EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, February 23, 2015

DIAMOND ATUPIWA JINI, LAMPATA MAMA'KE


Musa mateja/Ijumaa wikienda
Imevuja! Kuna madai kwamba staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ ametupiwa jini lakini likamkosa na kumpata mama yake mzazi, Sanura Kassim ‘Sandra’ kisha kumsababishia ‘gonjwa’ la ajabu, Ijumaa Wikienda linakupa mchapo kamili.


Staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akiwa na mama yake mzazi, Sanura Kassim ‘Sandra’.
TUJIUNGE NA CHANZO
Kwa mujibu wa chanzo makini, watu wanaodaiwa kuwa ni wabaya wa Diamond (Anti-Diamond) walimtupia jini staa huyo lakini bahati nzuri likamkosa na kwa bahati mbaya likampata mama yake ambaye alipata ugonjwa wa kupooza ghafla.

“Ujue kumekuwa na sintofahamu kwa muda mrefu juu ya ugonjwa wa mama Diamond lakini habari za uhakika ni kwamba, mama Diamond yupo hoi baada ya kutupiwa jini ambalo mlengwa wake alikuwa Diamond.

“Mungu tu hakupenda limpate Diamond lakini inasemekana kwamba jini hilo ni hatari endapo lingempata Diamond kwa jinsi lilivyokuwa, basi pengine leo tungekuwa tunazungumza mengine,” kilisema chanzo hicho.

DIAMOND ALIJUA ‘MCHEZO’ HUO?
Chanzo hicho kilizidi kumwaga data kwamba, Diamond alijua kwamba mama yake ametupiwa jini ndiyo maana alikuwa akisuasua kutoa uamuzi wa kumuwahisha nchini India kwa matibabu ya hospitali.
“Diamond alijua kuhusu mpango huo wa wabaya wake kutaka kummaliza kishirikina ndiyo maana hakutaka kumkimbiza haraka hospitali na badala yake alijikita kwenye swala na dua kwani yeye anaamini katika dini zaidi,” kilisema chanzo hicho.

Hata hivyo, baada ya kutafakari kwa umakini wa hali ya juu, imeelezwa kwamba, Diamond alilazimika kumpeleka mama yake nchini India na kupatiwa matibabu kisha kurejea nchini.

ALIRUDI MZIMA
Kwa mujibu wa ndugu wa Diamond ambaye hakupenda jina lake lichorwe gazetini, hivi karibuni (kabla ya Valentine’s Day), mama Diamond alirejea nchini akiwa na afya njema lakini siku chache baadaye alizidiwa tena na kurudishwa India huku ndugu wakijawa na hofu.

“Alirudi Bongo lakini hakukaa sana akazidiwa tena tukalazimika kumrudisha India kwani hali ilizidi kuwa mbaya. Tumekuwa hatutaki kueleza sana juu ya suala hili maana Diamond mwenyewe hapendi haya mambo yajulikane,” alisema ndugu huyo.

DIAMOND AFUNGUKA
Baada ya chanzo hicho kuvujisha ‘ubuyu’ huo, mwanahabari wetu alimvutia waya Diamond ambapo alikiri kwamba mama yake yupo India lakini hakutaka kulizungumzia zaidi eneo hilo badala yake akaanza kushusha lawama kwa wale aliodai wanamsema vibaya.

“Mama bado yuko kwenye matibabu nchini India na hali yake kusema kweli si nzuri, naomba hapo nisizungumzie sana. Kuhusu masuala ya kutupiwa jini, mimi namuamini Mungu, naamini mama atapona.
 

“Inaniuma kila siku ninaposikia watu wanaongea vitu ambavyo si kweli na kwa namna nyingine nashindwa kujibu vitu ambavyo mwenyewe sivijui hivyo yote namwachia Mungu, maana yeye ndiye jibu la yote.

“Halafu pia kuna muda ufike, watu wawe wanafahamu mimi pia ni binadamu kama binadamu wengine, wasiwe wananijazia vitu utafikiri mimi sina moyo, wawe waelewa, sipo katika kipindi kizuri kwa sasa na si kila kitu wanachosikia au kuona lazima mimi nikizungumzie, kuna mambo mengine ni ya ndani ya ukoo na yako juu yangu sana, hivyo ukiona kimya simaanishi kuna watu nimewadharau,” alisema Diamond.

TUMEFIKAJE HAPO?
Hivi karibuni kuliibuka madai kwamba kwa makusudi Diamond alishindwa kuhudhuria msiba wa baba Abdul Sykes ‘Dully’ na badala yake picha zikavuja zikimuonesha akiwa kisiwani Zanzibar na mpenzi wake Zarina Hassan ‘Zari’ kitu ambacho mwenyewe alikikanusha.

“Si kila picha unayoiona katika mtandao wa kijamii basi itakuwa imepigwa muda huo, inaweza kuwekwa leo kumbe ni ya muda mrefu,” alisema Diamond.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate