea mashitaka yote, akajibu:
“Samahani sana nawaomba mnipumzishe kuniandika...najua ni nani na kwa
 nini ananitenda hivyo, ni kwa sababu anataka kunitumia kwa faida yake 
na ni mtu hatari sana kwangu na kwa taifa zima.
“Mtu huyo anafanya haya ili kuniziba mdomo kwani najua siri zake nyingi na nzito, nashindwa kusema ataniua.”
“Mtu huyo anafanya haya ili kuniziba mdomo kwani najua siri zake nyingi na nzito, nashindwa kusema ataniua.”
Hata hivyo, Rose alipotakiwa kumtaja kwa jina mtu huyo ambaye Risasi Jumatano halimjui, alikataa katakata akisema anaogopa!
CHANZO: GPL 



No comments:
Post a Comment