
Kwa mbwembwe na mapozi tofauti, huku wakiachia sentensi zilizoashiria kila dalili na ishara za ubongo kuchanganyikana na ‘maji ya Ilala’ (pombe) wawili hao walinaswa katikati ya wiki iliyopita ndani ya Ukumbi wa Escape One, Mikocheni jijini Dar kulikokuwa na harusi ya msanii mwenzao, Haji Adam ‘Baba Haji’.
Awali, mastaa hao walikuwa wameketi viti tofauti huku shamrashamra za sherehe zikiendelea, lakini katika hali isiyokuwa ya kawaida wakati wa kuondoka, Wastara alimfuata Anti Lulu kwa madai ya kumuaga, ndipo wakasindikizana hadi nje ya ukumbi.

Ndani ya dakika sifuri, Ijumaa Wikienda lililokuwa limepenyeza ‘kijumbe’ wake kwenye pati hiyo, liliwafotoa picha kisha kuwahoji kulikoni wawe na furaha ya namna hiyo licha ya kuwepo kwa tetesi zikiwahusisha na bifu?
“Sisi ni wanawake, hatuwezi kununiana,” alisema Wastara na Anti Lulu kushadadia.
No comments:
Post a Comment