EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, June 17, 2015

WEMA, JOKATE WAMZOMEA DIAMOND!

Musa Mateja
KAMA mbwai na iwe mbwai tu! Hiyo ndiyo kauli pekee iliyoweza kuakisi kitendo cha warembo, Wema Sepetu ‘Madam’ na Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ kuamua kumzomea zilipendwa wao, Nasibu Abdul ‘Diamond’ baada ya kuzidiwa tuzo na hasimu wake, Ali Kiba, Risasi Mchanganyiko lina full stori.
Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ akicheka baada Ali Kiba kuchukua tuzo ya nne kwenye Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.
ENEO LA TUKIO
Tukio hilo lililojidhihirisha laivu ni la chuki lilijiri wikiendi iliyopita kwenye Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam ambapo warembo hao walikuwa wamehudhuria kwenye sherehe za utoaji Tuzo za Kilimanjaro Music Award 2015, ambapo walishangilia kila Ali Kiba alipopata tuzo huku wakizomea pale Diamond alipopata.
Warembo, Wema Sepetu ‘Madam’ na Jokate Mwegelo ‘Kidoti’.

ZOMEA YANOGA
Warembo hao waliokuwa wamekaa sehemu tofauti ukumbini humo, kwa pamoja waliunganisha nguvu na kupata sapoti ya mashabiki wengine waliohudhuria hafla hiyo iliyomalizika kwa Ali Kiba kupata tuzo tano huku Diamond akiambulia mbili.
MCHANGANUO ULIVYO
Ali Kiba ambaye hakuwepo ukumbini na tuzo zake kupokelewa na mwakilishi, alijinyakulia tuzo za Mtumbuizaji Bora wa Mwaka, Wimbo Bora wa Mwaka (Mwana), Mtunzi Bora wa Mwaka (Bongo Fleva), Wimbo Bora wa Afro Pop (Mwana) na Mwimbaji Bora wa Kiume huku Diamond akitwaa za Wimbo Bora wa Zouk/Rhumba (Nitampata Wapi) na Video Bora ya Mwaka (MdogoMdogo).
Staa wa Bongo, Nasibu Abdul ‘Diamond’.
WAPENDA UBUYU WAHOJI
Kutokana na zomeazomea hiyo kuwa kubwa, waalikwa wanaojua kufuatilia mambo ya watu walianza kuhoji kulikoni  Jokate na Wema waungane kumzomea Diamond wakati wao wenyewe hawapatani.
“Dah ama kweli mapenzi ya Kibongo si ya kuyatilia maanani, sitaki kuamini kama Wema huyu ni wa kuonekana beneti na Jokate wakati mwanzo walikuwa hawasalimiani, kingine kinachonishangaza leo Wema huyuhuyu aliwahi kutolewa nishai na Jokate ndani ya ukumbi huuhuu katika shoo ya Diamond are Forever eti leo ni marafiki wanakaa hadi wanapiga picha ya pamoja,” alisema mmoja wa mashabiki.
Wema Sepetu ‘Madam’.
‘AFTER PART’ SASA!
Kuonesha kuwa walidhamiria, baada ya shoo ya utoaji tuzo kumalizika, Wema alionekana akijipongeza na wenzake kwenye ukumbi maalumu ambao ulikuwa umeandaliwa (after party) akipiga ‘gambe’ na kucheza muziki kujipongeza sanjari na Jokate hadi kulipopambazuka.
DIAMOND ANASEMAJE?
Kutokana na hali hiyo kujionyesha waziwazi, siku iliyofuata, paparazi wetu alimtafuta Diamond ili kumsikia anazungumziaje suala la warembo hao kumzomea lakini hakutaka kuwazungumzia zaidi akafungukia tuzo hizo kwa jumla.
Staa wa Bongo, Ali Kiba.
“Kiukweli sina kinyongo, napenda kutoa pongezi kwa washiriki, washindi wote na waandaaji, bahati mbaya mimi sikuweza kuhudhuria maana nilikuwa Afrika Kusini kwenye hafla ya utambulisho wa wasanii waliochaguliwa kuwania Tuzo za MTV Base (MAMA’S), pamoja na kutokuwepo hapo naomba kuwafahamisha Watanzania kuwa nimefurahishwa na washindi wote na tuzo zote.
AJIPIGIA DEBE KIAINA
“Namshukuru Mungu pia kwangu mimi kuchaguliwa kwa mara nyingine katika kuwania Tuzo za MTV kwenye tuzo ya Msanii Bora wa kiume Afrika, Mtumbuizaji Bora wa Kiume Afrika na nyimbo Bora ya kushirikiana Afrika, naomba watu wote tuungane katika hili tena ili tuweze kupiga kura kwa wingi na kuleta heshima kwenye nchi yetu na Afrika kwa ujumla,” alisema Diamond.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate