EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, February 11, 2015

NAY WA MITEGO USIPOJIPANGA TUTAKUPANGA!

KWAKO mkali wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’. Mambo vipi? Mishe zinasemaje? Binafsi mimi ni mzima wa afya, maisha yanasonga mbele kwa kasi ya ajabu. Tunapambana!
Nimekukumbuka leo kwa barua maana kitambo kidogo hatujaonana. Nakupongeza kwa nyimbo zako maana hata wale waliosema ulibebwa na Diamond katika wimbo wa Muziki Gani, sasa hivi wanajutia kauli zao.

Wanaona walikosea maana umefyatua nyimbo zako mwenyewe na unaendelea kukimbiza mitaani.
Madhumuni ya barua hii ni kutaka kukueleza kwamba wewe ni staa hivyo unapaswa kuwa mfano wa kuigwa na kila mtu katika jamii. Hutakiwi kuteleza hata kidogo. Ukiwa wewe ndiyo kinara wa majanga, utatolewa mfano kwamba hufai kuigwa kutokana na matendo yako maovu.
Kila mmoja anatambua uwezo wako, anatambua hatua ambayo umefikia kimuziki. Watu wanatambua kwamba una mchumba ambaye una mikakati ya kufika naye mbali kwa maana ya ndoa Mungu akipenda.
Kinachoshangaza ni kwamba, inakuwaje unaonekana katika pozi za kimahaba na mwanamke mwingine? Picha zenyewe zinatia kinyaa?
Mwishoni mwa wiki iliyopita gumzo katika mitandao ya kijamii ilikuwa ni wewe na picha zako za utupu na mwanamke huyo ambaye hakuwa mchumba wako.Ndugu yangu, picha zile hazikuwa nzuri kwako. Zimekudhalilisha na hata kukuletea ugomvi kwa mchumba wako.
Kwa nini ulikubali kupiga picha za namna ile? Zilikuwa za nini? Ulikuwa na malengo gani? Hata kama mlikuwa katika ‘shooting’ ya wimbo kwa nini ulikubali kupigwa picha katika hatua ile?
Tena bora zingevujishwa na mtu mwingine, wewe mwenyewe unatajwa kuwa ndiye chanzo cha kusambaa kwa picha hizo kupitia mitandao yako ya kijamii, hivi kwenye kichwa chako uliwaza kabla ya kufanya?
Unapaswa kujiheshimu hata kama ni video ya wimbo, naamini kwa desturi zetu, kamwe huwezi kuruhusiwa kurusha video ya namna hiyo hewani. Tamaduni zetu haziruhusu, unasubiri nani akuzuie kufanya hivyo wakati wewe kama kioo cha jamii unapaswa kuwa mfano?
Una watoto sasa, ulimwengu wa sasa si ule wa zamani. Picha zako za utupu zinachapishwa magazetini, zitasambaa kwenye mitandao mbalimbali na wanao pia watajionea bila wasiwasi. Watajifunza nini kutoka kwa baba? Jibu najua unalo na haliwezi kuwa zuri kwa mtu muungwana.

Ulimwengu wa sasa, ukifanya vituko vya namna hiyo, rekodi zake zinabaki kwenye mitandao. Vizazi na vizazi vitakuja kuona hayo uliyoyafanya juzi. Badilika kaka!Ni matumaini yangu utakuwa umenielewa, kwa leo naishia hapa, naamini utafanyia kazi mawazo yangu na kubadilika.
Wasalaam,

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate