EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, June 18, 2012

Euro 2012 : Ujerumani na Ureno zafuzu kwa robo fainali


Ujerumani
                                             Ujerumani yafuzu kwa robo fainali
Mashabiki wengi wanaifikiria timu ya Ujerumani imo katika nafasi nzuri ya kuwa bingwa Euro 2012
Lars Bender alifunga bao la ushindi la Ujerumani siku ya Jumapili zikiwa zimesalia dakika 10 kabla ya kipenga cha mwisho, na kuiwezesha nchi yake kuwa miongoni mwa nchi nane ambazo zitashiriki katika michuano ya robo fainali.

Mechi nyingine ya kundi hilo la B ambayo ilichezwa wakati mmoja, kati ya Ureno na Uholanzi, Ureno walifuzu kwa ushindi kama huo wa magoli 2-1.
Bender, mwenye umri wa miaka 23, na ambaye ni mchezaji wa Bayer Leverkusen ya Ujerumani, aliizima ndoto ya Denmark ya mwaka 1992, walipowashinda Wajerumani katika fainali.
Ujerumani iliweza kuongoza katika mechi hiyo dakika ya 19 wakati Lukas Podolski alipofunga, lakini Michael Krohn-Dehli aliweza kuisawazishia Denmark dakika sita baadaye na kuipatia nchi yake matumaini ya kufika robo fainali.

Wachezaji wa Ujerumani hawakupendezwa na safari kutoka kituo chao cha nyumbani cha Gdansk, Poland, hadi Ukraine, lakini kutokana na ushindi wa Lviv, wameweza kufuzu kuingia robo fainali na watafurahia kuicheza mji ambao wameezeka kambi yao.
Kabla ya mechi ya Jumapili, mara ya mwisho Denmark ilipopambana na Ujerumani katika mashindano makubwa, ilikuwa ni fainali ya 1992, wakati Yugoslavia ilipopigwa marufuku kucheza, na hatimaye Denmark iliwashangaza wengi ilipoishinda Ujerumani katika fainali.
Timu ya Ujerumani ya mwaka huu ndio timu yenye vijana wenye umri mdogo zaidi katika mashindano ya mwaka huu, kwa jumla wachezaji wengi wakiwa na umri wa miaka 25 na siku 107.
Hii ni mara ya kwanza kwa Ujerumani kukamilisha mechi za makundi kwa rekodi safi mno ya asilimia 100.
---------------------------------------------------------------------------------------------------------------
                                                 Ureno imo katika robo fainali
Ureno
Cristiano Ronaldo aliiwezesha Ureno kuingia robo fainali
Mabao mawili ya mshambulizi Cristiano Ronaldo yaliiwezesha Ureno kuingia robo fainali ya michuano ya Euro 2012, kwa kuifunga Uholanzi, na pasipo shaka yoyote, kuwalazimisha kurudi nyumbani.

Kwa Uholanzi kuwa na matumaini yoyote kuendelea kusalia katika mashindano hayo, walilazimika kuifunga Ureno magoli 2-0, na bao la kwanza la mkwaju wa kupinda kutoka kwa Rafael van der Vaart liliwapa matumaini Uholanzi walipoweza kutangulia.
Lakini mchezo wa Uholanzi uliendelea kufifia, na Ronaldo alifanikiwa kusawazisha, alipopigiwa mpira na mwenzake Joao Pereira.
Nani alimsaidia Ronaldo kufunga kwa mara ya pili, na Ureno ikavuka hatua ya makundi na kujiandikishia nafasi katika robo fainali.

Ureno sasa itacheza na Jamhuri ya Czech, inayoongoza kundi A.
Kwa Uholanzi, timu hiyo imeonyesha mchezo duni sana, kwa kushindwa katika mechi tatu za makundi, ilhali miaka miwili iliyopita, wao walimaliza katika nafasi ya pili katika fainali ya Kombe la Dunia nchini Afrika Kusini.

Itawachukua muda Uholanzi kumsahau Ronaldo, mchezaji nyota wa Real Madrid ya Uhispania, ambaye aliifungia klabu hiyo magoli 60 msimu uliopita, na katika mechi dhidi ya Jumapili alicheza kwa kasi na kwa juhudi na kuwaacha Waholanzi wamezubaa.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate