EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, August 12, 2015

Daktari: Mbowe yuko salama

Siku moja baada ya Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Freeman Mbowe kuugua ghafla akiwa kwenye maandaamano na kuwahishwa hospitali ya Taifa Muhimbili, imebainika kuwa hali hiyo imesababishwa na kufanya kazi kwa muda mrefu bila kupumzika.
Daktari bingwa wa Moyo Kitengo alicholazwa kiongozi huyo, Dk Tulizo Sanga alieleza kuwa baada ya jopo la madaktari wanane kumfanyia uchunguzi waligundua kwamba tatizo kubwa lililokuwa likimsumbua Mbowe ni uchovu ambalo kitaalam linaitwa ‘Fatigue’.
“Jopo la madaktari lilimfanyia vipimo na tumegundua kuwa tatizo kubwa linalomsumbua ni uchovu unaosababishwa na kusafiri na kufanya kazi kwa muda mrefu bila kupumzika.
“Uamuzi uliochukuliwa ni kumuweka mapumziko kwa ajili ya uangalizi zaidi ndani ya saa 48 lakini hali yake inaendelea vizuri anaweza kuruhusiwa muda wowote,” alisema Dk Sanga
Dk Sanga alieleza kuwa Mbowe alipokelewa hospitalini hapo kwenye kitengo cha magonjwa ya dharura akitokea katika hospitalia ya Doctors Plaza iliyopo Kinondoni.
Mwananchi lilishuhudia viongozi kadhaa wa upinzani wakiwasili katika Jengo la Moyo kumjulia hali kiongozi huyo.
Baadhi ya viongozi walioonekana ni Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, Juma Duni Haji, Godbless Lema, Joshua Nassari na Mwenyekiti mwenza wa Ukawa, James Mbatia.
Kwa upande wake, Mbowe aliwatoa hofu watanzania na kuwahakikishia kwamba yupo salama na waondokane na hofu ambayo imeonekana kuenea kwenye mitandao na vyombo vya habari.
“Hakuna hali yoyote ya hofu na wasiwasi kama ambavyo imeshaanza kujengeka kwenye mitandao ya kijamii nipo hospitali kwa sababu za kitabibu na si vinginevyo.
“Ninachoweza kuwaambia Watanzania niko salama na hali yangu inaendelea vizuri, tatizo nililonalo limetokana na kufanya kazi usiku na mchana bila kupumzika,” alisema Mbowe.
Akizungumza na wanahabari Mbatia aliwata watanzania kuendelea kumuombea kiongozi huyo na kuwaunga mkono Ukawa ili waendeleze harakati zao katika kipindi hiki cha kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu.
“Suala la kuugua ni kawaida kwa kila binadamu ninachoweza kusema tuondelee kumuombea ili arejee kwenye mapambano na wazidi kutuunga mkono kwenye harakati zetu”alisema Mbatia
Kuhusiana na uwezekano wa ugonjwa wa Mbowe kusitisha ziara za Ukawa mikoani Mbatia alisema ratiba inaendelea kama kawaida na afya ya kiongozi huyo ikitengemaa ataungana na wenzake kwenye harakati hizo.
Mbowe aliugua ghafla juzi akiwa katika maandamano ya kumsindikiza mgombea urais kwa tiketi ya chama hicho, Edward Lowassa baada ya kuchukua fomu za kugombea urais katika Tume ya Taifa Uchaguzi (NEC).

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate