EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Sunday, June 10, 2012

Madaktari waibana serikali, watangaza kugoma

CHAMA Cha Madaktari Tanzania (MAT) kimetangaza mgogoro na Serikali na kuipa wiki mbili kuyapatia ufumbuzi matatizo yao la sivyo watafanya mgomo wa nchi nzima.  Wametoa msimamo huo walipokutana jana jijini Dar es Salaam ikiwa ni siku chache baada ya ujumbe wao uliokuwa kwenye mazungumzo na Serikali kugoma kusaini makubaliano kwa kile walichoeleza mpaka wapate ruksa ya wanachama.  Jana ilikuwa ni siku ya ujumbe huo kuwasilisha taarifa ya makubaliano ambayo Serikali ilitaka waisaini na hivyo wanachama hao hawakuyaridhia hivyo kuamua kutangaza mgogoro.
 
Kutoka ndani ya kikao hicho cha ndani zilieleza kuwa madai ambayo Serikali imeshindwa kuyatekeleza ni nyongeza ya mishahara, mazingira mazuri ya kazi, marupurupu, nyongeza ya posho ya wito wa dharura, posho za nyumba na chanjo.
 Mkutano huo ambao uliwashirikisha madaktari pamoja na viongozi wa chama hicho walikubaliana kutangaza mgogoro wa wiki mbili na baada ya hapo wataingia katika mgomo ili kuishinikiza Serikali kuyapatia ufumbuzi madai yao.
 
 Walidai kuwa kamati iliyoundwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ilishindwa kuyatatua matatizo yao kwa kigezo kwamba Serikali haina uwezo wa kifedha.
 “Hata kama Serikali ingekuwa na fedha isingeweza kuongeza mishahara kama ambavyo tunataka kutokana na madai kwamba itasababisha migogoro na watumishi wengine,” kilisema chanzo chetu kutoka ndani ya mkutano huo wa madaktari.
 
 Madaktari hao walilalamika kwamba ahadi iliyotolewa na Rais Jakaya Kikwete kwenye mkutano wao ya kuhakikisha madai yao yanashughulikiwa kikamilifu wakati akiwataka warejee kazini baada ya mgomo waliofanya Januari mwaka huu, haikutekelezwa. 
 “Haiwezekani Serikali imeshindwa kutatua madai yetu hata moja na sisi tuendelee kukaa kazini hii ni dharau na kitakachofanyika ni kurudi kama tulivyofanya awali na itakuwa zaidi ya mgomo tulioufanya,” alisikika akilalamika mmoja wa wajumbe kwenye mkutano huo.
 
Walielezea kushangazwa kwa tabia ya Serikali kutotekeleza ahadi zake hadi pale watu wanapochukua hatua mbadala, kama vile kuandamana na kugoma.
 Mmoja wa madaktari ambaye hakutaka kutajwa jina lake alisema wamekubaliana waendelee kufanya migomo kushinikiza kukubaliwa matatizo yao.
 Walidai kuwa Serikali imekuwa ikifanya kazi kwa mazoea na wakati mwingine ikiingiza siasa katika masuala ya msingi kitu ambacho ni hatari kwa jamii na taifa kwa ujumla.
 Wanasema serikali imeshindiwa hata kuwapatia chanjo ya kuwakinga na maambukizo ya magonjwa mbalimbali wakiwa kazini.
 
“Serikali kweli imeshindwa hata kutufanyia chanjo na kusema itafanya hivyo kwa awamu huu ni uuaji kwani tunafanya kazi katika mazingira magumu, lakini inashindwa kututhamini,” alilalamika daktari huyo.  Walionya kuwa Serikali isipokuwa sikivu kwa safari hii watafanya mgomo ambao utakuwa mbaya kuliko ule uliofanyika awali na kusababisha taharuki kubwa kwenye hospitali nchini hususan Muhimbili.
 
Hata hivyo, baadaye Mjumbe wa MAT, Dk Godbless Charles aliwaambia waandishi wa habari kuwa walichoamua wanachama katika mkutao wasio ni mrejesho wa tathmini ya taarifa ambayo ilitolewa na Serikali baada ya kikao kilichofanyika Machi 31 mwaka huu. 
“Sisi tumewapelekea na wao wakataka irudi mezani na kupitiwa upya madai kabla ya wiki mbili na yawe yamepatiwa ufumbuzi,” alisema Dk Charles.
 
Akielezea juu ya mazungumzo yao alisema: “Tangu kamati hiyo ilipoundwa na Waziri Mkuu ili kushughulikia madai yetu, tumekutana mara sita na mara zote tulishindwa kufikia mwafaka. “Baada ya kurejesha taarifa ambazo hazikuwa na majibu ndio maana tukaamua kuitisha kikao cha ndani ili wanachama waamue wenyewe wasije kutuona tunawasaliti,” alisema.
 
 Rais wa MAT,  Dk Namala Mkopi alikiri kwamba wanachama wamekubaliana kutangaza mgogoro wa wiki mbili na serikali na baada ya hapo watapanga hatua za kuchukua.”
 Mgomo uliofanyika Januari mwaka huu ulisababisha vifo kwa wananchi kwa kukosa huduma ambapo Waziri Mkuu Pinda aliwasimamisha kazi mara moja Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Blandina Nyoni na Mganga Mkuu Dk Deo Mtasiwa.  Madai mengine ya madaktari hao ilikuwa ni kuwang’oa mawaziri jambo ambalo Rais Kikwete alilitekeleza kwa kutowarejesha kwenye Baraza alilolisuka upya kwa kuteua wengine.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate