EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, May 28, 2015

MTOTO WA JOHARI AIBUA MASWALI

KUFUATIA kuibuka kwa habari ya msanii nguli, Blandina Chagula ‘Johari’ kubeba mimba na kujifungua kwa siri hadi mtoto kufikisha umri wa miezi 7 na kuripotiwa kwa mara ya kwanza na gazeti ‘tumbo moja’ la hili la Risasi Jumamosi, mambo mengi mapya ikiwemo maswali yameibuka na kuzua ‘sintofahamu’ juu ya uhalisia wa jambo hilo, Amani linakupa mchapo kamili.
Msanii nguli, Blandina Chagula ‘Johari’.
Saa chache baada ya habari hiyo kusomwa na mamilioni ya Watanzania wakiwemo wadau wa sanaa na burudani wiki iliyopita, minong’ono na mishangao ilianza kutambaa ambapo wengi walidadisi kwa kina ili kujua ‘lipi ni tui la nazi na yapi ni maziwa’ juu ya habari hiyo.
MASWALI YALIYOIBULIWA
Miongoni mwa maswali yaliyoibuliwa ni pamoja na mimba aliibeba akiwa wapi? Alitoka Dar kwenda Shinyanga anakodai kujifungulia mimba ikiwa na muda gani? Anaweza kuianika kadi ya kliniki? Nini sababu ya kuficha mimba hadi mtoto anafikisha miezi 7 na nini kimemsukuma kumwanika mtoto?
“Jamani, mbona hatuelewi haya mambo? Hivi inawezekana kweli kwa mtu maarufu kama Johari kubeba mimba na hadi kujifungua na mtoto kufikisha miezi yote hiyo (7) bila kujulikana?” alihoji Latifa Lusengi wa Sinza- Makaburini.
“Hiyo mimba aliibebea wapi? Mbona alikuwa akionekana hana tumbo?” alihoji mama Jane wa Mwananyamala.
MASTAA SASA
Kuashiria kuwa mjadala ulikuwa mzito, hoja na maswali hayakuishia kwa wadau tu kwani hata baadhi ya mastaa waliozungumza na mwandishi wetu ama ana kwa ana au kwa njia ya simu kwa nyakati tofauti, walionesha wasiwasi mkubwa juu ya habari ya utata huo huku wengine wakiomba hifadhi za nomino zao kwa kile walichokiita ni “kujitunzia heshima kwa Johari.”
Mtoto wa Johari.
MAINDA
Ruth Suka ‘Mainda’ ndiye alifungua pazia la majadala huu kwa upande wa mastaa, baada ya mwandishi wetu kumpigia simu na kumtaka atoe maoni yake juu ya kujifungua kwa ‘mbia’ wake huyo.“Mmh! Kama kweli Johari amejifungua, basi mimi nampongeza kwani kuzaa ni baraka, lakini sasa afikirie na suala la kufunga ndoa na huyo aliyezaa naye kwani hata umri unamruhusu, asikomee tu mtoto.”
“Nyie acheni utani bwana, sisi tunashinda naye kila siku iwe baa au sehemu tofauti, mbona hatukuona hata hizo dalili na ishara za mimba na sisi wanawake tunajuana sana kwa mambo kama hayo? Sijui lakini,” alihoji  msanii mwingine wa kike ambaye amekuwa akionekana mara kwa mara na Johari na kuomba hifadhi ya jina.
“Kama ni kweli kulikoni afiche mimba?” aliuliza kwa kifupi msanii wa kiume.
JOHARI AZIDI KUPIGILIA MSUMARI
Baada ya mwanahabari wetu kusikia maswali hayo kutoka kwa wadau na baadhi ya wasanii, alimtafuta Johari kupitia simu yake ya kiganjani ambapo alifunguka, kisha kukata simu.

“Mimba niliibebea tumboni, kwani kwa mwanamke kuzaa ni tatizo? Au walitaka niutangazie ulimwengu kuwa nimebeba mimba na nitajifungua siku fulani? Siko hivyo bwana.“Wanaotangaza hadi siku za kubeba mimba ni wao na umaarufu wao, mimi ni mtu mzima, naomba nilale kwanza, nina usingizi sana nitakutafuta baadaye,” alisema Johari na kukata simu na kuizima kabisa.
KUTOKA AMANI
Kuzaa ni jambo la heri, tunamuomba Johari kukata kiu ya maswali yote ya wadau na mashabiki wake ili kuondoa mkanganyiko, ikiwezekana aanike cheti cha mtoto ili kuwakata ‘vilimi’ wale ambao hawataki kuamini kile anachokizungumza. Hakuna sababu ya kufanya jambo lenye baraka na neema kama hili kuwa siri na kuficha wakati yeye ni mtu maarufu–Mhariri.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate