EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, March 25, 2015

MCHUNGAJI, MKE WA MWANAJESHI LAIVU!

Waandishi wetu
DUNIA inaelekea mwisho. Mchungaji mmoja wa Kanisa la Pentekoste, raia wa Kenya aitwaye Pasca Mugambi hivi karibuni alinaswa chumbani ‘live’ katika gesti moja iliyopo Manzese Tip Top akiwa na mke wa askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) ambaye ni muunini wake, Risasi Mchanganyiko linakupa kisa kamili.
Mchungaji Pasca Mugambi akikosa la kufanya baada ya kufumaniwa.
TUJIUNGE NA CHANZO
Chanzo kilicho karibu na mke wa mjeshi huyo kilisema kuwa mchungaji huyo alikuwa akifanya shughuli zake za maombezi mjini Dodoma na kwamba askari huyo alimuita ili ampe huduma za kiroho mama yake mzazi aliye mgonjwa, baada ya kuwa amefahamishwa kwake na rafiki yake mmoja.
“Mchungaji huyo alikuwa akiishi sehemu nyingine hapa Dar lakini akienda kila siku nyumbani kwa mjeshi huyo kumfanyia maombi mama yake. Sasa akiwa pale akavutiwa na mke wa jamaa akaanza kumtongoza, ikiwa ni pamoja na kumtumia picha zake mbalimbali za utupu, (tunazo),” kilisema chanzo hicho.
 

MKE ‘AMCHOMA’ MCHUNGAJI
Inadaiwa kuwa kitendo cha kutongozwa na mchunga kondoo huyo hakikumpendeza mwanamke huyo, ambaye aliamua kulifikisha suala hilo kwa mumewe ili wajue cha kufanya.
MJESHI AANDAA ADHABU NYEPESI
Chanzo chetu kinadai kuwa mwanaume huyo mwenye cheo jeshini, alimwambia mkewe kuwa asingependa kumuadhibu mchungaji huyo kwa kutumia cheo chake, badala yake akataka kushirikishwa kwa makamanda wa kitengo maalum cha Operesheni Fichua Maovu (OFM) cha Global Publishers.
MJESHI AMWAGA UBUYU KWA OFM
“Huyu mchungaji nilimtoa Dodoma baada ya kupewa namba zake na rafiki yangu mmoja ili aje kumuombea mama yangu ambaye ni mgonjwa, lakini sasa namshangaa amepeleka maombi mengine kwa mke wangu, anamsumbua sana kuwa anampenda, nataka nimkomeshe ili iwe fundisho kwa wachungaji wengine wenye tabia kama yake,” mjeshi huyo aliwaambia makamanda wa OFM kwa njia ya simu.
MCHUNGAJI AINGIZWA KINGI
Baada ya kukubaliana na mumewe juu ya kumkomesha mkware huyo, mke alikubali ombi la mchungaji huyo (huku moyoni akiwa na lake jambo), mchungaji naye bila hiyana akajaa na kumuomba mwanamke huyo wakutane katika gesti hiyo tayari kwa kuivunja amri ya sita ya Mungu iliyo katika kitabu kitakatifu cha Biblia.
Mchungaji Pasca akiwa na muumini wake aliyenaswa nae.
MCHUNGAJI ATANGULIA GESTI
Akiwa na uchu, mchungaji huyo alitangulia ndani ya gesti hiyo (jina lake linahifadhiwa kwa sababu za kibiashara) na kupewa chumba namba 103 na kumtaarifu ‘bibie’ kuwa alikuwa tayari amefika.

MJESHI ABANA CHOBINGO
Wakati mawasiliano hayo yakifanywa, mjeshi huyo alikuwa na mkewe ‘chobingo’ wakiwasubiri makamanda wa OFM ambao walipoungana nao, mume huyo aliwatambulisha kwa mkewe na kuwapa mchongo mzima.
UTAMBULISHO WA FASTAFASTA
“Huyu ndiye mke wangu ambaye anasumbuliwa sana na huyo mchungaji, tulikuwa tunawasubiri mfike ili yeye aende chumbani kwa sababu tayari mchungaji ameshafika na anamsubiri,” alisema mjeshi huyo ambaye jina lake linahifadhiwa kwa sababu maalum.
MWENYEKITI WA MTAA AITWA
Ili kwenda kisheria zaidi, OFM ilimtafuta Mwenyekiti wa Serikali wa mtaa huo aliyejitambulisha kwa jina moja la Mzee Mushi na kumpa mkanda kamili ambapo alikubali kutoa ushirikiano ikiwa ni pamoja na mmiliki wa gesti hiyo.
MCHUNGAJI AKUTWA NA BUKTA
Katika kundi lililowajumuisha wote hao, walifika chumbani hapo baada ya muda mfupi wa kusubiri na walipogonga, mlango ulifunguliwa na kuwakuta wawili hao wakiwa wamekaa kitandani na tayari wameshavua nguo zao za juu, mchungaji akiwa na bukta na fulana.“Mh! Hii ni aibu jamani yaani mchungaji kukutwa katika hali hii, waumini wataiga nini kwake?” alihoji mhudumu mmoja wa gesti hiyo.Akivaa baada ya fumanizi hilo.
ETI ALIKWENDA KUFANYA MAOMBI
Alipoulizwa na mwenyekiti sababu za kuwepo na mke wa mtu anayefahamiana naye, yeye akiwa mtumishi wa Mungu, mchungaji huyo alijibu kuwa aliombwa na dada huyo kumfanyia maombi.“Jamani naomba mnisamehe, shetani alinitangulia nilitaka kufanya maombi humu ndani,” alisema kwa kigugumizi mchungaji huyo.
MJESHI AMSAMEHE MCHUNGAJI
Katika hali ya ujasiri mkubwa, mjeshi huyo alimchukua mkewe na kumsamehe mchungaji huyo, lakini akamuonya kuachana na mchezo huo kwani anaweza kupoteza maisha yake.

Stori: Issa Mnally, Imelda Mtema na Hamida Hassan.
CHANZO: GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate