EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, February 5, 2015

Mjumbe wa NEC Ludewa ambae ni mwenyekiti wa UVCCM wilaya hiyo afariki dunia‏

 Aliyekuwa MNEC  wa  wilaya ya  Ludewa  Elizabeth Haule  wa  pili kushoto enzi za uhai  wake  akiwa na viongozi  wa  wilaya  hiyo wakati wa mkutano mkuu wa wilaya ya  Ludewa mwaka jana ,kulia  ni mbunge wa  jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe ,aliyesimama ni mwenyekiti  wa CCM wilaya  ya Ludewa Stanley Kolimba na wa kwanza  kushoto katibu  wa CCM wilaya ya  Ludewa Eliud Semauye (picha na maktaba ya matukiodaimaBlog)
 
Na  MatukiodaimaBLOG

CHAMA  cha  mapinduzi (CCM)  wilaya ya  Ludewa  mkoani  Njombe  kimepata  pigo  kubwa kufuatia  kifo  cha  aliyekuwa  mjumbe  wa  Halmashauri  kuu ya wilaya  hiyo (NEC)  Bi  Elizabeth Haule.


Mbali ya  kuwa MNEC  wa  wilaya  hiyo  Haule  pia  alikuwa ni mwenyekiti  wa UVCCM wilaya ya  Ludewa  kabla ya  kujiuzulu kwake mwezi  February mwaka jana baada ya  kuchaguliwa nafasi hiyo ya  NEC na  nafasi   hiyo  kuwa  wazi  hadi sasa.


katibu   mwenezi  wa  CCM  wilaya  ya  Ludewa  Felix Haule  alisema  kuwa  kifo cha  kionozi  huyo  kimetokea  usiku  wa kuamkia leo akiwa katika  Hospitali ya  wilaya ya  Ludewa ambako  alilazwa jana  mchana kwa tatizo la  moyo.


Bw  Haule  alisema  kuwa siku ya  jumatatu wiki  iliyopita   marehemu  alipata   kuongoza  kikao  chake  cha mwisho   cha baraza la vijana  la  wilaya ya  Ludewa  na baada ya  hapo hali  yake ya afya  ilianza  kuzidi  kuwa mbaya  zaidi kabla ya kuamua jana  kwenda Hospitali ambako  walimlaza 


Alisema  kuwa mazishi ya  mjumbe  huyo wa NEC  wilaya ya  Ludewa yanataraji  kufanyika  kesho  kutwa jumamosi kijijini kwake Mholo kata ya Luana wilayani  Ludewa .

Aliyekuwa MNEC  wa  wilaya ya  Ludewa Elizabeth   Haule  (kulia) akishiriki  na   vijana  wenzake  kuigiza
Kwa  upande  wake  mbunge wa  jimbo la  Ludewa  Deo Filikunjombe  akielezea  kifo cha  MNEC  huyo  alisema  kuwa amepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya  kifo  hicho na kuwa kwa  sasa  anafanya maandalizi ya  kuelekea   jimboni  Ludewa  ili  kuungana na  wana CCM na  wananchi  wa wilaya   hiyo katika mazishi ya  kiongozi huyo.

Marehemu Elizabeth Haule  enzi  za uhai  wake
Mbunge  Filikunjombe  alisema  kuwa  CCM wilaya ya  Ludewa  imempoteza  kiongozi mchapa  kazi na aliyekuwa na uwezo  mkubwa katika  kukitumikia  chama ngazi ya  wilaya na Taifa na  kuwa kati ya  vijana  ambao wamekuwa mbele  kujenga  chama katika  wilaya   hiyo ni pamoja na marehemu huyo kwani  siku  zote za  uhai  wake alikuwa  ni mhumini mzuri  wa kunadi  sera  za CCM na hakuwa kiongozi mwenye majivuno  wala makundi.

Hivyo  alisema  kuwa  kifo  cha MNEC  huyo kimekuja  huku  wilaya ya  Ludewa ikiwa katika maandalizi ya  kuanzimisha miaka 38  ya kuzaliwa kwa  CCM sherehe  iliyopangwa  kufanyika siku ya jumapili  ya February 8 mwaka   huu kwa mara ya kwanza katika kata ya Kilondo mwambao mwa ziwa nyasa  lakini kutokana na msiba  huo  mkubwa sherehe   hizo  zitasogezwa  mbele  hadi Februari  15 mwaka  huu.


" Mimi   pia nilikuwa  nikijiandaa  kwa ajili ya  kuanza  safari ya  kuelekea  wilayani Ludewa  katika sherehe za miaka 38 ya kuzaliwa  kwa CCM kama mgeni  rasmi ila sitaweza  kufanya   hivyo na  chama  kimeamua  kusogeza  sherehe  hizo hadi jumapili ya ijayo  ili  kupisha maombolezo kwa  wana CCM kwa  kifo  cha kiongozi   huyo"





No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate