EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, February 13, 2015

RAY C, BABA MWENYE NYUMBA WAKE KIMEUKA

Stori:Waandishi wetu/Ijumaa
Inadaiwa kuwa kimenuka kati ya msanii Rehema Chalamila ‘Ray C’ na baba mwenye nyumba wake, Hussein Kassim baada ya mdada huyo kudaiwa kugoma kutoa vyombo vyake kwenye mgahawa aliopangishwa na mkataba kuisha.
Msanii Rehema Chalamila ‘Ray C’.
Ray C aliyekuwa akitoa huduma ya chakula na vinywaji kwa wafanyakazi wa Hospitali ya Mwananyamala jijini Dar kupitia mgahawa wake maarufu kwa jina la Ray C Restaurant, alifikia hatua hiyo baada ya kudai kuwa na yeye alipwe fidia ya shilingi laki moja kwa ajili ya ukarabati alioufanya.
Akizungumza na gazeti hili, baba mwenye nyumba hiyo alisema baada ya Ray C kugoma kutoa vitu vyake, aliamua kwenda kumshtaki kwa mabosi wao wa kitengo cha Methadone ambacho kinamtibu Ray C na yeye mwenyewe kwani wote ni waathirika wa madawa ya kulevya.
Baba mwenye nyumba huyo alidai baada ya kumshtaki katika kitengo hicho, Ray C aliahidi kwenda kuvunja ukuta ambao aliujenga na kuchukua vitu vyake hivyo baada ya siku mbili na angepeleka ufunguo kwa mkuu wa kitengo cha Methadone.


Baba mwenye nyumba wa Ray C.
“Mkataba uliisha Januari 19, mwaka huu lakini akakaa kimya mpaka nilivyoenda kumwambia maana alikuwa ameshikilia ufunguo wangu huku mimi nimeshapata mteja mwingine.
“Kila nikimwambia aje kutoa vitu vyake anakataa na kusema mpaka nimlipe laki moja aliyofanyia ukarabati wakati mimi hakunishirikisha, sikutaka kufika huku maana Ray C ni mwenzangu tunakunywa naye dawa lakini ukorofi wake ndiyo umesababisha haya yote,” alisema Hussein.
Baada ya siku mbili kupita, mkuu wao alimtaka aende kisheria ambapo alienda kuripoti katika Ofisi ya Serikali ya Mtaa wa Minazini, Mwananyamala na Ray C akaandikiwa barua ya wito mara ya kwanza, hakwenda baada ya hapo akaandikiwa kwa mara ya pili, Jumanne iliyopita ambayo alifika akiwa amechelewa.
Ray C baada ya kuambiwa dhumuni la wito huo kwa afisa mtendaji, aliahidi kutoa vitu hivyo siku iliyofuata.Alipoulizwa Ray C kuhusiana na tukio hilo, alikiri kupelekwa serikali ya mtaa na kusema vitu vingi vinavyoongelewa dhidi yake havina ukweli.
“Hayo wanayozungumza ni mambo ya Kiswahili tu, mimi nimeshaachia fremu ila bado kuchukua vitu vyangu tu, nenda serikali ya mtaa utapata maelezo kamili maana hao wanataka kunichafulia jina tu,” alisema Ray C.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate