EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, June 30, 2015

DENTI KIDATO CHA KWANZA AFIA BWAWANI!

Na Kulwa Mwaibale
MSIBA! Mohamed Juma (14) ambaye alikuwa mwanafunzi wa kidato cha kwanza, Shule ya Sekondari ya Toangoma wilayani Temeke, Dar amefia bwawani wakati akiogelea.
Tukio hilo lililoacha majonzi kwa ndugu, jamaa, marafiki na wanafunzi wenzake, lilijiri Juni 26, mwaka huu, majira ya alasiri.
Mwanafunzi wa kidato cha kwanza, Shule ya Sekondari ya Toangoma wilayani Temeke, Dar, Mohamed Juma (14) amefia bwawani wakati akiogelea.
Akizungumza na Uwazi kwa masikitiko makubwa ya kumpoteza mwanaye, baba mzazi, Juma Shaha alisema familia yake imepata pigo kubwa kwa kuondokewa na mtoto wao wa kiume.
“Nashindwa nianzie wapi kuzungumza maana tumepata pigo kubwa sana kuondokewa na mwanangu wa kwanza katika uzao wetu wa watoto watatu wa kiume, inauma sana kwa kweli,” alisema Juma.
Juma alisema, majira ya saa 4 asubuhi ya siku ya tukio, Mohamed aliaga  kwenda twisheni na baadaye saa 8 kuelekea 9 alasiri alikwenda kwa rafiki zake Kilakala, Kongowe.
“Jambo la kushangaza, hadi inafika saa 2 usiku, Mohamed hakuonekana nyumbani ndipo tulianza kumtafuta,” alisema mzazi huyo.

Baba Mohamed alisema alikwenda kutoa taarifa Kituo cha Polisi Kongowe ambapo walimweleza aendelee kumtafuta.
Aliongeza kuwa, baada ya hapo alikwenda kutoa taarifa kwa Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Tuangoma ambaye aliungana naye kumtafuta bila mafanikio.
Juma alisema kuwa, licha ya kutoa taarifa Polisi Kongowe, alishauriwa kuripoti pia Kituo Kikuu cha Polisi Mbagala-Maturubai.
Alisema, wakati akirejea nyumbani kutoka kituoni, mkewe, Rahma Juma alimpigia simu na kumfahamisha kwamba rafiki zake Mohamed  walipeleka nguo za marehemu nyumbani.
Aliendelea kusimulia kuwa, walipowahoji watoto hao, Gabriel na Musa walisema wakati wakijiandaa kuogelea kwenye bwawa hilo lililopo Toangoma, walimuona nyoka mkubwa ndipo walichukua nguo na kukimbia wakimuacha Mohamed.
Mzee huyo alisema walipokwenda Toangoma alikokutana na Mkuu wa Sekondari ya Toangoma, Nchimbi na vijana kadhaa wakaenda kwenye bwawa hilo.
Walipofika, vijana wanaoweza kuogelea walijitosa kwenye bwawa kumtafuta Mohamed ambapo walifanikiwa kumuibua akiwa amenasa kwenye matope huku ameshafariki dunia.
Mzazi huyo alisema kwamba, katika jambo la kushangaza, Mohamed hakunywa maji kama inavyokuwa kwa watu wanaokufa vifo vya ajali ya maji.
“Baada ya polisi kufika walinihoji nikawaeleza kisa cha mwanangu kufariki dunia ndipo wakauchukua mwili kwenye gari na kuupeleka nyumbani kwangu, tukafanya taratibu za mazishi na kumzika katika Makaburi ya Kimicha yaliyopo hukuhuku Kongowe,” alisema Juma kwa huzuni.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate