EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, March 9, 2015

DAKTARI AANIKA UGONJWA WA BANZA STONE


Gladness Mallya/ijumaawikienda
Inasikitisha sana! Huku akitundikiwa dripu nyumbani kwao, Sinza ya Vatican jijini Dar, daktari ameanika ugonjwa unaomtesa staa wa muziki wa Dansi Bongo, Ramadhan Masanja ‘Banza Stone’ kuwa vipimo vinaonesha anashambuliwa na fangasi kichwani (ubongo) na shingoni.
Staa wa muziki wa Dansi Bongo, Ramadhan Masanja ‘Banza Stone’.
YU HOI TENA
Habari zinaeleza kuwa tatizo hilo limesababisha Banza kuwa hoi kwa mara nyingine akiumwa na kichwa kupita kiasi hivyo kushindwa kufanya lolote.Kufuatia maumivu anayoyapata, Banza amewaomba Watanzani wamuombee kwani anaamini katika maombi yao.

MAOMBI MUHIMU
Akizungumza kwa tabu na Ijumaa Wikienda, Banza ambaye kwa sasa hawezi kunyanyuka kwenye kochi alisema anatamani angepona ili arudi jukwaani hivyo maombi yao ni muhimu kuliko kitu chochote na ni msaada tosha kwake.
“Kikubwa nawaomba Watanzania waniombee kwani hali niliyonayo siyo ya kawaida, nasikia maumivu makali sana ya kichwa na shingo hadi nashindwa kula.“Hata kuongea ndiyo hivi kwa shida na muda mwingi naweka kitambaa cha maji ya baridi kwenye paji la uso ili kupunguza makali ya maumivu,” alisema Banza kwa masikitiko makubwa.
Banza kwa sasa anatibiwa nyumbani kwao baada ya kupata matibabu kwenye Hospitali ya Sinza-Palestina ambapo anaongezewa maji (dripu) na kuendelea kumeza dawa za ugonjwa huo.
DAKTARI ATHIBITISHA
Banza alisema ugonjwa huo amethibitishiwa na daktari wake kwenye hospitali hiyo baada ya kuchukuliwa vipimo.
FANGASI KICHWANI AU KWENYE UBONGO IKOJE?
Kwa mujibu wa mtaalam wa magonjwa ya kichwa, kitaalam ugonjwa huo huitwa Mucormycosis.
Ni ugonjwa ambao katika siku za hivi karibuni umekuwa maarufu huku ukisababisha vifo vya watu wengi. Kitaalam, ugonjwa huu husababishwa na fangasi waitwao Murcorales ambao huingia ndani ya mwili wa binadamu kwa njia ya hewa.
Ukivuta hewa yenye fangasi hao, huingia na kwenda moja kwa moja kwenye mfumo wa damu kisha kuanza kuzunguka ndani ya mwili kufuata damu. Baada ya kukaa kwa wiki kadhaa kwenye mfumo wa damu, huhamia kwenye uti wa mgongo (spinal) ambapo huzaliana kwa wingi na kuanza kusambaa kuelekea kwenye ubongo.
Fangasi hawa wanapofika kwenye ubongo, huushambulia na kusambaa kwa kasi ambapo uwezekano wa mgonjwa kupona huwa mdogo. Kati ya kila watu 100 wenye ugonjwa huo, karibu 30 hupoteza maisha.
DALILI ZA UGONJWA
Dalili za awali za ugonjwa huo ni kuwa na uvimbe mwekundu unaotokea kuzunguka macho ambao huongezeka kadiri fangasi wanavyozidi kushambulia ubongo.
Dalili nyingine ni pamoja na kuumwa kichwa upande mmoja, uso kuuma, homa kali, kupumua kwa shida na kutokwa kamasi za rangi nyeusi.Pia ngozi ya mwili wa mgonjwa huanza kubadilika rangi na kuwa nyekundu. Hali hiyo huendelea hadi ngozi inapobadilika zaidi na kuwa nyeusi.
TIBA
Vipimo vya ugonjwa huo hufanywa kwa mashine ya MRI ambapo mtu akibainika ameambukizwa fangasi hao, hutibiwa kwa upasuaji wa ubongo na kuondoa sehemu zilizoathirika pamoja na kutumia dawa kali za Amphotericin B au Posaconazole, wakati mwingine dawa hizi huchanganywa pamoja.
WATU WALIOPO KWENYE HATARI
Watu wanaoweza kuupata ugonjwa huu kwa urahisi ni wagonjwa wa kisukari, HIV, waliofanyiwa upasuaji wa kupandikiza viungo ndani ya miili yao kama figo au ini, na matumizi ya dawa za ‘corticosteroids’ kwa kipindi kirefu.
CHANZO: GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate