EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, March 7, 2015

BARNABA: WAIFU WANGU NI MODO MKALII!

MAMBO vipi msomaji wa safu hii ya Mpaka Home, tumekutana tena katika maeneo yetu ya kujidai. Ni sehemu pekee ya kuweza kujua maisha halisi ya mastaa nyumbani kwa mastaa wetu Bongo.
Barnaba akiwa na mke wake.
Wiki hii nimetia timu mitaa ya Mwananyamala-Komakoma, kumsaka kijana machachari, anayesumbua kwa kuwa na sauti kali ya kumtoa nyoka pangoni, si mwingine bali ni Barnaba Elias.
Nyumbani kwake Barnaba anaishi na mkewe halali wa ndoa, Zubeda Mussa, pamoja na mtoto wao kipenzi, Steve.Amezungumza mengi, twende pamoja:

RATIBA YAKE YA SIKU IKOJE?
“Mimi naamka mapema sana saa 11:00 alfajiri kwa ajili ya kufanya mazoezi ya kukimbia, baada ya kurudi mazoezini, naoga kisha napata kifungua kinywa halafu narudi tena kulala kwani ninakuwa  nimeamka mapema sana na kama sina kazi siku hiyo nitaamka mchana na kufanya kazi zangu kwenye studio yangu ambayo nimeifungua hapa nyumbani inayoitwa High Table Sound.”
Barnaba Elias akiwa na familia yake.
ANAPENDA KUFANYA NINI AKIWA NYUMBANI?
“Kwa kweli hakuna kitu nachokipenda zaidi kama kukaa na familia yangu, kujadili zaidi maisha mimi na mke wangu na mara nyingi napenda kucheza mpira na mwanangu kitu ambacho tunakifurahia wote.”
ANAPENDELEA CHAKULA GANI?
“Kwa upande wa chakula, napenda sana ugali, wali, ndizi na mbogamboga kwa upande wa mchana lakini kifungua kinywa nakunywa chai na kitu chochote aina ya mkate kwa ajili ya sauti.”
NI WAGENI GANI ANAWAHITAJI KWAKE?
“Mimi napendelea sana wageni wastaarabu na wenye heshima ingawaje sichagui mgeni wa kuja kwangu kwa sababu napenda sana wageni.”
Mwanamuziki Barnaba akiwa kwenye studio yake ya nyumbni.
NINI AMBACHO ANAKITAMANI KWA SASA?
“Unajua kwa sasa nina mtoto wa kiume lakini natamani sana mtoto wa kike angekuwepo hapa nyumbani ingekuwa poa sana lakini naamini Mungu atanipa tu.”
KUNA TOFAUTI ALIVYOKUWA KWAKE NA KWAO?
“Tofauti ni kubwa sana kwa kweli, kule nilikuwa chini ya wazazi wangu lakini hapa na mimi ni baba wa familia na ninajipangia mimi mwenyewe vitu vyangu na familia yangu.”
ATAENDELEA KUISHI KWENYE NYUMBA YA KUPANGA?
“Kwa kweli Mungu akinisaidia mwaka huu na mimi nitakuwa nimeshahamia kwangu, nashukuru nimejitahidi na mimi nimepata kwangu sasa.”
VIPI UNAMSHIRIKISHA WAIFU KWENYE MUZIKI WAKO?
“Ndiyo kama katika wimbo wa Wahaladee, nilikuwa sioni haja ya kumtafuta Video Queen (modo) mwingine wakati mke wangu ana vigezo vyote, ni mkali ambapo nilimuweka na akafiti kwelikweli.”

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate