EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, February 21, 2015

AIBU! TICHA MBARONI KWA KUMUUZISHA MTOTO MAYAI MUDA WA SHULE

CHANZO: GLOBAL PUBLISHERS
MATUKIO ya mateso, unyanyasaji na utumwa kwa watoto yanashika kasi nchini! Safari hii mwalimu wa shule moja ya msingi iliyopo Mburahati jijini Dar aliyetajwa kwa jina moja la Lucy ametia aibu baada ya kutiwa mbaroni katika Kituo cha Polisi cha Magomeni, Dar akituhumiwa kumtumikisha mtoto mwenye umri wa miaka 12 aitwaye Sakina kwa kumuuzisha mayai ya kuchemsha na soseji.

Mwalimu huyo akijitetea juu ya sakata hilo.
Kwa mujibu wa mashuhuda wetu, tukio hilo lilichukua nafasi maeneo ya Kashuda Bar, Magomeni hivi karibuni baada ya wakazi wa eneo hilo kuhamaki kumuona binti huyo akitembeza mayai na soseji mtaani wakati umri wake ni mdogo kinyume na sheria za ajira.
RAIA WAMZUNGUKA
Ilisemekana kwamba, baada ya kukerwa na kitendo hicho huku Sakina akionekana hana furaha, raia hao wenye hasira kali walimhoji ambapo alimtaja mwalimu huyo kuwa ndiye bosi wake aliyemchukua kutoka Tanga kwa ajili ya kufanya kazi za ndani (hausigeli).

AFUATWA SHULENI
Ilidaiwa kwamba, wakifuatana na mtoto huyo, wakazi hao walifunga safari hadi shuleni kwa mwalimu huyo Mburahati ambapo wanahabari wetu walitonywa na kutia timu hadi kwa mkuu wa shule hiyo, Kibassa ambaye alikiri kuchukizwa na kitendo cha mfanyakazi wake kumwajiri mtoto wa miaka 12 kumtumikisha kazi akiwa ni mwajiri wa serikali.
Mwananfunzi Sakina anayedaiwa kuuzishwa mayai muda wa shule.
“Kimsingi nimesikitishwa kwa sababu Lucy ni mwajiriwa wa serikali, hapaswi kufanya jambo baya kama hili. Kwa umri wake alipaswa awe darasani,” alisema Kibassa.
MWALIMU AJITETEA
Kwa upande wake, Lucy alijitetea kuwa binti huyo aliletewa na mtu aliyemtaja kwa jina la Kizito aliyemuagiza mfanyakazi wa ndani, lakini baada ya kufika binti huyo alimkataa na kudai bado mdogo asingeweza kufanya kazi za ndani.
Mwalimu huyo alisema alikuwa akimsubiri binti mwingine mkubwa aletewe na Kizito ili amrudishe Sakina kwao na kudai kuwa hata biashara ya mayai hakumtuma yeye bali alimtuma John (kijana wake wa kazi) ila inawezekana Sakina alijiingiza kujisaidia na ugumu wa maisha.

Mwalimu huyo akiwekwa kikao.
BINTI ASIMULIA
Akiwa shuleni hapo, mbele ya bosi wake, Sakina alifunguka kuwa amekuwa akifanya biashara hiyo na kufanya kazi za ndani kwa Lucy huku akisimulia kunusurika kubakwa na kupitia mateso mengine kama kunyimwa chakula na kulazimika kutembeza mayai na soseji mchana kutwa.
“Nafanya kazi za ndani na kutembeza mayai, kuna kaka mmoja nilimwomba msaada ili nirudi nyumbani, akanilazimisha tufanye mapenzi ndipo anisaidie, nilipokataa akaniacha,” alisema Sakina.
Hata hivyo, mwalimu huyo alitolewa shuleni hapo chini ya ulinzi mkali kisha kufikishwa Polisi Magomeni katika dawati la jinsia kwa hatua zaidi.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate