EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, June 30, 2015

HUYU NDIYE ANAYEDAIWA KUUAWA MA MTOTO WA WAZIRI

Deogratius Mongela na Chande Abdallah
INASIKITISHA! Mmiliki wa Shule ya Msingi na Awali (International) ya Mount Zion iliyopo Bahari Beach, Dar, Annah Mizighi Mwambili, 47, (pichani) ameuawa na mwili wake kutupwa ndani ya shule yake baada ya kupotea kwa zaidi ya miezi sita huku mtoto wa aliyekuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Tatu Ntimizi, Said Ntimizi akidaiwa kuwa mmoja kati ya watuhumiwa wa mauaji hayo.
Mmiliki wa Shule ya Msingi na Awali (International) ya Mount Zion iliyopo Bahari Beach, Dar, Annah Mizighi Mwambili enzi wa uhai wake.
Duru za awali za upelelezi wa polisi, zinamtaja Said kuwa alikuwa na uhusiano wa karibu na marehemu bila kufafanua alihusikaje na mauaji hayo ya kinyama yaliyofanyika mwishoni mwa mwaka jana, siku na tarehe isiyojulikana na mwili wake kutupwa kwenye shimo la maji taka ndani ya eneo la shule aliyokuwa akiimiliki.
Aidha, nyuma ya taarifa hiyo ya mauaji, deni la shilingi milioni mia tisa (900,000,000) ambalo mwanamke huyo alikuwa akimdai mmoja kati ya watuhumiwa hao ambao majina yao yote bado hayajafahamika likitajwa kuwa ndiyo chanzo cha Annah kutolewa uhai.

ALIANZA KWA KUTOWEKA
Wakisimulia kwa uchungu namna Annah alivyotoweka nyumbani kwake, ndugu wa marehemu walisema, awali Desemba 26, mwaka jana kwenye Sikukuu ya Boxing Day, kuna wageni walifika nyumbani kwake, Boko, Dar, wakazungumza na baadaye wakaondoka naye na hakurudi tena.
 
Mtoto wa aliyekuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Tatu Ntimizi, Said Ntimizi anayedaiwa kuwa mmoja kati ya watuhumiwa wa mauaji hayo.
NDUGU WAPATA WASIWASI, WATOA TAARIFA POLISI
Ndugu hao walisema kuwa siku za kwanza hawakupata wasiwasi kwa vile ilikuwa kawaida ya marehemu kuwa mtu wa safari kutokana na biashara zake na kuongeza kuwa walianza kupata wasiwasi baada ya siku nne kupita huku kukiwa hakuna mawasiliano kati yao na marehemu, jambo lililowalazimu kuripoti Kituo cha Polisi cha Wazo Hill ambao walianza uchunguzi.


WAUMINI WAFUNGA NA KUSALI
Wakati wote huo, waumini wa kanisa alilokuwa akisali marehemu Annah la Winners Chapel lililopo Ukonga jijini Dar waliamua kufanya maombi ya kusali na kufunga kwa ajili ya kumuomba Mungu awaoneshe  mpendwa wao alipo.

MAITI YAPATIKANA SHULENI KWAKE MIEZI 6 BAADAYE
Kwa masikitiko makubwa, ndugu hao walisema, Juni 22, mwaka huu, ikiwa ni miezi sita na siku na chache tangu kupotea kwa ndugu yao, walipata taarifa iliyowashtua na kuwaumiza, kwamba mwili wa mpendwa wao umepatikana ukiwa umeharibika vibaya ndani ya shimo la maji machafu katika shule yake.
Ndugu, jamaaa na marafiki wakiwa katika misa ya mazishi.
HABARI ZA CHINICHINI
Habari za chinichini ambazo si rasmi zilizonyakwa na Gazeti la Uwazi, zinaeleza kuwa baada ya marehemu huyo kuchukuliwa nyumbani kwake, inadaiwa watuhumiwa walikwenda naye mpaka kwenye nyumba ya mganga mmoja maarufu wa kienyeji (jina kapuni) ambako walimuua kisha kuuchukua mwili wake na kuutupa shimoni.

POLISI WANASA TUKIO
Kama Waswahili wasemavyo, damu nzito kuliko maji ndivyo ilivyokuwa kwa Annah ambaye damu yake iliendelea kuwasumbua wahusika kiasi cha unyama wao kuwafikia polisi kupitia njia za kijasusi na hivyo kufanikiwa kumnasa mmoja wa watuhumiwa.
“Polisi walipopata taarifa za mauaji hayo, waliamua kufuatilia, wakabaini mmoja kati ya watuhumiwa hao yuko Arusha. Wakamuwekea mtego na kufanikiwa kumnasa, wakamleta jijini Dar ambapo aliwataja aliodai kushirikiana nao,” chanzo kutoka vyombo vya usalama kililiambia Uwazi.

MWALIMU MKUU AZUNGUMZA
Akizungumza na Uwazi, mwalimu mkuu wa shule hiyo, Dony Maige alisema shule yake ilikuwa imefungwa wakati marehemu ambaye ni mmiliki na mkurugenzi akiwa hajulikani alipo.
“Januari mwaka huu, tarehe za mwanzoni tulifungua shule kama kawaida baada ya likizo ya Desemba ambapo wanafunzi waliendelea na masomo. Lakini bajeti ilikuwa ngumu kutokana na mkurugenzi ambaye ndiye mtoaji wa fedha za matumizi ya shule na malipo ya wafanyakazi, kutoonekana.
“Hali hiyo ilisababisha baadhi ya wazazi kulazimika kuchangia huduma nyingine muhimu japokuwa walikuwa wamemaliza ada za watoto wao.

MWALIMU AWATOA MACHOZI WAOMBOLEZAJI
“Juni 21, mwaka huu tukiwa tumefunga shule na kutarajia kufungua tena kwa ajili ya muhula mpya wa masomo, ndipo nilipopokea simu kutoka vyombo vya usalama na kunitaka kusitisha zoezi la kufungua shule kwa kuwa kutakuwa na oparesheni maalumu katika eneo la shule. Nikaambiwa niwaondoe wafanyakazi wote isipokuwa mimi peke yangu.
“Nilishangaa, baada ya kufika shuleni na kuwaona polisi wakiwa eneo la tukio. Nilishtuka kutokana na maswali waliyokuwa wakiniuliza. Lakini jambo lililonishtua zaidi ni kuuona mwili wa marehemu Annah ukitolewa ndani ya shimo la maji machafu lililopo ndani ya shule ambayo kwa miezi yote sita wanafunzi na hata sisi walimu tulikuwa tukipita bila kujua.
“Kwa kweli sijawahi kukutana na kipindi kigumu kama hiki katika maisha yangu. Ni jambo la ajabu sana. Nimejiuliza maswali mengi na kukosa majibu,” alisema mwalimu huyo huku waombolezaji wakishindwa kuzuia machozi yaliyokuwa yakiwatiririka.

MWILI WAAGWA BILA KUFUNULIWA
Wakati wa kuuaga mwili huo, Jumamosi iliyopita nyumbani kwa marehemu, waombolezaji walitoa heshima zao za mwisho kwa masikitiko mbele ya jeneza la marehemu bila kufunuliwa kutokana na mabaki ya mwili huo kuharibika vibaya.
Mwili wa marehemu Annah ulipumzishwa katika Makaburi ya Kwakondo, Ununio jijini Dar. Hakika bwana ametoa, Bwana ametwaa, jina lake libarikiwe. Amina. Marehemu ameacha watoto watatu, Steven, Irene na Emerly Mwambili.

POLISI KINONDONI WALIVYOSEMA
Uwazi lilimpigia simu Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, ACP Emanuel Mlei na kumuuliza yafuatayo.
Uwazi:  “Kuna madai kwamba, mtoto wa aliyewahi kuwa waziri kwenye serikali ya awamu ya tatu, Tatu Ntimizi, Said Ntimizi mnamshikilia kwa mauaji ya mwanamke aliyekuwa mmiliki wa shule, Annah Mwambili, ni kweli?”
Kamanda: “Kuhusu hilo siwezi kulisema kwa sasa. Ila kesho (jana) nenda pale kwa Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamanda Suleiman Kova ataliongelea yeye.”
Uwazi bado liko kazini kuchimba tukio hili la kinyama na kwamba litaendelea kuwaletea mapya kadiri yanavyopatikana.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate