EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, February 18, 2015

MTOTO WA FLORA JIPU PWAA!

Stori: Richard Bukos na Issa Mnally/Risasi Mchanganyiko
BAADA ya utata wa uhalali wa baba wa mtoto wa Mwimba Injili maarufu Bongo, Flora Mbasha kutawala kwenye magazeti mbalimbali na mitandao ya kijamii, hatimaye jipu limepasuka baada ya baba mdogo wa Flora, aliyejitambulisha kwa jina moja la Kisekwa kufunguka kwamba mtoto huyo ni damu halali ya Mbasha, Risasi Mchanganyiko lina kauli yake kuthibitisha hilo. 
Mwimba Injili maarufu Bongo, Flora Mbasha.
NI MAHAKAMA YA ILALA
Kisekwa alifunguka hayo juzikati katika Mahakama ya Ilala jijini Dar alipokuwa amekwenda kusikiliza kesi ya aliyekuwa mume wa Flora, Emmanuel Mbasha kudaiwa kumbaka shemeji yake ambapo alisema anamshangaa Mbasha kushindwa kukiri ukweli ulio wazi kwamba mtoto ni damu yake wakati moyoni anautambua.
TUJIUNGE NA KISEKWA
“Inakuwaje Mbasha anashindwa kukubali ukweli kwamba mtoto ni wake wakati anatambua fika kwamba ujauzito ni mali yake kabla hata ya mgogoro wao? Ndugu wote tulikuwa tunajua hilo, upande wetu na hata kwao. Mbona hakuikataa tangu kipindi hicho?
Aliyekuwa mume wa Flora Mbasha, Emmanuel Mbasha.
Mgogoro wao ulikuwa wa mambo ya kawaida ya kifamilia, haukuhusiana hata kidogo na Flora kuchepuka wala nini, tangu mwanzoni mwa mgogoro wao wakiwa wanaishi pamoja wameshaitwa mara tatu katika ofisi za Ustawi wa Jamii na alielezwa kuwa mkewe ni mjamzito, akifahamu ni mali yake na akaonywa kuwa kitendo cha kuendekeza migogoro ya mara kwa mara kinaweza kumletea matatizo mkewe na kichanga kilichokuwa tumboni, mbona hakubisha? Tulikuwa tukijadili matatizo yao na kila mmoja kuweka hoja zake mezani, hakuna kati yao aliyehusisha mgogoro huo na suala la kuchepuka,” alisema Kisekwa.

Flora Mbasha wakati wa kujifungua.
KIAPO CHATAJWA
Kama hiyo haitoshi, kuonesha ana uhakika na anachokizungumza, Kisekwa alimtaka Mbasha ajiapize kwa kushika kitabu kitakatifu cha Biblia kama ana mashaka na ukweli aliouzungumza.
AKERWA NA MADAI YA GWAJIMA
Mzazi huyo alisema anakerwa zaidi jinsi ambavyo Mbasha amewahi kukaririwa akimhusisha mkewe kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima kwamba ni baba wa mtoto huyo.
“Anamsingizia tu baba wa watu (Gwajima) maskini ya Mungu kwa vile hapendi kuona anavyomsaidia Flora, lakini ukweli Gwajima sisi ni ndugu yetu, mimi G ananiita baba mdogo kama anavyooniita Flora,” alisema Kisekwa.
Mchungaji Gwajima.
MBASHA ANASEMAJE?
Wanahabari wetu walipomtafuta Mbasha kuhusiana na ukweli kwamba kichanga ni mali yake, hakutaka kukubali wala kukataa zaidi ya kupinga suala la ujomba wa Flora na Gwajima.
“Flora aseme ukweli, ujomba wa yeye na Gwajima umetoka wapi? Hilo tu ndiyo nataka alifafanue kwa undani maana wajomba zake wote mimi nilitambulishwa wakati ninamuoa,” alisema Mbasha.
Mwandishi: Kuhusu ukweli kwamba mtoto ni wako unazungumziaje?
Mbasha: Hilo litajulikana tu lakini mimi nataka kujua ujomba wake na Gwajima umetoka wapi? Hapo tu.
TUJIKUMBUSHE
Mbasha na Flora ambao waliishi kwenye ndoa na kufanikiwa kupata mtoto mmoja, mwaka jana walifikia hatua ya kutengana na kila mmoja kuishi kivyake baada ya kushindwa kutatua mgogoro wao wa muda mrefu wa kifamilia.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate