EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, November 28, 2014

CHENGE, CHENGE, CHENGE TENA?


 
Makala: Ojuku Abraham
KAMA Mwalimu Julius Kambarage Nyerere angekuwa bado anatawala nchi hii, ni watu wachache sana wangeweza kulijua jina la Andrew Chenge, yule mwanasheria mkuu wa zamani wa serikali, aliyekaa katika ofisi hiyo kubwa na yenye heshima, kuanzia mwaka 1993 hadi 2005.
Lakini katika nchi ambayo inaendeshwa kwa hila na dili, jina hili linajipatia umaarufu na kuenziwa, bila kujali ni kwa kiasi gani, Watanzania zaidi ya milioni 45 wanaishi kwa dhiki na mateso kutokana na yeye kuitumia vibaya ofisi ya umma kujinufaisha.
Ni katika kipindi chake akiwa mwanasheria mkuu wa serikali, ndipo nchi yetu imeshuhudia kashfa za mikataba mingi mibovu, isiyo na tija kwa nchi, ikisainiwa. Siyo tu mikataba bali hata sheria nyingi zisizofaa zikilazimishwa kutumika.

Orodha ya kashfa zake ni nyingi, lakini hapa nitatoa chache, ili tujiulize, kwa nini mtu huyu bado anaaminika kiasi eti cha kupewa hadi uenyekiti wa kuandika Katiba Mpya Inayopendekezwa?
Huyu ndiye alikuwa mwanasheria mkuu wa serikali katika skendo zote kubwa zinazohusu fedha za umma kuibiwa, kuanzia Meremeta Gold Mine, ununuzi wa ndege ya rais, ununuzi wa Rada na EPA. Katika skendo ya Tegeta Escrow, ambayo imeibuka akiwa nje ya ofisi, amepewa mgawo kwa sababu anajua kila kitu kuhusu IPTL, maana wakati ‘wezi’ hawa wanakuja, alikuwa ofisini.
Siyo hivyo tu, huyu jamaa akiwa mwanasheria mkuu wa serikali, ndiye aliyeshinikiza kupitishwa kwa sheria mbovu ya takrima, ambayo kimsingi ni rushwa. Wakati sheria ya kupinga matokeo ya ubunge
mahakamani ikimtaka anayepinga kulipia shilingi milioni tano inapitishwa, alikuwa pale akiiwakilisha serikali!Kama Jaji Frederick Werema katika skendo moja tu ya Tegeta Escrow amesababisha serikali kukosa shilingi bilioni 20 kama kodi, huyu mtu aliisababishia nchi hii hasara ya mabilioni mangapi katika mandingo yake yote? Kwa nini bado anapeta?
Kama tutasema kila kitu ambacho Chenge amekifanya katika kuharibu uchumi wa nchi hii, hatuwezi kumaliza, lakini lugha yake ya kejeli wakati akiulizwa kuhusu fedha alizoweka katika Kisiwa cha Jersey kule Uingereza katika ile skendo ya ununuzi wa Rada, yanaonesha kuwa ana fedha nyingi alizochota.
Zaidi ya shilingi bilioni moja aliziita vijisenti, akimaanisha alikuwa na zaidi ya hizo na kwamba hata wenzake nao wanazo nyingi pia.
Halafu, CCM inamteua kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Uandishi wa Katiba Mpya Inayopendekezwa. Ndiyo maana akabariki viondolewe vifungu muhimu kabisa kama vya maadili, ukomo wa ubunge na kuondoa nguvu ya wapiga kura katika kuwawajibisha wabunge wao.
Katika nchi ambayo inajali wananchi wake na inayopinga kwa nguvu zote vitendo vya ufisadi, Chenge hakutakiwa kuonekana akidunda mtaani. Alitakiwa awe amerudisha mali zote ambazo zilipatikana kwa kutumia vibaya ofisi ya umma. Nakaa na kujiuliza, ni nani anamlinda na kwa maslahi gani? Inakuwaje anaendelea kuaminika katika masuala yanayohusu uhai wa taifa?
Inakuwa vigumu kidogo kuamini kama yuko peke yake kwenye haya mambo na kama analindwa na tunaowaamini, basi kama taifa, bado tuna safari ndefu kufikia maendeleo tunayotaka!   

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate