EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, August 5, 2015

Diamond apagawa Aunt, Iyobo kuoneshana mahaba live

IYOBO (1)Moses Iyobo akiwa  na mzazi mwenzake, Aunt Ezekiel usiku wa kuamkia Agosti 3, mwaka huu ndani ya Ukumbi wa Hoteli ya Regency iliyopo Mikocheni jijini Dar.
Musa Mateja
Aah! Rais wa Wasafi Classic Baby (WCB), Nasibu Abdul ‘Diamond’, juzikati alijikuta akipigwa butwaa kufuatia kitendo cha mcheza shoo wake, Moses Iyobo ëMozeí na mzazi mwenzake, Aunt Ezekiel kuoneshana ‘mahaba nipeleke kuzimu’ hadharani, Risasi Mchanganyiko lilikuwepo kushuhudia.
IYOBO (7)
Tukio hilo la Diamond kupagawishwa na mahaba ya wawili hao lilijiri usiku wa kuamkia Agosti 3, mwaka huu ndani ya Ukumbi wa Hoteli ya Regency iliyopo Mikocheni jijini Dar ambapo kulikuwa na sherehe ya kuzaliwa ‘bethidei’ ya Iyobo. Lakini kabla ya kufika kwenye tukio hilo, twende hatua kwa hatua.
MWONEKANO WA DIAMOND UKUMBINI
Akiwa kwenye sherehe hiyo iliyojazwa pia na mastaa, muda mwingi Diamond alionekana mwenye furaha ya hali ya juu kufuatia mishemishe za bethidei hiyo iliyoandaliwa na Aunt kama moja ya kumshtukiza ‘sapraizi’ mpenzi wake huyo.
Habari zinasema mpaka Iyobo anaingia ukumbini hapo alikuwa hafahamu kama kuna sherehe ya kuzaliwa kwake.
IYOBO (2)
Rais wa Wasafi Classic Baby (WCB), Nasibu Abdul ‘Diamond’ akiwa kabeba keki.
MUDA WA MSHTUKO
Iyobo alizama ukumbini hapo saa 7 usiku kwa kuitwa na Aunt. Aunt pia ni staa wa sinema za Kibongo.
Baada ya Iyobo kuingia ukumbini alipata mshtuko kufuatia Diamond na nyota wa filamu za Bongo, Vincent Kigosi ‘Ray’ kumkaribisha kwa kummwagia maji na vinywaji mbalimbali ambapo waalikwa wengine nao waliungana kumuogesha huku wakimwimbia ‘hepi bethidei tu yu.’
IYOBO (3)
DIAMOND AFUNGUA SHAMPENI
Baada ya zoezi la kumkaribisha Iyobo aliyekuwa amelala zake nyumbani kwa Aunt kumalizika, Diamond alipewa chupa ya kinywaji aina ya shampeni kwa ajili ya kufungulia sherehe hiyo ambayo ilianza hapo.
IYOBO (5)
Moses Iyobo akiwa kamkumbatia mpenzi wake Aunt Ezekiel.
DIAMOND ACHEZA HUKU NA KULE
Katika hatua nyingine, waalikwa walitumbua macho kumwangalia Diamond ambaye muda mwingi alikuwa akicheza tena kwa vituko mbalimbali.
IYOBO (4)
ABEBA KEKI
Pengine ni kwa sababu ilikuwa bethidei ya mcheza shoo wake, kwani ulipofika wakati wa kupeleka keki mezani, Diamond aliibeba yeye hadi eneo husika kwa ajili ya ‘kulishania’.
IYOBO (6)
MAHABA NIPELEKE KUZIMU SASA!
Sasa wakati Aunt na Iyobo wakiwa katika tukio la kulishana keki kwa mtindo wa mahaba nipeleke kuzimu (mdomo kwa mdomo), Diamond alionekana kushtuka na kuwatumbulia macho (angalia picha ukurasa wa mbele).

Diamond aliendelea kuwatumbulia macho kama anayewachungulia huku akipanua mdomo kwa mshangao ambapo wawili hao wala kiroho hakikuwadunda kwamba wapo laivu.
KUMBE IYOBO ALIFUNDISHWA
Baada ya kuwashangaa wawili hao kwa karibia sekunde kadhaa, Diamond aliibuka na kusema kuwa, kulishana keki wawili hao kwa staili hiyo, ndivyo WCB ilivyomfundisha Iyobo kwamba, anapokuwa na mpenzi wake huyo sharti amlishe kwa kinywa na si kutumia uma.
DIAMOND HAWEZI KUFANYA HIVIIYOBO (8)
Jambo ambalo lilijitokeza kwenye sherehe hiyo ambapo waalikwa walisema katu, Diamond hawezi kulifanya hivyo kwenye sherehe nyingine (mbali na jukwaani) ni kitendo chake cha kuimba zaidi ya nyimbo zake tano ukiwemo Nana unaotamba kwa sasa. Huwa akialikwa mahali, Diamond huimba wimbo mmoja au mbili tu.
Hata hivyo, Diamond mwenyewe alisema kuimba nyimbo zote hizo na kuruhusu waalikwa kucheza ni moja ya kuonesha upendo na hamasa yake kwa Iyobo kwani bila yeye hakuna Diamond wala WCB kwa jumla.
IYOBO (9)
USIRI WA UMRI KAMA KAWAIDA
Hata hivyo, kama kawaida, mpaka mwisho wa shughuli hiyo, haikuelezwa wazi kwamba, Iyobo alikuwa akisherehekea kutimiza miaka mingapi ya kuzaliwa kwake zaidi ya kusemwa; ametimiza miaka kadhaa!

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate