EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, June 28, 2012

PICHA: MAPOKEZI YA DR. ULIMBOKA HOSPITALI YA MUHIMBILI

Wauguzi na Madaktari wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, wakilisukuma gari la wagonjwa lililombeba mpigania haki zao Dk. Ulimboka wakati akitolewa chumba cha X-ray akipelekwa Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI).



Madaktari wakisaidia kumuingiza Dk.Ulimboka katika gari la wagonjwa namba T 151 AVD la Hospitali ya AAR.
Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dk. Hellen Kijo Bisimba (katikati), akizungumza na waandishi wa habari Hospitali ya Taifa ya Muhimbili wakati akitoa taarifa ya kujeruhiwa kwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari inayoratibu mgomo wa madaktari nchini, Dk. Stephen Ulimboka, Dar es Salaam jana.
Dk. Cathbert Mchalo wa Taasisi ya Mifupa ya Moi (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari baada ya kumpokea, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania kwa ajili ya kupatiwa matibabu kufuatia majeraha aliyopata kutokana na kipigo.
Ofisa wa Polisi akimzuia mpiga picha wa gazeti la Tanzania Daima, Francis Dande, asimpige picha wakati wakimuondoa askari mwenzao aliyeshambuliwa na madaktari akituhumiwa kukutwa akipiga simu ya kuwataarifu wenzake kuwa Dk. Ulimboka hakufa.

Mmoja wa wana usalama wa (wa pili ushoto), akizozana na madaktari baada ya kumbaini akijifanya ni mwandishi wa habari na kumuamuru kuondoka eneo hilo mara moja.
Mmoja wa madaktari wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), wa pili kulia, akizozana na Askari Polisi waliofika hospitalini hapo wakidai wanatafuta redio yao ya mawasiliano iliyopotea wakati wa pilikapilika za kumpokea Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari inayoongoza mgomo wa madaktari nchini, Dk. Stephen Ulimboka, alipoletwa akiwa hoi kutokana na kipigo kutoka kwa watu waliomteka usiku wa kuamkia jana na kumtupa msitu wa Mabwepande.
Madaktari wakiwa wamepigwa butwaa nje ya viwanja vya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kufuatia tukio hilo.

Wauguzi wakiwa nje ya wodi ya Kibasila wakitafakari jambo kufuatia jambo hilo
Wauguzi wakiwa nje ya wodi ya Kibasila wakitafakari jambo kufuatia jambo
             Vilio vyatawala

Vilio vilitawala miongoni mwa Madaktari na Wauguzi katika Hospitali hiyo wakati Dkt. Ulimboka alipofikishwa kwa matibabu.

Madaktari walionekana wakiwa katika vikundi vikundi, huku wengine wakilaani kitendo alichofanyiwa Dkt. Ulimboka.

Wakati gari la wagonjwa likimtoa Dkt. Ulimboka kutoka katika chumba cha vipimo kwenda wodini, Madaktari waliokuwapo eneo hilo walionekana wakilisukuma gari hilo huku wakiimba mwimbo wa mshikamano, na wengine wakibugujikwa machozi.

Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dkt. Hellen Kijo Bisimba alisema amesikitishwa sana na tukio hilo na unyama aliofanyiwa Dkt. Ulimboka.

"Serikali baada ya kuona imeshindwa kufikia muafaka na madaktari hasa baada ya kwenda mahakamani wameanza kuwatisha madaktari hao kwa kuwashambulia hii ni hatari sana kwa taifa na kitendo alichofanyiwa Ulimboka ni vitisho hatutaweza kukaa kimya kwa jambo hili," alisema Dkt. Kijo-Bisimba.


"? Usalama wa Taifa ?"

Hata hivyo, katika tukio la kumpokea Dkt. Ulimboka waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali hasa wapiga picha walikuwa na wakati mgumu kufuatia vijana wanaodaiwa kuwa ni wa  "Usalama wa Taifa" kuwazuia wasipige picha huku wakitaka kuzivunja kamera zao jambo ambalo lililalamikiwa na baadhi ya Madaktari waliohoji, ni kwa nini wawazuie wanahabari.

"Kwanini wanawazuia waandishi wa habari kupiga picha?  Waachwe wapige ili wapeleke ujumbe kwa Watanzania juu ya unyama aliofanyiwa mwenzetu," alisema mmoja wa Madaktari hao.

Waandishi wa habari walilaani kitendo cha kuzuia kufanya kazi yao na wana usalama hao.
 
Kauli ya Kamanda Kova
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova akizungumza na waandishi wa habari kuhusu tukio hilo, amesema Dkt. Ulimboka aliokotwa na msamaria mwema ambaye hakutaka kumtaja jina lake kwa sababu za kiusalama na kutoharibu upelelezi, kuwa msamaria mwema huyo alimwokota Dkt. Ulimboka katika msitu wa Mabwepande  uliopo nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam na kutoa taarifa kituo cha Polisi cha Bunju, ambapo Askari  aliyekuwa zamu alichukua maelezo yake na baada ya hapo, alipelekwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa matibabu zaidi.

Kamanda Kova alisema Jeshi la Polisi Kanda Maalum limeunda jopo maalum kwa ajili ya uchunguzi na upelelezi wa tukio hilo la utekaji nyara, kwani ni tukio la kwanza kutoke nchini.

Ameongeza kwamba, wahusika wote watakaobainika kuhusika na tukio hilo wachukuliwa hatua za kisheria na sheria itafuata mkondo wake ili kukomesha matukio mengine kama hayo.

                              Source: http://www.wavuti.com/#ixzz1z3XDAV7E

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate