EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, February 5, 2015

Ulaji vyakula vya asili huzuia saratani’

BalancedDiet

Na Michael Sarungi, Dar es Salaam

WATANZANIA wametakiwa kujenga utamaduni wa kula vyakula vya asili katika kujikinga na ugonjwa wa saratani, ambao hivi sasa umekuwa tishio duniani.
Mbali na hilo, pia wametakiwa kuepuka uvutaji wa sigara, ulevi wa kupindukia na kubadili aina ya maisha kama njia ya kukabiliana na ugonjwa huo.


Akizungumza na MTANZANIA Dar es Salaam jana, daktari bingwa wa magonjwa ya saratani wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road, Dk. Harrison Chuwa, alisema katika kipindi cha mwaka mmoja hali ya ugonjwa huo imezidi kuwa mbaya.


“Katika kuadhimisha Siku ya Saratani Duniani leo, hali imekuwa ikibadilika na katika kipindi cha miaka mitatu, taasisi hiyo imekuwa ikipokea wagonjwa wa saratani 1,500 hadi 4,000 kwa mwaka,” alisema.


Alisema kati ya wagonjwa hao, wengi wao ni wale ambao ugonjwa huwa umefikia hatua za juu kiasi cha kusababisha matibabu yao kuwa ya gharama kubwa.
“Kwa kweli hata hali yetu ya maisha imekuwa ikichangia kwa kiwango kikubwa kuongezeka kwa ugonjwa huu hapa nchini. Kuacha kula vyakula vya asili na mboga za majani ni tatizo… badala yake vyakula vya kemikali nyingi vimechukua nafasi jambo ambalo si zuri kwa afya za Watanzania,” alisema Dk. Chuwa.


Alisema zipo njia nyingi za kuzuia saratani, ikiwamo kula vyakula vya asili, hasa ugali wa dona ulioandaliwa vizuri na kufanya mazoezi ya viungo.
Dk. Chuwa alisema kwa mujibu wa Taasisi ya Global Cane, hadi kufikia mwaka 2012, iliripotiwa kuwapo wagonjwa wapatao milioni 14.1 duniani, kati yao milioni 8.2 walifariki dunia.


“Unajua tatizo la nchi nyingi za Afrika ni elimu juu ya ugonjwa huu. Watu wengi bado wana uelewa mdogo juu ya ugojwa huu, ndiyo maana wengi wanakuja wakiwa wamechelewa,” alisema Dk. Chuwa.
Tezi dume kupimwa bure


Wakati huohuo, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii inaandaa kampeni ya kuwapima bure wananchi ugonjwa wa saratani ya tezi dume.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma jana, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif Rashid, alisema upimaji huo utafanyika kama sehemu ya kukabiliana na ugonjwa huo.


Dk. Rashid alikuwa akizungumzia maadhimisho ya Siku ya Saratani Duniani ambayo hufanyika Februari 4 kila mwaka.


“Katika kuadhimisha Siku ya Saratani Duniani, wizara kwa kushirikiana na Taasisi ya Saratani ya Ocean Road ya Dar es Salaam, itatoa ujumbe uwafikie wananchi wote, ukieleza jinsi tunavyoweza kudhibiti saratani tutakaposhirikiana, na pia tutatoa elimu zaidi kwa umma kuhusu maradhi hayo.
“Pia, tutawapima wananchi saratani ya shingo ya kizazi na matiti, lakini pia wizara yetu inaandaa kampeni ya uchunguzi wa saratani ya tezi dume utakaofanyika mapema mwaka huu.
“Katika hili, tarehe kamili ya uchunguzi huu itatangazwa mipango itakapokamilika na upimaji huu utafanyika bure. Kwahiyo wananchi wote wanakaribishwa kwa ajili ya upimaji huo,” alisema Dk. Rashid.
Akizungumzia maradhi ya saratani kwa ujumla, alisema yamekuwa yakiongezeka kila siku duniani ingawa idadi kubwa ya wagonjwa iko katika nchi zinazoendelea.
“Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), kila mwaka wagonjwa wapya milioni 12.6 hugundulika duniani wakiwa na saratani.
“Hapa nchini idadi ya wagonjwa wapya wa saratani kila mwaka ni 34,000, lakini wengi wao hawafiki hospitalini kutokana na sababu mbalimbali,” alisema Dk. Rashid.

CHANZO: MTANZANIA

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate