EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, January 29, 2015

RAIS KIKWETE MGENI RASMI MAADHIMISHO SIKU YA SHERIA

Jaji Mkuu wa Tanzania Mh. Othman Chande (Kulia) akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari kuhusu maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini mwaka 2015. Maadhimisho hayo yanaongozwa na maudhui yasemayo “ Fursa ya kupata haki: wajibu wa Serikali, Mahakama na wadau”. Kushoto ni Mh. Hussein Kattanga, Mtendaji Mkuu wa Mahakama.
Msajili Mkuu wa Mahakama, Ignas Kitus (kulia) akizungumza akifafanua jambo wakati Jaji Mkuu wa Tanzania Mh. Othman Chande alipokutana na waandishi wa habari kuzungumzia maadhimisho ya Siku ya Sheria leo jijini Dar es salaam.
Waandishi wa habari waliohudhuria mkutano huo leo. Picha na Aron Msigwa -MAELEZO.
 
Na. Aron Msigwa – MAELEZO.
 Rais Jakaya Kikwete anatarijiwa kuwa mgeni rasmi katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya sheria nchini (Law Day) itakayofanyika Februari 4, 2015, katika viwanja vya mahakama vilivyopo mtaa wa Chimala jijini Dar es salaam.
 
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam, Jaji Mkuu wa Tanzania Mh. Othman Chande amesema kuwa maadhimisho hayo kwa mwaka huu yanaongozwa na maudhui yasemayo  “ Fursa ya kupata haki: wajibu wa Serikali, Mahakama na wadau”.
 
 Amesema kwa mara ya kwanza maadhimisho hayo yataambatana na maonesho ya Wiki ya   Shera yatakayofanyika  katika viwanja vya Mnazi Mmoja   kuanzia  tarehe  30 Januari  2015  hadi  tarehe  2 Februari  2015 .
Mh.Chande ameeleza kuwa maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini na maonesho ya Wiki ya Sheria yanaashiria mwanzo wa shughuli za mahakama kwa mwaka 2015  na kufafanua kuwa kipaumbele kitatolewa katika kupunguza mrundikano wa mashauri ya muda mrefu yaliyoko mahakamani na kushughulikia mashauri yenye mvuto mkubwa kijamii,miradi mikubwa, uhujumu uchumi, madawa ya kulevya, Biashara ndani na nje ya nchi na Rushwa.
 
Kuhusu maonesho hayo amesema yanalenga  kutoa elimu kwa wadau wa sheria na huduma za kisheria kwa wananchi kuhusu Ufunguaji na uendeshaji wa mashauri mbalimbali hasa mirathi, Utatuzi wa migogoro kwa njia ya suluhu, kueleza mfumo mpya wa ulipaji wa tozo za kimahakama kwa njia ya benki, Kutoa msaada wa kisheria, kutolewa vyeti vya mawakili, kupokea maoni na malalamiko kwa ajili ya kuyatafutia ufumbuzi.
 
Ameeleza kuwa wadau wakuu  watakaoshiriki katika maonesho hayo ni Mahakama, Tume ya Utumishi wa Mahakama, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka, Chuo cha Uongozi wa Mahakama- Lushoto, Taasisi ya Mafunzo ya Uansheria kwa vitendo Tanzania na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora.
 
Wadau wengine ni Taasisi zinazotoa msaada wa kisheria, TAKUKURU, Jeshi la Polisi, Magereza, Chama cha Mawakili Tanganyika na Tume ya kurekebisha sheria.
 
Amesema pamoja na maonesho hayo kutakuwa na matembezi maalum ya kuadhimisha Wiki ya Sheria tarehe 1 Februari 2015 yatakayoongozwa na Rais mstaafu wa awamu ya pili Mh. Ali Hassan Mwinyi kuanzia Mahakama Kisutu kupitia barabara za Serena-Ohio, Gymkana –Obama Road, Mahakama ya Biashara, Barabara ya Kivukoni, Sokoine , Railway, Nkurumah, Lumumba na Mkunguni hadi Mnazi Mmoja.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate