EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, March 20, 2015

MGOMBEA URAIS UKAWA YUPO CCM

WAKATI joto likizidi kupanda kuhusu nani atapeperusha bendera ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi mkuu ujao, siri imevuja kuwa upande wa pili, yaani upinzani unaoundwa na vyama vinavyojinasibu kuwa ni Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) utamsimamisha mgombea wake ambaye kwa sasa ni kada mwenye wafuasi wengi ndani ya CCM, Uwazi Mizengwe linakujuza.
Steven Wassira.
Habari za kuaminika kutoka ndani ya kambi ya Ukawa inayoundwa na vyama vya Chadema, Cuf, NCCR-Mageuzi na NLD, zinasema kwa muda mrefu, mgombea huyo amekuwa katika mazungumzo na chama kimoja kikubwa cha upinzani Tanzania Bara na kwamba wameshakubaliana mambo makubwa muhimu ya kuzingatiwa ili kukamilisha mchakato huo.
Inadaiwa kuwa awali mazungumzo yalikuwa kati ya Chadema na kada huyo wa CCM ambaye ni miongoni mwa viongozi waliopewa adhabu na kamati kuu (CC) ya chama hicho kwa kosa la kuanza mapema kampeni za kuwania kiti hicho, wakifikia makubaliano kuwa endapo chama chake kitamuengua katika kuwania nafasi hiyo, basi afanye hivyo kupitia chama hicho lakini kwa sharti la kugawana vyeo yeye na wafuasi atakaoondoka nao.

“Kambi ya kada huyo ina hofu ya mzee wao kukatwa kutokana na mizengwe inayosukwa na wapinzani wake ndani ya chama. Kwa kuwa ni lazima mtu wao awanie urais, basi wameamua kuweka mbadala. Vikao vimefanyika na walifikia hatua nzuri kwa sababu wanaamini endapo mgombea huyo ataondoka CCM na kujiunga kule wana uhakika wa kupata kura nyingine zikitoka hata kwa wafuasi wa chama hicho tawala,” alisema mtoa habari wetu.
Inadaiwa kuwa awali, kulikuwa na hofu ya mpango huo kuharibika baada ya Chadema kujiunga na vyama vingine vya upinzani na kuunda Ukawa, ambao wametangaza kumweka mgombea mmoja atakayekubaliwa na pande zote, lakini imeelezwa kuwa mazungumzo yanaendelea na upo uwezekano mkubwa wa mpango huo kukubaliwa na viongozi wa vyama vingine kutokana na nguvu kubwa ya ushawishi iliyonayo chama hicho.
“Kwa jinsi alivyo na wafuasi wengi ndani ya CCM na vuguvugu la mabadiliko linalosubiri uchaguzi wa mwaka huu, kuna uwezekano mkubwa wa kushinda kupitia Ukawa. Kada huyo ametaka kuwekewa nafasi kadhaa katika serikali itakayoundwa na makubaliano yamefikiwa juu ya vyeo ambavyo watu wa Ukawa watapata katika serikali inayotarajiwa kuundwa,” kilisema chanzo hicho.
Kwa mujibu wa mtoa habari wetu, baadhi ya nafasi ambazo Ukawa wametaka kupewa ni ile ya mgombea mwenza (atakayekuwa makamu wa rais), waziri mkuu, wizara ya fedha, wizara ya sheria, wizara ya mambo ya ndani, wizara ya ulinzi, wizara ya nishati na madini, wizara ya ujenzi na uchukuzi pamoja na nyingine nyeti ambazo zinadaiwa kuwa ndiyo uti wa mgongo wa uchumi wa nchi.
“Wanaamini wakizikamata wizara hizo, basi wanao uwezo wa kubadilisha mambo na hivyo kuonesha tofauti kati ya uongozi wao na ule wa CCM. Ninavyokueleza hivi, vikao bado vinaendelea kwa sababu kila upande unataka kujiridhisha kabla ya kufikia makubaliano rasmi,” kilisema chanzo hicho.
Juzi, Uwazi Mizengwe lilimtafuta Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Tanzania Bara, John Mnyika kupitia simu yake ya mkononi na kumuuliza kuhusu mipango hiyo lakini alikataa katakata kuwepo kwa suala hilo akidai ni uvumi ambao hauna ukweli wowote.
“Huo uvumi hauna ukweli, mgombea wa Ukawa atatoka Ukawa. Wananchi wana imani na Ukawa na siyo mtu kutoka chama kilichoshindwa kujivua magamba ya ufisadi na kuwa chama cha mafisadi,” alisema Mnyika ambaye pia ni mbunge wa Ubungo kwa tiketi ya Chadema.
Alipoulizwa kama Ukawa watakuwa tayari kumpokea kada wa CCM mwenye wafuasi wengi kwa kigezo cha kuongezewa kura katika uchaguzi huo na kumpa nafasi ya kuwania urais, Mnyika alisema milango ipo wazi kwa kiongozi yeyote mwenye maono na maadili ambaye atakuwa tayari kumuunga mkono mgombea atakayeteuliwa na Ukawa, siyo mwenye uzoefu wa ufisadi na uongozi mbovu.
“Tayari Ukawa ina wafuasi wengi ambao wakiungana na wananchi wengine wasio na vyama lakini wapenda mabadiliko wanatosha kuiondoa CCM madarakani, lakini kama yupo mwenye maono na maadili aliye tayari kujiunga na Ukawa toka CCM ili kuongeza kura za mabadiliko aje, lakini nasisitiza, awe na uadilifu na uwezo siyo uzoefu wa ufisadi.”
Kwa upande wake, Katibu wa Itikadi, Uenezi wa Halmashauri Kuu ya CCM, Nape Moses Nnauye alipoulizwa juu ya suala hilo alipuuza na kusema ni porojo za mtaani ambazo CCM haishughuliki nazo.
Makada wa CCM wanaotajwa kuwa na nguvu katika chama hicho ambao pia wanatumikia adhabu ya kuanza kampeni mapema ni pamoja na Emanuel Nchimbi, Edward Lowassa, William Ngeleja, January Makamba, Steven Wassira na Bernard Membe. Wengine ambao hawako kwenye adhabu ni Mizengo Pinda, Hamis Kingwangalla na Lazaro Nyalandu.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate