EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, November 21, 2014

IMEFICHUKA ANAYEWAUZA MASTAA BONGO HUYU HAPA!

CHANZO: GLOBAL PUBLISHERS
Imefichuka! Kwa muda mrefu kumekuwa na taarifa za chini kwa chini kwamba baadhi ya mastaa wa kike Bongo, hasa wale wa filamu ‘Bongo Movies’ huuzwa kwa wanaume, mara nyingine kwa kujua au kutojua lakini wenyewe wamekuwa wakikanusha hivyo kutoa ‘kibarua’ kwa Ijumaa kuingia mzigoni kisha kumuibua mmoja wa wahusika (kuwadi) anayerahisisha biashara hiyo haramu ya ngono.
Jokate Mwegelo akipozi.
UCHUNGUZI
Uchunguzi wa gazeti hili ulibaini kwamba, kuwadi huyo huwa anajua dau la kila staa hivyo anapopata mwanaume hasa mapedeshee, wafanyabiashara na baadhi ya vigogo serikalini, huwaunganisha kwa kutoa namna ya mawasiliano au kuwaunganisha moja kwa moja.

MADAI MAZITO
Uchunguzi huo ulibaini uwepo wa madai mazito kwamba wapo baadhi ya mastaa wa kike wa Bongo Movies ambao hugombewa na makuwadi kwa sababu wana soko kubwa.
“Jaribu kufikiri msanii haonekani location (eneo la kuigizia sinema) wala sinema aliyocheza haijulikani lakini muda mwingi utamuona anatanua kwenye viwanja vya starehe, lazima ujiongeze kwamba kipato kinatoka wapi?
Staa wa filamu Bongo Aunt Lulu.
“Mimi nakwambia hii Bongo Movies imebaki jina tu, sioni mwanga mbeleni kwa sababu hawa mabinti hawapo serious zaidi ya kutafutiwa wanaume,” kilidai chanzo chetu ambacho ni mfuatiliaji wa karibu wa kazi za sanaa Bongo.
STAA GANI MWENYE SOKO KUBWA?
Madai mazito yaliendelea kushushwa kwamba wapo wanunuaji ambao huhonga magari (bila kadi) ambapo baadaye hukamatwa kimafia na kurejeshwa kwa mhongaji.
Ikazidi kufahamika kwamba, mastaa wenye sifa ya kuhongwa magari ni wale wenye majina makubwa.

Staa wa filamu Bongo, Jacqueline Wolper Massawe.

KUANZIA SH. MIL. 5 HADI BUKU 50
Ilisemekana kwamba wapo mastaa wanaotajiwa dau kubwa kuanzia Sh. milioni tano na kuendelea na wapo wa chini ya hapo hadi buku hamsini (50,000).

Mpaka sasa kuna mastaa wanaowindwa na makuwadi kwa kuwa wana soko na bei zao kwenye mabano ni pamoja na Elizabeth Michael ‘Lulu’ (Mil. 5), Jokate Mwegelo (Mil. 5), Wema Isaac Sepetu (Mil. 5), Kajala Masanja (Mil. 5) na Jacqueline Wolper Massawe (Mil. 5).
Staa wa filamu Bongo, Jacqueline Pentzel ‘Jack Chuz’.
Wengine ni Baby Joseph Madaha (Mil. 5), Miriam Jolwa ‘Jini Kabula’ (Mil. 3), Aunty Ezekiel (Mil. 3), Jennifer Mwaipaja ‘Shumileta’ (Mil. 2) Isabela Francis ‘Vai wa Ukweli’ (Mil. 1), Lulu Mathias ‘Anti Lulu’ (Mil. 1), Jacqueline Pentzel ‘Jack Chuz’ (Mi. 1) na wengine kibao ambapo kwa sasa upepo umegeukia kwa wale wanaochipukia.
ANAYEWAUZA MASTAA HUYU!
Katika kusaka ukweli juu ya skendo hiyo, jina la mmoja wa makuwadi hao ambaye ni mwigizaji wa kike Bongo, Lungi Maulanga (pichani) ilitajwa.
Staa wa filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’.
Mbali na Lungi pia alitajwa mwigizaji mmoja wa kiume wa Bongo Movies na jamaa mwingine ambaye huwa ni mdandiaji wa ishu za mastaa (majina tunayo, tutayataja tukijiridhisha kisheria).
LUNGI ASAKWA
Baada ya kutajiwa jina la Lungi, gazeti hili lilimsaka mwigizaji huyo anayedaiwa kuwauza baadhi ya mastaa hao kwa wanaume ambapo alibanwa vilivyo hadi akaanika siri nzito nyuma ya biashara hiyo kubwa isiyo na kodi.
Staa wa filamu Bongo, Wema Sepetu.
Mbali na kukiri kuwakuwadia mastaa hao kipindi cha nyuma kabla ya kuacha, Lungi alifunguka kwamba amekuwa akisumbuliwa na wanaume wakware wakitaka awaunganishe na mastaa ambao alidai alishafanya nao kazi hiyo muda mrefu.
MSIKIE LUNGI Ijumaa: Habari yako Lungi... Lungi: Nzuri, mmekuja kufuata nini hapa (nyumbani kwake Kinondoni, Dar)? Ijumaa: Mbona unajihami? Tumekuja kukusomea mashitaka yako! Lungi: Mashitaka gani? Siku hizi nimetulia, sijichanganyi kama zamani, kulikoni tena? Ijumaa: Hapa kuna madai mazito...
Staa wa filamu Bongo, Vai wa Ukweli.
Lungi: Hebu semeni kilichowaleta, kwanza siku hizi sipendi kukutana na waandishi wa habari! Ijumaa: Kuna za chinichini kwamba wewe ndiye unayewauza mastaa wa Bongo na ndiyo biashara inayokuweka mjini kwa kuwa hata location huonekani. Je, ni kweli?
Lungi: (kwa hasira) yaani mimi niwekwe mjini na mastaa? Kwani hamjui anayeniweka mjini? Au mnataka niwafukuze na panga?Ijumaa: Kwa nini unakuwa mkali Lungi? Unachotakiwa kufanya ni kutoa majibu kwa sababu kuna shosti’ako ametutajia staa uliyemuuza juzi tu!
Staa wa filamu Bongo, Aunty Ezekiel akipozi.
Lungi: (bila kujua anarekodiwa) juzi! Sikieni, nawaheshimu sana, mimi nilikuwa nikifanya biashara hiyo siku nyingi na niliacha kwa sababu hao mastaa hawana maana, wakishapata wanajisikia na kusahau walipotoka.
“Huyo aliyewaambia ana ushahidi gani kama juzi nimeshamuuza staa? Ijumaa: Oke, tuache hilo! Unakumbuka dau kubwa ulilowahi kupewa wakati unawakuwadia? Lungi: (kwa mara ya kwanza anatabasamu) nilishawahi kupata hadi Sh. milioni tatu na kima cha chini laki tano, lakini jamani mbona ni siku nyingi?
Staa wa filamu Bongo, Lungi Maulanga.
“Kwanza mimi sitaki hizo habari kabisa. Nimechoka kusumbuliwa na wanaume kwa ishu hizo.” Ijumaa: Hilo dau kubwa ulilipata kwa mwanaume wa Dar, mikoani au nje ya nchi? Lungi: Watu wa mikoani ndiyo wanakata mkwanja mkubwa, hapa Dar longolongo tu. Hiyo Sh. milioni tatu niliipata kwa jamaa mmoja wa Arusha.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate