EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, June 26, 2015

VIFO MASTAA KUTIKISA UPYA!

Gladness Mallya na Mayasa Mariwata
MSHTUKO! Wakati wimbi la wasanii Bongo likizidi kuwa kubwa katika kutangaza nia ya kuwania nafasi mbalimbali za uongozi kwenye siasa kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, mwaka huu, mtabiri maarufu nchini, Maalim Hassan Yahya Hussein amefunguka mazito juu ya vifo vya mastaa hao kutikisa upya huku wale watakaosalia wakipata nafasi za uongozi.
steveveeStaa wa bongo movie Steven Mangele ‘Steve Nyerere’.
TUJIUNGE MAGOMENI-MWEMBECHAI
Akizungumza na gazeti hili ofisini kwake, Magomeni-Mwembechai jijini Dar, mapema wiki hii, mtabiri huyo alisema kuwa, mwaka huu kinyota ni wa mafanikio makubwa kwa wasanii lakini pia vifo navyo vitakuwa vingi kwao.
Wema-SepetuMiss tanzania 2006 na muigizaji wa Bongo movie Wema Sepetu.
NI MWAKA WAO KINYOTA
Alisema kwamba, kwa wale watakaosalimika huku wakiwa wamejiingiza kwenye kinyang’anyiro cha kugombea uongozi wa kisiasa, wote watafanikiwa kwa kuwa mwaka huu ni wao.
Maalim alisema kuwa, mwaka huu kinyota ni wao ndiyo maana wamejitokeza wengi kwenye kuwania nafasi hizo tofauti na vipindi vingine vya uchaguzi vilivyopita.

king-majutoMuigizaji mkongwe King Majuto.
“Mwaka huu kinyota ni wa mafanikio kwa wasanii lakini pamoja na kufanikiwa sana vifo navyo vitakuwa ni vingi mno, kwa hiyo wale wote waliojiingiza kwenye siasa watafanikiwa na watapata madaraka,” alisema mtabiri huyo.
WAFANYEJE KUKABILIANA NA VIFO?
Ili kukabiliana na jinamizi hilo la umauti, mtabiri huyo aliwataka mastaa kuwa watu wa ibada muda wote na kuachana na mambo ya starehe za kidunia.
“Usalama wao ni kuacha starehe. Hiyo ndiyo itakuwa njia sahihi ya kuepukana na roho wa vifo lakini kama hawatafanya hivyo, vifo vitakuwa vingi na vitawatikisa vilivyo,” alisema Maalim.
MASTAA WALIOTANGAZA NIA
Mpaka sasa mastaa wengi wameshatangaza nia ya kugombea nafasi za ubunge kupitia vyama mbalimbali vya siasa akiwemo, Wema Isaac Sepetu, Wastara Juma, Salome Urasa ‘Thea’, Aunt Fifii, wote Viti Maalum kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Wengine ni Steven Mengere ‘Steve Nyerere’, Amri Athuman ‘King Majuto’ kupitia tiketi ya CCM,  Seleman Msindi ‘Afande Sele’ kwa ‘leseni ya Chama cha  Alliance for Change and Transparency (ACT-Wazalendo) na Joseph Haule ‘Profesa Jay’ kupitia Chama cha Demokrasia na Maendele (Chadema).
Kwa mujibu wa Maalim, mastaa hao anawatabiria kuwika na wengine kuibuka kidedea kwenye uchaguzi kwa kuwa nyota zao zinang’aa kwa mwaka huu.
Katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita kuliibuka upepo mbaya wa vifo vya mastaa wa tasnia mbalimbali kabla ya wimbi hilo kutulia hivi karibuni huku mtabiri huyo akionesha shaka kuwa kinyota ishu hiyo inaweza kuanza kutikisha upya kabla ya uchaguzi mkuu.
WANGEKUWEPO
Baadhi ya mastaa waliokuwa na nguvu ya ushawishi mkubwa kwa mashabiki wao ambao kama wangekuwa hai walikuwa na nafasi kubwa ya kupata uongozi kisiasa endapo wangegombea ni pamoja na  marehemu Steven Kanumba ‘The Great’, Adam Kuambiana, John Maganga, Rachel Haule na Juma Kilowoko ‘Sajuki’ na wengine wengi ambao vifo vyao vilitikisa ulimwengu wa burudani Bongo.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate