WAKATI joto likizidi kupanda kuhusu nani atapeperusha bendera 
ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi mkuu ujao, siri imevuja 
kuwa upande wa pili, yaani upinzani unaoundwa na vyama vinavyojinasibu 
kuwa ni Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) utamsimamisha mgombea wake 
ambaye kwa sasa ni kada mwenye wafuasi wengi ndani ya CCM, Uwazi 
Mizengwe linakujuza.
Habari za kuaminika kutoka ndani ya kambi ya Ukawa inayoundwa na 
vyama vya Chadema, Cuf, NCCR-Mageuzi na NLD, zinasema kwa muda mrefu, 
mgombea huyo amekuwa katika mazungumzo na chama kimoja kikubwa cha 
upinzani Tanzania Bara na kwamba wameshakubaliana mambo makubwa muhimu 
ya kuzingatiwa ili kukamilisha mchakato huo.
Inadaiwa kuwa awali mazungumzo yalikuwa kati ya Chadema na kada huyo 
wa CCM ambaye ni miongoni mwa viongozi waliopewa adhabu na kamati kuu 
(CC) ya chama hicho kwa kosa la kuanza mapema kampeni za kuwania kiti 
hicho, wakifikia makubaliano kuwa endapo chama chake kitamuengua katika 
kuwania nafasi hiyo, basi afanye hivyo kupitia chama hicho lakini kwa 
sharti la kugawana vyeo yeye na wafuasi atakaoondoka nao.
“Kambi ya kada huyo ina hofu ya mzee wao kukatwa kutokana na mizengwe
 inayosukwa na wapinzani wake ndani ya chama. Kwa kuwa ni lazima mtu wao
 awanie urais, basi wameamua kuweka mbadala. Vikao vimefanyika na 
walifikia hatua nzuri kwa sababu wanaamini endapo mgombea huyo ataondoka
 CCM na kujiunga kule wana uhakika wa kupata kura nyingine zikitoka hata
 kwa wafuasi wa chama hicho tawala,” alisema mtoa habari wetu.
Inadaiwa kuwa awali, kulikuwa na hofu ya mpango huo kuharibika baada 
ya Chadema kujiunga na vyama vingine vya upinzani na kuunda Ukawa, ambao
 wametangaza kumweka mgombea mmoja atakayekubaliwa na pande zote, lakini
 imeelezwa kuwa mazungumzo yanaendelea na upo uwezekano mkubwa wa mpango
 huo kukubaliwa na viongozi wa vyama vingine kutokana na nguvu kubwa ya 
ushawishi iliyonayo chama hicho.
“Kwa jinsi alivyo na wafuasi wengi ndani ya CCM na vuguvugu la 
mabadiliko linalosubiri uchaguzi wa mwaka huu, kuna uwezekano mkubwa wa 
kushinda kupitia Ukawa. Kada huyo ametaka kuwekewa nafasi kadhaa katika 
serikali itakayoundwa na makubaliano yamefikiwa juu ya vyeo ambavyo watu
 wa Ukawa watapata katika serikali inayotarajiwa kuundwa,” kilisema 
chanzo hicho.
Kwa mujibu wa mtoa habari wetu, baadhi ya nafasi ambazo Ukawa 
wametaka kupewa ni ile ya mgombea mwenza (atakayekuwa makamu wa rais), 
waziri mkuu, wizara ya fedha, wizara ya sheria, wizara ya mambo ya 
ndani, wizara ya ulinzi, wizara ya nishati na madini, wizara ya ujenzi 
na uchukuzi pamoja na nyingine nyeti ambazo zinadaiwa kuwa ndiyo uti wa 
mgongo wa uchumi wa nchi.
“Wanaamini wakizikamata wizara hizo, basi wanao uwezo wa kubadilisha 
mambo na hivyo kuonesha tofauti kati ya uongozi wao na ule wa CCM. 
Ninavyokueleza hivi, vikao bado vinaendelea kwa sababu kila upande 
unataka kujiridhisha kabla ya kufikia makubaliano rasmi,” kilisema 
chanzo hicho.
Juzi, Uwazi Mizengwe lilimtafuta Naibu Katibu Mkuu wa Chadema 
Tanzania Bara, John Mnyika kupitia simu yake ya mkononi na kumuuliza 
kuhusu mipango hiyo lakini alikataa katakata kuwepo kwa suala hilo 
akidai ni uvumi ambao hauna ukweli wowote.
“Huo uvumi hauna ukweli, mgombea wa Ukawa atatoka Ukawa. Wananchi 
wana imani na Ukawa na siyo mtu kutoka chama kilichoshindwa kujivua 
magamba ya ufisadi na kuwa chama cha mafisadi,” alisema Mnyika ambaye 
pia ni mbunge wa Ubungo kwa tiketi ya Chadema.
Alipoulizwa kama Ukawa watakuwa tayari kumpokea kada wa CCM mwenye 
wafuasi wengi kwa kigezo cha kuongezewa kura katika uchaguzi huo na 
kumpa nafasi ya kuwania urais, Mnyika alisema milango ipo wazi kwa 
kiongozi yeyote mwenye maono na maadili ambaye atakuwa tayari kumuunga 
mkono mgombea atakayeteuliwa na Ukawa, siyo mwenye uzoefu wa ufisadi na 
uongozi mbovu.
“Tayari Ukawa ina wafuasi wengi ambao wakiungana na wananchi wengine 
wasio na vyama lakini wapenda mabadiliko wanatosha kuiondoa CCM 
madarakani, lakini kama yupo mwenye maono na maadili aliye tayari 
kujiunga na Ukawa toka CCM ili kuongeza kura za mabadiliko aje, lakini 
nasisitiza, awe na uadilifu na uwezo siyo uzoefu wa ufisadi.”
Kwa upande wake, Katibu wa Itikadi, Uenezi wa Halmashauri Kuu ya CCM,
 Nape Moses Nnauye alipoulizwa juu ya suala hilo alipuuza na kusema ni 
porojo za mtaani ambazo CCM haishughuliki nazo.
Makada wa CCM wanaotajwa kuwa na nguvu katika chama hicho ambao pia 
wanatumikia adhabu ya kuanza kampeni mapema ni pamoja na Emanuel 
Nchimbi, Edward Lowassa, William Ngeleja, January Makamba, Steven 
Wassira na Bernard Membe. Wengine ambao hawako kwenye adhabu ni Mizengo 
Pinda, Hamis Kingwangalla na Lazaro Nyalandu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
HABARI MBALIMBALI
‘Dk. Cheni’
‘Sharo Milionea
‘Thea’
African Women
AGNESS MASOGANGE
AK CLASSIC COSMETICS
ALI KIBA
Amanda Poshy
Ant
ANT LULU
Ashley Toto
Aunt Ezekiel
Aunty Ezekiel
AUNTY LULU
Azam Fc
Baby Madaha
BAHATI BUKUKU
Barnaba
BATULI
BBA
Beauty of the day
Belle 9
BI KIDUDE
BIBI BOMBA
Big Brother
Big Brother Africa
Bill Gates
BINTI KIZIWI
BOB JUNIOR
Bodi ya Filamu
Bongo Movie
Bongo Movies
CCM
CHADEMA
Chombezo
Christina Shusho
Chuchu hans.
Clouds Media Group
Club Bilicanas
DAR LIVE
DAVINA
Dayna Nyange
Diamond
Dida
Diva Loveness Love
Dj Ommy Crazy wa Maisha Club
DOGO JANJA
DOKI
DR.CHENI
DSTV
Dude
Dully Sykes
EBSS 2013
Elizabeth Michael
Epiq Bongo Star Search (EBSS)
ESHA BUHETI
Ester Bulaya
Feza Kessy
FIESTA 2014
Flaviana Matata
FLORA MBASHA
FLORA MVUNGI
Francis Cheka
GARDNER
GLOAL PUBLISHERS
GLOBAL TV ONLINE
H. BABA
Halima Mdee
HAMISA
Happy birthday
Hemedi
Hemedy Suleiman
HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE
Hoyce Temu
Huddah Monroe
HUSINA
IRENE PAUL
Irene Uyoya
ISABELLA
J film 4 life
Jack Chuz
JACK PATRICK
Jacob Steven ‘JB’
Jacqueline Dustan
JACQUELINE WOLPER
Jaji Khamis 'Kashi'
Jay Dee
JENNIFER KYAKA (ODAMA)
JIDE
JINI KABULA
JK
JO
Johari
Jokate Mwigelo ‘Kidot’.
JOTI
Joyce Kiria
Joyce Kiwia
JUX
K-LYNN
KADINDA
kaja
Kajala Masanja
Kapotive Star Singers
KATUNI
Kemmy
Kero Zetu
KHADIJA OMAR KOPA
KIKWETUKWETU
KILI MUSIC AWARDS
KOLETA
Lady Jay Dee
Lady Jaydee
Lake Oil
LAVEDA
Linah Sanga
Linex
Lisa Jensen
Loveness Diva
Lucy Francis Komba
Lulu
M2 The P
MABILIONEA
Madam Rita
MADELA
Magazeti
Mahusiano
Maimartha Jesse
MAINDA
MAISHA
Makala
Malkia Elizabeth
MAMTEI
MANDELA
MARIAM ISMAIL
Masanja Mkandamizaji
Mashindano ya Miss Tanzania
Matangazo
Matonya
MaxMalipo
MAYA
MELLIS EDWARD
MENINAH
MGOSI MKOLONI
Mh Halima Mdee
mic
Michezo
MILLEN HAPPINESS MAGESE
MISS CHANG'OMBE
MISS DAR CITY CENTER
Miss East Africa
MISS REDD'S IRINGA 2013
MISS TANGA 2013.
MISS TANZANIA 2014
Miss Tanzania mwaka 2011
MISS TEMEKE 2014
MISS USTAWI
MISS UTALII TANZANIA 2012/13
Miss vyuo vikuu 2013
MKALA
MREMBO HUDDAH
Mrisho Mpoto
Mrisho Ngassa
MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES.
MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013
Mtitu
muziki
Mwana FA
MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14
Mzee Majuto
Nancy Sumari
Nani Mtani Jembe?
NAPE
Nassoro ‘Nora’
Natasha
Nay wa Mitego
Necta
Nelly Kamwelu
NEY WA MITEGO
Nisha
NSSF;Zantel
Nyamwela
NYimbo
Nyota  yako
OBAMA TANZANIA
OMMY DIMPOZ
P FUNK
PAM D
Peniel Mgilwa ‘Penny’
PETIT MAN
Profesa Jay
Q - CHILA
Q Boy
Q Chilla
QUEEN DARLEEN
RACHEL NDAUKA
RAIS KIKWETE
Rais Kikwete.
Rasimu Ya Katiba TZ
Ray
Ray C
Redd’s Miss IFM
REDD'S MISS KAGERA 2013
REDD'S MISS TZ
REDDS MISS TANZANIA 2014
Redds Miss wa Mikoa
REHEMA FABIAN
RICHIE RICHIE
Rihanna
ROSE MUHANDO
Rose Ndauka
Ruge Mutahaba.
SABASABA 2013
Saida Karoli
Saikolojia
Sajeti
SAJUKI
Sandra
SHAA
Shamsa Ford
Sheikh Ponda
Shilole
Sintah
Siwema
Skin Tricks
Snura Mushi
Spika Makinda
staa
Staa Wetu
Stella Mwangi
STYLE ZA NYWELE
Taifa Stars
Tamasha la matumaini
TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013
Tangazo
TANZANIA
TEGO
TENGENEZA WEBSITE NA BLOG
TID
Tundaman
Tupo wangapi?
TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14
Twanga Pepeta
USA PAGEANT 2014
VAI
Wastara
WEMA
WEMA SEPETU
Yanga
Yanga Bingwa 2013
YOUNG D
Yvonne Cherry ‘Monalisa’
Z Anton.
Zari
Zito kabwe

No comments:
Post a Comment