EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, June 12, 2015

DAKTARI: KAJALA HAWEZI KUZAA TENA!

Imelda mtema
MAJANGA juu ya majanga! Siku chache kufuatia kufanyiwa kipimo na kubainika kuna tatizo kwenye ubongo baada ya kupigwa chupa kichwani kwenye Klabu ya New Maisha, Masaki jijini Dar, mkali wa sinema za Bongo, Kajala Masanja ‘Kay’ amepata pigo lingine la daktari kumwambia hawezi kuzaa tena!
Mkali wa sinema za Bongo, Kajala Masanja ‘Kay’.
Kwa mujibu wa chanzo makini, Kajala alipewa maelezo hayo mapema wiki hii baada ya kufanyiwa kipimo na daktari bingwa wa hospitali moja iliyopo maeneo ya Morocco jijini Dar.
HISTORIA YA TATIZO
Kwa mujibu wa chanzo hicho, awali staa huyo alikuwa akisumbuliwa na tatizo la maumivu makali ya tumbo kwa kipindi kirefu na mara kwa mara hali iliyomlazimu kwenda kwenye hospitali mbalimbali za jijini Dar na kutibiwa lakini bila mafanikio.
“Unajua awali, aliamini amepata vidonda vya vitumbo (Ulcers).
“Pamoja na kupewa dawa mbalimbali kama ‘antibiotic’ kama Amoxicillin, Tetracycline, Clarithromycin na Metronidazole, dawa zenye uwezo wa kupunguza uzalishaji wa tindikali tumboni lakini wapi.
HALI YAZIDI KUWA MBAYA
“Kutokana na hali yake kuzidi kuwa mbaya ndipo mwanzoni mwa wiki hii alipojisikia maumivu ya kupindukia hivyo alikwenda kwenye hospitali ile iliyopo Morocco na majibu ya vipimo yakaonesha kuwa ana uvimbe mkubwa kwenye kizazi!” Kilisema chanzo hicho.
Mnyetishaji wetu alidai kuwa, daktari huyo alimshauri kufanyiwa upasuaji wa haraka ili kuondoa uvimbe huo kwa sababu anaweza pia kunyemelewa na tatizo la kansa achilia mbali ishu ya kutozaa tena.
KAJALA AISHIWA NGUVU
“Yaani Kajala aliishiwa nguvu kabisa alipoambiwa maneno hayo na kujikuta akimwaga machozi,” kilisema chanzo hicho.

KAJALA ASAKWA KUTHIBITISHA
Baada ya gazeti hili kupata habari hiyo, lilimtafuta Kajala ambapo alikiri kukutwa na tatizo hilo na ni kitu ambacho kimemchanganya sana hasa akimwangalia binti yake Paula (aliyezaa na Prodyuza wa Bongo Records, Paul Matthyasse ‘P Funk’), bado mdogo hivyo kujikuta akidondosha chozi.
“Yaani mtu akikuambia una ugonjwa kama huo, lazima uumie kwa kweli na mara nyingi namfikiria mtoto wangu bado mdogo. Kwa sasa najitahidi kufanya matibabu ya haraka ili kuondoa tatizo hilo,” alisema Kajala.
Kajala Masanja ‘Kay akiwa na mwanaye.
KITAALAM
Kwa mujibu wa daktari mmoja wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) ambaye aliomba jina kusitiriwa, mwanamke akiwa na uvimbe mkubwa kwenye mfuko wa uzazi na kwa muda mrefu, matibabu yake salama ni kukiondoa kizazi.
“Lakini kuna wanawake wanapatwa na  vimbe mbalimbali kwenye mfuko wa kizazi lakini si kubwa, ni rahisi kuondoa kwa kuchubua kitaalam na kizazi kikabaki salama,” alisema daktari huyo.
WEMA BILA KUJALI
Wakati huohuo, Kajala amekumbwa na janga baada ya aliyekuwa shosti wake wa kufichiana siri kama siyo kutunziana mambo yao ya ndani, Wema Sepetu kumpaka runingani!
Baada ya Kajala kujishusha akisema yupo tayari kupatana na mwenzake, Wema, mwanadada huyo amemshukia Kajala akimwita ‘bogasi’ yaani mjinga na kwamba ni mtu mzima lakini hana akili.
Akizungumza kupitia Clouds TV Jumanne iliyopita, Wema alifunguka kwamba hivi karibuni alishangazwa na kitendo cha Kajala kuandika vitu vya ajabu kwenye ukurasa wake wa Mtandao wa Instagram akisema amejishusha kumuomba msamaha ili aonewe huruma kwa watu na yeye (Wema) aonekane kuwa hafai.Mkali wa sinema za Bongo Wema Sepetu.
“Kabla ya kuandika vile nilikuwa nipo tayari hata akija kwangu nimkaribishe nimsikilize lakini kwa sasa sitaki kuambatana na Kajala.“Kajala ni mtu mzima lakini hana akili. Kuwa na Kajala ulikuwa ni upepo tu unapita. Alichokifanya mimi namuona bogus,” alisema Wema.
Kwa upande wake, Kajala alimjibu kwa kifupi bila kutaka kubebanisha maneno kwa kusema: “Siku zote duniani ukikimbizana na chizi na wewe utaonekana chizi, nimejishusha, nimechoka.”

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate