EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, December 27, 2014

MTOTO ASOMBWA NA MAJI, AFARIKI

 
CHANZO: GLOBAL PUBLISHERS
MTOTO wa miaka sita, Bernard Benjamin ambaye alikuwa mwanafunzi wa Shule ya Msingi Nyamunge, wilayani Ilemela jijini Mwanza, amesombwa na mafuriko na mwili wake kukaa siku kumi na tano bila kuharibika.
Mafuriko yaliyosababisha kifo cha marehemu mtoto Bernard Benjamin.
Tukio hilo lilijiri Desemba 2, mwaka huu kwenye Mto Kenge jijini hapa, maeneo ya Mabatini, Wilaya ya Nyamagana baada ya kujaa maji ambapo marehemu alisombwa na mafuriko hadi pembezoni mwa Ziwa Victoria.

Baba mzazi wa marehemu Bernard, Benjamin David alisema siku ya tukio yeye alikuwa safari na mama wa mtoto alikuwa kazini, watoto walibaki na msichana wa kazi nyumbani.
Baba wa marehemu Bernard Benjamin akihuzunika.
“Ilikuwa Jumanne asubuhi, mvua kubwa sana ilinyesha kwa saa moja na nusu hivi na kusababisha mafuriko. Watoto wangu wote walikuwa nyumbani, lakini mvua ilipokatika walitoka nje na kuanza kucheza.
“Marehemu alikuwa anaondoka bila kuaga kama mara tatu na kila alipofuatwa alikutwa akicheza pembezoni mwa mto huo ambao  umepita jirani na nyumba yangu.“Katika hali ya kushangaza mara ya tatu wenzake walimfuata na kuanza kurudi naye wakati huo marehemu alikuwa yupo nyuma ndipo aliteleza na kutumbukia kwenye maji ya mto.
Mwili wa marehemu Bernard Benjamin ukiwekwa kaburini.
“Alipiga kelele na wenzake walivyosikia sauti nao walipiga mayowe, mmoja wao alijitosa kwenye maji ili amuokoe lakini kasi ya maji ilimshinda na kujikuta akijiokoa mwenyewe kwa kushika mti, watu wakamuwahi na kumuokoa.
“Tuliutafuta mwili tangu siku hiyo hadi Jumatano ya Desemba 17. Saa 10 jioni mke wangu alipigiwa simu na mtu aliyejitambulisha kuwa ni muumini wa kanisa kwetu, akasema kuna mwili wa mtoto umekutwa ufukweni mwa Ziwa Victoria eneo la Miti Mirefu.
Mama mzazi wa marehemu Bernard Benjamin akiweka mchanga kaburini.
“Nilikwenda na kukuta polisi wameshafika. Nilipouona mwili niliutambua kuwa ni wa mwanangu akiwa ameshafariki dunia lakini haukuwa umeharibika.“Bado alikuwa na nguo alizovaa siku ya tukio, viungo vyake vyote vilikuwa salama ila mwili ulikuwa mweupe sana kutokana na kukaa muda mrefu kwenye maji.
Mtoto Bernard Benjamin enzi za uhai wake.
“Tuliupeleka mwili Hospitali ya Rufaa ya Bugando, madaktari walimfanyia uchungzi na kusema mwili haukuharibika kutokana na kufukiwa na mchanga mwingi kwenye maji, nilimshukuru Mungu kwa hilo,” alisema baba wa marehemu.Mazishi ya mtoto huyo yalifanyika Alhamisi ya Desemba 18, mwaka huu katika Makaburi ya Nyakato Sokoni jijini Mwanza.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate