LICHA ya Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na
Uzima, Josephat Gwajima kukanusha mara zote kwamba, hahusiki na
kusambaratika kwa ndoa ya Mwimba Injili Flora Mbasha na mumewe, Emmanuel
Mbasha, lakini mume huyo ambaye amekuwa akimshutumu Gwajima ameibuka na
jipya, Amani linakupa zaidi.Mwimba Injili Flora Mbasha na mumewe, Emmanuel Mbasha
Jipya aliloibuka nalo Mbasha ni kudai kuwa, msala uliompata Mchungaji
Gwajima wa kumtolea maneno yenye kuudhi Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo
Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycap Kadinali Pendo na kisha kuhojiwa
polisi na kupata mshtuko, kuzimia hadi kulazwa hospitali ni malipo ya
Mungu kwake kutokana na kilio chake.
ATUMIA DAKIKA 15
Akizungumza na Amani kwa njia ya simu kwa dakika 15 juzi, Mbasha
alisema: “Ile hali (kupoteza fahamu) ya Gwajima ni malipo. Mimi
nilishasema jamani, mtu akikutendea ubaya malipo ni hapahapa duniani,
hakuna kwingine.
“Mimi ndoa yangu haipo, mke wangu anajua yeye anavyoishi. Kwa hivyo
mimi nimekuwa nikiishi kwa manung’uniko kila siku, unadhani nini
kitatokea kwake?”
AMTAKA AKAMWOMBE MSAMAHA
Mbasha alikwenda mbele zaidi kwa kutoa tamko na agizo kwa mchungaji huyo kwa kusema:
“Tena namwomba Mungu ampe afya Gwajima, akitoka hospitali alikolazwa (TMJ, Dar) anitafute kuniomba msamaha.
“Ni vyema na itakuwa vyema zaidi akinitafuta na kuniomba msamaha ili
kila mmoja aishi kwa amani. Mimi nisiwe na kinyongo na yeye na wala yeye
asiwe na kinyongo na mimi.”
KUHUSU ALICHOKIONGEA GWAJIMA
Mbasha hakumalizia hapo, alipoulizwa kama kauli ya Gwajima iliyosababisha mtafaruku ilikuwa sawasawa au la! Mbasha alisema:
“Hilo atajua yeye mwenyewe na Mungu wake, mimi sijui. Ila ninachojua
mimi ni kitu kimoja tu, kwamba Mungu amenilipia basi, sasa aniombe
msamaha.”
MCHUNGAJI WA GWAJIMA ANENA
Naye mchungaji mmoja wa kanisa la Gwajima alipopatikana kwa simu na
kuulizwa kuhusu madai ya Mbasha, alisema: “Yule hajui maandiko sawasawa.
Hakuna uhusiano wowote kati ya kilichompata mchungaji wangu na hisia
zake kuhusu mkewe Flora.
“Gwajima na Flora hawana uhusiano wowote usiofaa. Sasa yeye anaposema
kalipiwa, kalipiwa kitu gani? Mungu anaweza kulipa jambo la hisia?”
WANACHOAMINI WENGINE
Mbali na Mbasha, baadhi ya wasomaji wa gazeti hili walisema kwamba,
wanamwamini Mchungaji Gwajima ni miongoni mwa watumishi wa Mungu
waliojaliwa hekima hivyo kauli aliyoitoa yenye maneno yenye kuudhi
huenda ulikuwa mpango maalum wa roho chafu aseme yale ili yamkute
yaliyomkuta na kujifunza kitu.
“Gwajima ana hekima bwana. Ni Mchungaji mwenye kujitambua, yale
maneno aliyomsema Askofu Pengo lazima ni mpango wa roho chafu, pale
Gwajima ana kitu cha kujifunza.
“Mimi sisemi kama alichokutananacho ni kwa sababu ya ‘maombi’ ya
Mbasha kwa Mungu wake, ila nasema Gwajima ana kitu cha kujifunza kwa
matamshi yake na mazingira ya utumishi pia,” alisema Johnson Mwaduma,
mkazi wa Mwananyamala, Dar.
WITO KWA SERIKALI
Kufuatia manenomaneno ya chini kwa chini kwamba, huenda serikali
ikalifungia kanisa lake lililopo Kawe jijini Dar, baadhi ya wasomaji
waliitaka serikali kutofikiria kufanya hivyo kwani Gwajima ni mchungaji
mwenye waumini wengi sana nchini.
“Yule ana makanisa nchi nzima, sasa serikali ikisema ilifungie kanisa
lake ina maana waumini maelfu kwa maelfu watarudi nyuma kiroho na
matokeo yake ni kuanza kupata watu watenda maovu.
“Lazima ikumbukwe kwamba, mchungaji anapowahubiria waumini wake
kutenda mema, kuacha dhambi pia anaisaidia serikali katika kupambana na
maovu.
“Halafu yule Gwajima mwenyewe ni mchungaji wa kweli, ana imani, ana
nguvu ya kiroho, amesaidia wengi kimwili na kiroho pia. Anatakiwa
kuendelea kutiwa moyo kwa vile ni mtu mwongofu,” alisema Simon Salele,
mkazi wa Sinza D, Dar es Salaam.
TUJIKUMBUSHE
Wiki mbili zilizopita, kwenye Viwanja vya Tanganyika Perkers ambako
kuna kanisa, Gwajima alitoa mahubiri yaliyolenga kumshutumu Kadinali
Pengo kwa kitendo chake cha kwenda kinyume na maazimio ya Baraza la
Maaskofu Tanzania kuhusu msimamo wao wa Mahakama ya Kadhi nchini.
Hali hiyo ilimfanya Gwajima kuitwa Polisi Kituo cha Kati, Dar na
kuhojiwa. Akiwa katika mahojiano, ghafla alisikia kizunguzungu,
akaanguka na kupoteza fahamu. alikimbizwa katika Hospitali ya Polisi
Baracks kisha Hospitali ya TMJ, Dar kwa matibabu zaidi.
Juzi, Gwajima aliruhusiwa kutoka hospitalini hapo lakini akachukuliwa
hadi Kituo cha Polisi Oysterbay kwa mahojiano zaidi na kuachiwa kwa
dhamana.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
HABARI MBALIMBALI
‘Dk. Cheni’
‘Sharo Milionea
‘Thea’
African Women
AGNESS MASOGANGE
AK CLASSIC COSMETICS
ALI KIBA
Amanda Poshy
Ant
ANT LULU
Ashley Toto
Aunt Ezekiel
Aunty Ezekiel
AUNTY LULU
Azam Fc
Baby Madaha
BAHATI BUKUKU
Barnaba
BATULI
BBA
Beauty of the day
Belle 9
BI KIDUDE
BIBI BOMBA
Big Brother
Big Brother Africa
Bill Gates
BINTI KIZIWI
BOB JUNIOR
Bodi ya Filamu
Bongo Movie
Bongo Movies
CCM
CHADEMA
Chombezo
Christina Shusho
Chuchu hans.
Clouds Media Group
Club Bilicanas
DAR LIVE
DAVINA
Dayna Nyange
Diamond
Dida
Diva Loveness Love
Dj Ommy Crazy wa Maisha Club
DOGO JANJA
DOKI
DR.CHENI
DSTV
Dude
Dully Sykes
EBSS 2013
Elizabeth Michael
Epiq Bongo Star Search (EBSS)
ESHA BUHETI
Ester Bulaya
Feza Kessy
FIESTA 2014
Flaviana Matata
FLORA MBASHA
FLORA MVUNGI
Francis Cheka
GARDNER
GLOAL PUBLISHERS
GLOBAL TV ONLINE
H. BABA
Halima Mdee
HAMISA
Happy birthday
Hemedi
Hemedy Suleiman
HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE
Hoyce Temu
Huddah Monroe
HUSINA
IRENE PAUL
Irene Uyoya
ISABELLA
J film 4 life
Jack Chuz
JACK PATRICK
Jacob Steven ‘JB’
Jacqueline Dustan
JACQUELINE WOLPER
Jaji Khamis 'Kashi'
Jay Dee
JENNIFER KYAKA (ODAMA)
JIDE
JINI KABULA
JK
JO
Johari
Jokate Mwigelo ‘Kidot’.
JOTI
Joyce Kiria
Joyce Kiwia
JUX
K-LYNN
KADINDA
kaja
Kajala Masanja
Kapotive Star Singers
KATUNI
Kemmy
Kero Zetu
KHADIJA OMAR KOPA
KIKWETUKWETU
KILI MUSIC AWARDS
KOLETA
Lady Jay Dee
Lady Jaydee
Lake Oil
LAVEDA
Linah Sanga
Linex
Lisa Jensen
Loveness Diva
Lucy Francis Komba
Lulu
M2 The P
MABILIONEA
Madam Rita
MADELA
Magazeti
Mahusiano
Maimartha Jesse
MAINDA
MAISHA
Makala
Malkia Elizabeth
MAMTEI
MANDELA
MARIAM ISMAIL
Masanja Mkandamizaji
Mashindano ya Miss Tanzania
Matangazo
Matonya
MaxMalipo
MAYA
MELLIS EDWARD
MENINAH
MGOSI MKOLONI
Mh Halima Mdee
mic
Michezo
MILLEN HAPPINESS MAGESE
MISS CHANG'OMBE
MISS DAR CITY CENTER
Miss East Africa
MISS REDD'S IRINGA 2013
MISS TANGA 2013.
MISS TANZANIA 2014
Miss Tanzania mwaka 2011
MISS TEMEKE 2014
MISS USTAWI
MISS UTALII TANZANIA 2012/13
Miss vyuo vikuu 2013
MKALA
MREMBO HUDDAH
Mrisho Mpoto
Mrisho Ngassa
MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES.
MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013
Mtitu
muziki
Mwana FA
MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14
Mzee Majuto
Nancy Sumari
Nani Mtani Jembe?
NAPE
Nassoro ‘Nora’
Natasha
Nay wa Mitego
Necta
Nelly Kamwelu
NEY WA MITEGO
Nisha
NSSF;Zantel
Nyamwela
NYimbo
Nyota yako
OBAMA TANZANIA
OMMY DIMPOZ
P FUNK
PAM D
Peniel Mgilwa ‘Penny’
PETIT MAN
Profesa Jay
Q - CHILA
Q Boy
Q Chilla
QUEEN DARLEEN
RACHEL NDAUKA
RAIS KIKWETE
Rais Kikwete.
Rasimu Ya Katiba TZ
Ray
Ray C
Redd’s Miss IFM
REDD'S MISS KAGERA 2013
REDD'S MISS TZ
REDDS MISS TANZANIA 2014
Redds Miss wa Mikoa
REHEMA FABIAN
RICHIE RICHIE
Rihanna
ROSE MUHANDO
Rose Ndauka
Ruge Mutahaba.
SABASABA 2013
Saida Karoli
Saikolojia
Sajeti
SAJUKI
Sandra
SHAA
Shamsa Ford
Sheikh Ponda
Shilole
Sintah
Siwema
Skin Tricks
Snura Mushi
Spika Makinda
staa
Staa Wetu
Stella Mwangi
STYLE ZA NYWELE
Taifa Stars
Tamasha la matumaini
TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013
Tangazo
TANZANIA
TEGO
TENGENEZA WEBSITE NA BLOG
TID
Tundaman
Tupo wangapi?
TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14
Twanga Pepeta
USA PAGEANT 2014
VAI
Wastara
WEMA
WEMA SEPETU
Yanga
Yanga Bingwa 2013
YOUNG D
Yvonne Cherry ‘Monalisa’
Z Anton.
Zari
Zito kabwe
No comments:
Post a Comment