EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, June 3, 2015

WEMA AONESHA MAHABA NIUE LIVE

CHANZO: GLOBAL PUBLISHERS
LIVE! The Big Boss wa Kampuni ya Endless Fame Productions, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ amejikuta akionesha mahaba niue kwa ‘kujibebisha’ kwa Mshiriki wa Big Brother Africa ‘Hotshots’ 2014 kutoka nchini Namibia, Luis Manana huku akimmwagia sifa nyingi na kudai ndiye laazizi wa moyo wake kwa sasa baada ya kuachana na mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond’.
The Big Boss wa Kampuni ya Endless Fame Productions, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ akiwa na Mshiriki wa Big Brother Africa ‘Hotshots’ 2014 kutoka nchini Namibia, Luis Manana.
TUJIUNGE VIWANJA VYA POSTA
Tukio hilo lililoshuhudiwa na gazeti hili lilijiri ndani ya Viwanja vya Posta, Kijitonyama jijini Dar, wikiendi iliyopita kwenye Shoo ya Instagram Party ambapo Wema alikuwa mmoja wa washiriki wa tamasha hilo lililohudhuriwa na mamia ya mashabiki hivyo walipata mshtuko waliposikia habari hizo njema kutoka kwa Madam.
AMMWAGIA SIFA KEDEKEDE
Akiwa kwenye pati hiyo, Wema alipanda stejini kwa ajili ya kuongea na mashabiki wake na baadaye alipanda Luis ndipo Madam akaanza kummwagia sifa kedekede na kabla ya kumtambulisha rasmi kuwa ndiye ubavu wake.
Kwa kinywa chake bila kumung’unya maneno, Wema alidai kwamba Luis ndiye mwanaume ampendaye kwa sasa hasa akivua shati lake kwani ana vitu adimu ambavyo vinamfanya asimruhusu kuwa mbali naye.
LUIS NAYE
Baada ya sifa hizo, Luis naye alisema kuwa alipanda ndege kutoka Namibia hadi Dar kwa ajili ya kuja kujumuika na mwanamke ampendaye ambaye ni Wema.
Wema na Luis Manana wakifuatilia jambo.
TEAM WEMA FULL SHANGWE
Utambulisho huo ulizua shangwe nyingi kutoka kwa mashabiki hasa Team Wema ambao kwa pamoja walionesha kusapoti uhusiano huo na hata baada ya kushuka walionekana kuwazonga huku wakipigana vikumbo kwa ajili ya kutaka kila mmoja kupiga nao picha. “Sisi Team Wema tumepitisha ile Team Haters (timu ya wenye chuki) wakale malimao kama alivyosema Gwajima (Askofu Josephat) kwamba kama kuna watu hawampendi Lowassa (Edward) basi wakale malimao,” alisikika mmoja wa Team Wema.

NI KWA MARA YA KWANZA BAADA YA DIAMOND
Usiku huo ulikuwa wa kwanza kwa mwaka huu kumuona Wema akimtambulisha mwanaume kwa mara ya kwanza kwenye tamasha kubwa kama hilo tangu alipoachana na Diamond ambaye kwa sasa anajivinjari na mwanamama Zarinah Hassani ‘Zari The Boss Lady’.Kuna madai kwamba baada ya wawili hao kuwa beneti tangu waliposhuka jukwaani walikwenda kulala hoteli moja kwa mujibu wa wafuatiliaji.
WALILALA WOTE HOTELINI
Chanzo chetu cha habari kilichokuwa ndani ya hoteli hiyo (jina linahifadhiwa) kilidai kwamba siku hiyo Wema na Luis waliingia hotelini hapo na kulala hadi kesho yake, jambo ambalo lilikuwa siyo kificho tena hasa kwa wahudumu na watu wote walioongozana na msafara wa wawili hao. “Kweli kabisa Luis anatoka kimapenzi na dada yetu Wema maana nimeshuhudia tangu jana, Wema alikuja hotelini na baadaye wakaondoka wote.
...Wakikumbatiana kimahaba.
“Hata usiku wakati wanatoka Viwanja vya Posta pale Kitonyama walirudi na kulala pamoja, achilia mbali hiyo, Wema na Luis ni watu ambao wanaonekana kuwa katika mapenzi kwa muda sema tu Luis alikuwa hajapata nafasi ya kuja Dar,” kilisema chanzo hicho.
KUMBE LUIS ANAJUA KISWAHILI!
Baada ya kujiridhisha na uwepo wa uhusiano wa wawili hao, mwanahabari wetu alifuatilia kwa makini baadhi ya akaunti zinazotumiwa na Luis kwenye mitandao ya kijamii ambapo aligundua kuwa jamaa huyo amekuwa akimuweka Wema kwenye peji zake huku akimmwagia sifa na maneno ya kimahaba tena kwa Lugha ya Kiswahili.
Baadhi ya maneno aliyokuwa ameandika Luis katika peji yake ya Instagram akiambatanisha na picha zao yalisomeka: “Najaribu kumtuliza... Mtoto mzuri.“Huyu msichana anaweka tabasamu usoni mwangu.”

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate