EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, August 21, 2015

Wema avunja ndoa


HALI si shwari kwenye familia ya Kampuni ya Endless Fame Productions kufuatia madai mazito yanayomgusa mkurugenzi wake, Wema Isaac Sepetu akihusishwa na kuvunjika kwa ndoa ya mdogo wa mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ almaarufu kwa jina la Esma Platnumz aliyeolewa na Hamad Manungwa ‘Petit Man’.
MAI NDANI
Katika sakata hilo, mtangazaji maarufu Bongo, Maimartha Jesse ‘Mai’, Esma na Mtangazaji Nasra Rajesh ‘Lady Naa’ wanadaiwa kuunda kundi lenye lengo la kuwasuta wezi wa waume za watu (Wema aliwekwa kwenye tageti) lililopewa jina la Al-Shabaab.
Wakati mpango huo ukiendelea, Mai anadaiwa alielezea mkasa wa kuvunjika kwa ndoa ya Esma na Petit Man kwenye Instagram huku akimtaja Wema kuhusika kwa mafumbo, jambo lililomfanya staa huyo wa filamu (Wema) aogelee matusi ya kutosha.
MADAI YA WEMA KUHUSIKA
Madai kamili yanamhusisha Wema na uvunjifu wa ndoa hiyo akituhumiwa ‘kuchepuka’ na Petit Man kwa muda mrefu sasa huku mwenyewe akikanusha vikali.

USHAHIDI WA MESEJI
Madai yalizidi kushushwa kwamba, sakata hilo lina ushahidi ikiwa ni pamoja na Esma kubamba meseji zisizo na dalili njema kutoka kwa Wema zikiwa kwenye simu ya Petit Man.
“Ukibahatika kukutana na Esma halafu umkute kwenye ‘mood’ ya kuongea, atakueleza jinsi mume wake alivyokuwa na ukaribu wa kupitiliza kwa Wema. Yawezekana hawakuwahi kuchepuka lakini ukaribu wao ulikuwa wa kupitiliza kiasi cha kuibomoa ndoa hiyo.
SIMU ZA WEMA HADI USIKU WA MANANE
“Esma anadai kuwa kuachana kwake na Petit Man hakuhusiani sana na meseji za Diva (Mtangazaji wa Clouds FM, Loveness Malinzi) kwani hizo zilisherehesha ugomvi wao tu, ila kilichomfanya hadi akaamua kubwaga manyanga ni utitiri wa meseji za wanawake na simu kibao za Wema kumhitaji Petit Man hadi usiku wa manane wakati ni mume wa mtu,” kilidai chanzo hicho.
WEMA ANASEMAJE?
Kufuatia madai hayo, Ijumaa lilimtafuta Wema  alipopatikana alisema: “Mimi nimekuwa nikimsapoti Petit kwenye mambo yake na Esma, sasa kama kuna watu wanasema maneno ya kunifanya nionekane mbaya, hao ni watu wasio na nia njema na mimi.
“Nakaa na Petit kama mwanangu lakini pia ni mfanyakazi wa Endless Fame na Esma sina tatizo naye, zaidi watu wanaibua tu mambo yao. Sipendi kabisa…”
ESMA KIMYA
Esma alipotakiwa kufunguka juu ya madai ya Wema kuhusika kwenye kuvunjika kwa ndoa yake alisema kwa kifupi: “Hilo suala liko kwenye ngazi ya kifamilia, siwezi kuliongelea kwa sasa.”
WEMA AKEREKA
Kufuatia maneno ya kuuma kwenye mtandao aliyokuwa akiendelea kuandika Mai, Agosti 18, Wema alishindwa kuvumilia hivyo kwenda kumripoti kwenye Kituo cha Polisi cha Kijitonyama.
Paparazi wetu aliponyetishiwa ‘ubuyu’ huo wa Wema kulifikisha ‘soo’ hilo polisi, alinyanyua mguu hadi kituoni hapo ambapo alikutana na askari wakiongozana na Wema hadi Mitaa ya Sofani, Kijitonyama ambako kuna duka la Mai lakini hawakumkuta hadi kesho yake (Jumatano asubuni) alipotiwa mbaroni.
MSIKIE MAI
Baada ya Mai kufikishwa kituoni hapo alishikiliwa kwa saa kadhaa akihojiwa na alipotoka na kutakiwa kusema chochote kuhusiana na tukio hilo alisema:
“Huu ni mziki mnene, Wema amechokoza moto.”
PETIT MAN NA ESMA


Katika ndoa yao, Petit Man ambaye ni mmoja wa wafanyakazi wa Endless na Esma wamedumu kwa takriban miaka miwili na kujaliwa mtoto mmoja kabla ya mambo kwenda mrama hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate