EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, April 9, 2015

LULU, MAMA KANUMBA WAFIKA PABAYA

HALI ni mbaya! Staa wa sinema za Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ na mama wa aliyekuwa nyota wa fani hiyo, Steven Kanumba, Flora Mtegoa wamefikia pabaya baada ya mama huyo kumshushia Lulu maneno  makali na ya shutuma, Amani lina taarifa.
Staa wa sinema za Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’.
Habari zilizojiri ndani ya chumba cha habari cha gazeti hili zinadai kuwa, mama Kanumba amemlalamikia Lulu kwamba, amemtupa na kumtenga tofauti na zamani ambapo uhusiano wao ulikuwa kama wa mama na binti yake.
“Jamani habari nzito kwa sasa ni mama Kanumba na Lulu. Mama Kanumba anamshutumu Lulu kwa kumtenga. Anasema ni miezi mitano sasa Lulu hajafika nyumbani kwake wala kuwasiliana naye kwa simu,” kilisema chanzo kimoja.
Kikaendelea: “Hivi kesho (Jumanne iliyopita), ni Kanumba Day. Imepangwa kufanyika Dar West (Dar), inawezekana Lulu asiende au Mama Kanumba asiende. Lakini hata kama watakwenda na wakakutana, watachekeana kwa jino pembe lakini uhusiano wao si mzuri jamani.”
Mama Kanumba akilia peke yake kaburini.
MAMA KANUMBA ATAFUTWA
Ili kupata usahihi wa madai hayo, Amani lilimsaka mama Kanumba kwa njia ya simu ambapo alipopatikana alikuwa na haya ya kusema:“Lulu si Lulu yule jamani. Lulu sasa hivi amebadilika. Awali aliniambia hatanitupa, lakini sivyo. Lulu siku hizi haji kunisalimia wala hanipigii simu.”

ANACHOAMINI YEYE
“Imefika mahali nawaza kwamba, huenda alipenda Kanumba aondoke ili yeye apate mafanikio makubwa aliyonayo sasa. Lulu amenitenga, amenitenga, amenitenga!”
MANENO YA MAMA KANUMBA KABURINI KWA KANUMBA
Juzi, Jumanne, ambayo ilikuwa siku ya kuadhimisha mwaka wa tatu tangu kifo cha staa huyo, mama huyo alishiriki kwa kwenda kwenye Makaburi ya Kinondoni jijini Dar kwa lengo la kusafisha kaburi la mtoto wake. Baada ya zoezi la kusafisha kaburi kumalizika, mama Kanumba aliongea na Amani na kuyasema haya:
“Nasikitika sana namna ambavyo Lulu amekuwa tofauti na maneno yake ya zamani kwamba atakuwa sambamba na mimi katika kuadhimisha kumbukumbu ya Kanumba. Lakini leo kama hivi, hajatokea.
“Pia nasikitishwa na kitendo cha kufanya bethidei ya mdogo wake jana (Jumatatu usiku) kule Posta wakati anajua ndiyo usiku ambao Kanumba alifariki dunia.
Mama Kanumba akiwa na simanzi kubwa.
“Mbaya zaidi, akiulizwa na watu kwa nini sasa hivi hayupo sambamba na mimi kama zamani, anajibu majibu ambayo hayaeleweki. Kumbe maneno yake ya zamani kwamba atakuwa sambamba na mimi yalikuwa ya usaliti.
“Kwa hiyo na mimi sasa nimeamua kubaki peke yangu kama nilivyo, nitaendelea kumuenzi Kanumba mwanangu kwa sababu mimi ndiyo mama yake kwa hiyo nalia peke yangu.”
LULU ALITOA AHADI YA UONGO
Katika mazungumzo yake, mama Kanumba alikwenda mbali zaidi kwa kusema: “Kuna siku aliahidi kwamba atajengea picha ya Kanumba ikiwa ndani ya kioo na kuiweka juu ya kaburi, hajafanya hivyo. Nitafanya mwenyewe.“Labda amepuuza kwa vile anajiona anazidi kukua kisanii, ni supastaa ndiyo maana anatoa ahadi za uongo.”
ALICHOKISEMA LULU SASA
Lulu alipotafutwa juzi ili kuzungumzia malalamiko ya mama mkwe wake huyo, hakupatikana lakini wiki iliyopita alizungumza na paparazi wetu kuhusu mtazamo wa maisha yake kwa jumla ambapo alisema:“Mimi kwa sasa hivi nina mtazamo mwingine kabisa kuhusu maisha. Kwanza sidhani kama nitamwaga machozi tena kuhusu Kanumba maana nimelia sanasana.“Mtu ambaye naweza kumlilia ni mama yangu (Lucresia Karugila) na mdogo wangu. Lakini si mtu mwingine. Kwa sasa naangalia zaidi familia yangu.”
Marehemu Steven Kanumba enzi za uhai wake.
TUJIKUMBUSHE KIDOGO
Kanumba alifariki dunia Aprili 7, 2012 kwa kuanguka katika mazingira yaliyodaiwa yalitokana na ugomvi kati yake na Lulu. Tukio hilo lilitokea nyumbani kwa Kanumba, Sinza ya Vatcan, Dar.
Baada ya kifo hicho, Lulu alikamatwa na kuwekwa mahabusu ya Segerea jijini Dar na baadaye kuachiwa kwa dhamana.
Baada ya kutoka mahabusu, yeye na mama yake walimfuata mama Kanumba na kuomba msamaha ambapo mama huyo aliupokea na kusema anamwona Lulu kama mtoto wake na yote ya nyuma yamepita. Kuanzia hapo, Lulu na mama Kanumba wamekuwa na ukaribu wa kindugu huku kila mwaka wakifanya kumbukumbu ya Kanumba pamoja.
Katika kumbukumbu ya juzi, Lulu hakutokea  na mama Kanumba alisema hajapewa taarifa yoyote. Lulu alipotafutwa kwa simu ili kumsikia anasema nini kuhusu kutotokea makaburini, hakuwa hewani!
CHANZO: GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate