EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, June 18, 2012

Moto wa bajeti kuanza leo

MJADALA mzito wa bajeti ya serikali iliyowasilishwa Alhamisi wiki iliyopita, utaanza kuunguruma leo, huku kambi ya upinzani bungeni ikitabiriwa kuibua hoja nzito pale itakapowasilisha hotuba ya bajeti mbadala ya fedha.
Taarifa za kuaminika kutoka ndani ya kambi ya upinzani inayoundwa na wabunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), zinasema kuwa hotuba hiyo mbadala ya bajeti, itakayosomwa leo, itaibua mambo mazito ambayo yanaweza kuwatibua upya hata wabunge wengine ambao wamekuwa wakiitetea ile ya serikali.

Kwa mujibu wa habari hizo, bajeti ya kambi ya upinzani imeandaliwa na jopo la wachumi na wataalamu ambao ni wanachama wa chama hicho, na ripoti sahihi za wasomi waliobobea katika nyanja na sekta zote muhimu zikiwemo za madini, kilimo, miundombinu, elimu, afya katika ngazi za kitaifa na kimataifa.
Imedaiwa kuwa bajeti hiyo, itaibua ‘madudu’ mengi ambayo yamefanywa na serikali, ikiwemo hoja za matumizi ya fedha ambazo zilitolewa kwa zaidi ya miaka mitano katika miradi ambayo baadhi yake haijakamilika na mingine haipo, lakini kila mwaka inatengewa fedha.

“Kuna miradi mikubwa ikiwemo ya uzalishaji umeme ambayo kwa miaka mitatu mfululizo imetengewa kiasi kikubwa cha fedha, lakini haijakamilika na mingine haijaanza kabisa.
“Kibaya zaidi, serikali mwaka huu nayo imeomba fedha bila kusema zile zilizotengwa kwa miaka ya nyuma zimeenda wapi na kwa nini mradi haujaanza,” alisema mmoja wa wabunge walioshiriki kuandaa bajeti hiyo.
Semina yaibua hasira
Wakati hali ikiwa hivyo, jana kundi la wabunge wanaounda Chama cha Kupambana na Rushwa (APNAC) walicharuka na kuafikiana kuichachafya hotuba ya bajeti bila kujali tofauti za kiitikadi, baada ya kuelezwa namna serikali inavyopoteza fedha kizembe.

Hasira za wabunge hao ziliibuka wakati wa semina iliyoandaliwa na Taasisi ya Policy Forum, baada ya kuelezwa kinaganaga jinsi serikali inavyopoteza mamilioni ya fedha kutokana na misamaha isiyo na tija kwa taifa, huku ikiongoza kwa kuomba mikopo nje ya nchi.
Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila (NCCR-Mageuzi) aliweka wazi jinsi makampuni ya madini yanavyoongoza kwa kuliibia taifa, kiasi cha kuifanya sekta hiyo ishindwe kuchangia kikamilifu pato la taifa.
Alisema inashangaza sana kuona kuwa kiwanda cha bia kama Serengeti na kile cha sigara ni miongoni mwa walipa kodi wakubwa 15 wakati kampuni kama Baricck ikiwa haimo.

Kafulila aliliambia Tanzania Daima kuwa, ikiwa CCM italazimisha kupitisha bajeti hii kwa vitisho, itakuwa imejimaliza kwa sababu Watanzania wa sasa si wale wa juzi.
“Sioni pa kukwepa, na kama kuna mbunge anataka kuendelea na ubunge wake hata akiwa ndani ya CCM, akubali kufia wapiga kura wake. Najua wengi wanaipinga na wengi wameniambia hivyo,” alisema.
Akichangia zaidi, Mbunge wa Nkasi Kaskazini, Ali Kessy Mohamed (CCM) mbali na kuonesha masikitiko yake kwa namna bajeti ilivyo, aliwataka wabunge kuwa makini katika masuala muhimu ya nchi.
Kessy alisema serikali imewaacha watu wakizurura ovyo, na kujiingiza katika biashara zisizozalisha, hivyo kusababisha kupanda kwa bidhaa muhimu nchini.
Katika hatua inayoonesha kuwa serikali itakuwa katika wakati mgumu bungeni kuanzia leo, Waziri kivuli wa 

Fedha, Kabwe Zitto ameeleza wazi msimamo wa CHADEMA, kuwa wanaipinga bajeti hiyo kutokana na ukweli kuwa haimlengi Mtanzania wa kawaida bali imelenga kuwanufaisha wachache.
Zitto ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, alitoa msimamo huo juzi wakati akiwahutubia wananchi wa Kata ya Kihesa mjini Iringa.
Alisema kuwa, umasikini wa watu unasababishwa na mfumuko wa bei za vyakula, huku serikali ikishindwa kudhibiti hali hiyo inayoendelea kuwaumiza.

“Mfumuko wa bei umefikia asilimia 18.7 ambacho ni kiwango kikubwa sana kwa maisha ya Mtanzania ambaye anatumia asilimia nane kununua chakula na kipato chake kinazidi kushuka siku hadi siku badala ya kupanda kutokana na rasilimali zilizopo,” alisema Zitto.Alifafanua kuwa, mfumuko wa bei za vyakula pekee umefikia asilimia 25 na ule wa bei ya nishati ukiwa kwenye asilimi 28 huku deni la taifa likizidi kukua kila siku.
“Kama leo tukilazimika kulipa deni la taifa, basi kila mtu kuanzia mtoto atakayezaliwa leo hadi wazee, atalipa sh 488,000,” alisema Zitto.
                Habari na  Charles Misango, Dodoma wa Tanzania Daima

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate