EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, March 26, 2015

JELA ILIVYOVUNJA UHUSIANO WA MASTAA BONGO


Jack Patrick, akiwa na mumewe wa ndoa, Abdulatif Fundikira.
Na Waandishi wetu
KATIKA ulimwengu wa wapendanao kuna changamoto nyingi ambazo wapenzi hukutana nazo huku wengine wakizishinda na baadhi kushindwa.
Wapo wapenzi walioshindwa kuendelea na uhusiano wao mara baada ya mmoja kuugua, kupata ulemavu na sababu nyingine nyingi, lakini wapo walioendelea kuvumiliana pamoja na sababu zote hizo na hatimaye penzi lao likazidi kuimarika na kuwa mfano katika jamii.
Hali hiyo haipo kwa watu wa kawaida peke yao bali hata kwa mastaa wetu wamejikuta wakiangukia katika mtihani huo na kushindwa kuhimili kusimamia mapenzi yao. Kifungo au jela ni moja ya sababu zinazosababisha ndoa au uhusiano wa mastaa wengi na wenza wao kuharibika.
Katika makala haya tunakuletea orodha ya baadhi ya mastaa ambao wamekumbwa na sakata hilo:-
Jack Patrick,

Mumewe na Jux
Jack Patrick ambaye aliwahi kushiriki Shindano la Miss Tanzania 2011, alijikuta akitiwa jela mwishoni mwa mwaka 2013 huko Macao, Hong Kong, China baada ya kudaiwa kukutwa na kete 66 za heroin. Wakati Jack anatumikia kifungo chake mumewe wa ndoa, Abdulatif Fundikira alidaiwa kushindwa kuvumilia na kumuoa kisiri Miss Tanzania 2011, Salha Israel hivyo kuhitimisha rasmi uhusiano wao.
Hata hivyo, wadadavuzi wa mambo walidai kuwa hiyo ilitokana na malipizi kwa kuwa hata wakati Abdulatif aliposwekwa lupango akihusishwa na ishu hiyohiyo ya madawa ya kulevya, Jack Patrick naye aliwahi kumsaliti kwa kutoka na msanii wa Bongo Fleva, Juma Mussa ‘Jux’.
Kajala na Mumewe.
Kajala na Mumewe
Kajala ni staa wa muvi ambaye sakata lake lilianza baada ya yeye na mumewe kuswekwa ndani kwa kosa la kutakatisha fedha na mashtaka mengine. Kajala alitakiwa kutoa faini ya shilingi milioni kumi na tatu (13) au kwenda jela miaka saba (7) huku mumewe, Faraja Chambo akienda jela kutumikia kifungo cha miaka 12 baada ya kushindwa kutoa faini ya shilingi milioni 213.  Ashukuruwe Wema Sepetu ambaye alimtoa Kajala kwa kulipa kiasi hicho cha fedha.
Akiwa uraiani, Kajala alidaiwa kushindwa kuvumilia kukaa na upweke na kukwaa skendo za mapenzi ikidaiwa kutoka na wanaume tofauti lakini kubwa ni ya kutoka na Kigogo mmoja (jina tunalihifadhi) anayetanua naye sehemu mbalimbali wakati mumewe akiozea jela bila msaada wowote kutoka kwake, japokuwa mara kadhaa amekuwa akimuomba Kajala amtoe.
Z. Anto akiwa na aliyekuwa mumewe Sandra.
Binti Kiziwi na Z. Anto
Baada ya kutoka na video ya Wimbo wa Binti Kiziwi, Mbongo Fleva, Z. Anto aliamua kumuoa binti aliyetumika katika video hiyo ‘video queen’ (Sandra Khan).
Hata hivyo, misukosuko ya ndoa yao ilianza baada ya kutimiza miaka mitatu ambapo Z. Anto na Sandra walitengana kwa kudai kuwa mkewe alikuwa akishirikiana na makundi mabaya. Uhusiano wao uliisha rasmi baada ya Sandra kunaswa mwanzoni mwa mwaka 2013 huko Hong Kong, China akiwa na ‘mzigo’. Katika moja ya mahojiano, Z. Anto alidai kuwa kwa sasa anaendelea na maisha yake na anatafuta msichana mwingine wa kuoa.
Aunt Ezekiel na Sunday Demonte.
Aunt Ezekiel na Sunday Demonte
Staa wa muvi, Aunt Ezekiel aliwashtusha watu baada ya kuolewa na Sunday Demonte, Mtanzania aishiye ughaibuni.
Habari zilidai kuwa mumewe huyo ameswekwa rumande jijini Abu Dhabi katika nchi za Falme za Kiarabu (UAE) kwa kesi ya madawa ya kulevya. Kama mastaa wengine, Aunt Ezekiel naye alishindwa kujizuia na kuchepuka na dansa wa Mbongo Fleva, Diamond Platnumz, Mose Iyobo na hatimaye kubeba mimba ambayo siyo ya mumewe Sunday.
Na CHANDE ABDALLAH NA DEOGRATIUS MONGELA

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate