EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, February 27, 2015

TOP TEN YA MASTAA KUVAA NUSU UTUPU SIYO ISHU KWAO!

MAKALA: AMRAN KAIMA/Ijumaa
Ukifuatilia sana kwenye nchi za wenzetu kama vile Marekani na kwingineko, mastaa hawako makini na suala la uvaaji. Yaani si ajabu kuona staa mkubwa akikatiza mtaani akiwa amevaa nguo ya ndani na ukishangaa utaonekana mshamba.
Jokate Mwegelo.
Wanaovaa hivyo hawajakosa nguo za heshima za kuvaa bali ni ule ulimbukeni wa kutaka wawe gumzo na kuendelea kuwa maarufu.Kutokana na athari ya utandawazi, hapa Bongo wapo mastaa ambao nao wameiga kiasi cha kutoona aibu kuvaa nguo zinazoacha wazi maungo yao.Najua wapo wengi lakini leo nimeona nikupe kumi bora ya mastaa hao.

Baby Joseph Madaha
Huyu ni mwanamuziki na muigizaji. Wengi wanamfahamu kwa kupenda kuyaacha wazi matiti yake sambamba na kupenda kuvaa visketi na vigauni vinavyoacha wazi sehemu kubwa ya mapaja.
Stejini ndiyo kabisa hadi kufuli lake kama siku hiyo amelivaa haoni aibu kulifanya lionekane kwa mashabiki wanaofuatilia shoo yake.
Miriam Jolwa ‘Jini Kabula’
Ni muigizaji aliyejaribu kuingia kwenye muziki lakini akashindwa. Naye ni kati ya mastaa wasiothamini miili yao. Ni mrefu kwa umbo lakini cha ajabu hupendelea kuvaa vipensi na visketi vifupi huku naye akiona poa watu kuona nido zake.
Tamrina Poshi ‘Amanda’.
Tamrina Poshi ‘Amanda’
Kwa umbile wengi tunamjua kuwa ni kati ya mastaa waliofungashia ile mbaya. Hata hivyo, anatajwa kuwa miongoni mwa mastaa wa kike ambao hupenda kuwarusha roho wanaume akatizapo mtaani.
Kutokana na hilo, yeye ni muumini wa kutoanika nido zake lakini hupendelea kuvaa vigauni vifupi sana ambavyo wakati mwingine hata akitakiwa kuinama kuokota kitu hawezi, akiinama lazina kalio lake lote litabaki nje.
Isabella Mpanda ‘Bella’
Huyu ni kati ya mastaa mcharuko ambaye ni mama wa mtoto mmoja lakini linapokuja suala la kuvaa, mara nyingi hupenda kuvaa vinguo vifupi licha ya kwamba kimwili chake ni kidogo.
Jokate Mwegelo
Huyu havumi lakini yumo! Ni mwanamitindo ambaye ukimkuta kwenye sherehe za heshima huwezi kuamini kama ndiyo yule ambaye maeneo mengi yenye mkusanyiko wa watu huvaa vinguo vya kimitego.Kuona mapaja yake wala siyo ishu kwani kuna wakati huvaa vigauni vifupi sana au mashati makubwa bila suruali wala pensi. Hata hivyo, kuona nido zake ni shughuli.
Lulu Semagongo ‘Anti Lulu’
Nani asiyemjua huyu kwa vurugu zake? Naye ana wowowo kama Amanda. Ingekuwa ni mtu anayejiheshimu angekuwa ni wa kuvaa madira na magauni makubwa lakini kwa mcharuko wake, yeye ni mwendo wa nguo fupi tu. Hata linapokuja suala la sehemu ya kifua, mara nyingi haoni hatari kuyaanika matiti yake.
Vanessa Mdee ‘V- Money’
Huyu ni Mtangazaji wa Radio Choice FM ya jijini Dar anayefanya vizuri kwenye muziki. Ukimfuatilia sana utagundua ni binti anayependa sana kuvaa vipensi na wakati mwingine fulana tu ambazo hufunika sehemu ndogo ya mapaja. Awapo stejini ndiyo usiseme. Huwa anapendelea kuvaa sidiria na visketi ambavyo akionesha manjonjo yake, kama kavaa kufuli lazima lionekane.
Aunt Ezekiel.
Aunt Ezekiel
Kwa sasa ni mjamzito lakini kutokana na kasumba yake bado utamkuta kavaa kipensi. Kwenye mitoko yake mara chache sana utamkuta kavaa kiheshima. Kwa wale wanaojua katalogi zake akiwa viwanja watakubalinana na mimi kwamba, ni binti ambaye haoni hatari wanaume ‘kumchungulia’.
Zuena Mohammed ‘Shilole’
Naye kajaaliwa kuwa na kijungu flani hivi. Ni staa wa muziki na filamu ambaye inavyoonekana kuvaa nguo za heshima kwake ni mwiko, labda awe amealikwa kwenye ‘minuso’ ya watu wenye heshima zao.
Lungi Maulanga
Huyu ni msanii wa filamu ambaye linapokuja suala la kuvaa kiheshima huenda mkagombana. Akiwa viwanja utamjua kuwa ni binti wa mjini asiyependa kujibanabana.
 Kwa kifupi anapenda kuvaa nguo za kihasara.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate