EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, June 28, 2012

Tamko la LHRC kulaani ukatili aliofanyiwa Dkt. Ulimboka Steven / LHRC Public Statement on cruel attack to Dr. Ulimboka Steven

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU UKATILI,UNYAMA NAVITENDO VYA KUTWEZA ALIVYOFANYIWA MTETEZI WA HAKI ZA BINADAMU DKT. ULIMBOKA STEVEN

Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kwa kushirikiana na Mtandao Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania(THRD- Coalition) tunalaani kwa nguvu zote kitendo cha shambulio la kinyama na la kutweza alilofanyiwa Dkt. Steven Ulimboka.

Tunapenda kuujulisha umma wote kwa ujumla kuwa, tumepokea taarifa kuwa, watu wasiojulikana wakiwa na silaha ( ambao wanasadikiwa kuwa ni mawakala wa dola) siku na saa husika, pale karibu na klabu ya Leaders maeneo ya wilaya ya Kinondoni, jijini Dar-es-salaam,walimkamata(kumteka)Dkt Ulimboka.Walimuingiza kwenye gari dogo kwa nguvu. Gari hilo lilikua jeusi lisilo na namba zinazoeleweka. Hatimaye walimchukua kwa nguvu na kumfunga macho kwa kitambaa cheusi usoni na kumfunga kwa kamba miguuni na mikononi huku wakimpiga sana kwa vitu mbali mbali ikiwemo kitako cha bunduki na vitu vingine vyenye ncha kali.Matokeo ya vipigo hivyo vya kinyama vimesababishia daktari huyu kupata majereha na uvimbe katika sehemu nyingi za mwili wake kuanzia utosini hadi miguuni. Kwa kifupi ni kuwa alitekwa nyara na kuteswa.

Alfajiri ya tarehe 27Juni 2012, tulipata taarifa ya mkasa huu na kuwa Dkt. Ulimboka ambaye mwanzoni alikua amepotea alikuwa amepatikana na alikua ameshikiliwa katika kituo kidogo cha polisi huko Bunju.Tuliambiwa kuwa Dkt.Ulimboka alipatikana akiwa amepoteza fahamu na kuokotwa na msamaria mwema katika msitu wa Mabwepande jijini Dar-es-salaam na alikua ametokwa na damu nyingi sana. Waliomuokota ndio waliompeleka katika Kituo cha polisi Bunju.Tulipofika kituo cha polisi Bunju tuliweza kumchukua tukiwa na madaktari wenzie na hatimaye kwa sasa anaendelea na matibabu katika taasisi ya mifupa Muhimbili(MOI),
Kutokana na unyama huu na vitendo hivi vya kutweza utu wa mtu, Kituo cha Sheria na Haki a Binadamu na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania(THRD-Coalition), kwa niaba ya asasi zote zenye kujali haki za binadamu na watu binafsi watetezi wa Haki za Binadamu, kwa nguvu zetu zote na kwa uwezo tulionao, na kwa kumaanisha tunalaani kwa dhati kitendo hiki cha kumtesa na kumuumiza Dkt. Ulimboka ambacho hakikubaliki katika jamii ya kistaarabu.

Tunatoa tamko lifuatalo,

a) Kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

i. Kwanza watoe matibabu yanayofaa kuokoa maisha ya Dkt Ulimboka;
ii. Kufanya uchunguzi wa dhati wa tukio hili zima ;
iii. Kuwakamata wale wote waliohusika na tukio hili na wakala wao na kulitaarifu taifa kuhusu watu hao na sababu za kufanya jambo hili ovu lililomletea madhara makubwa Dr.Ulimboka;
iv. Na kwa weledimkubwa kuwatia hatiani na kuwashtaki wote waliohusika
v. Na kuhakikisha wahusika hao wanapata adhabu kali watakapotiwa hatiani.

b) Kwa Jeshi la Polisi:

- Kuacha kuwa na upande wowote katika mgogoro unaoendelea kati ya madaktari na serikali;
- Kuheshimu utawala wa sheria, haki za binadamu, kutomchukulia mtu kama ana hatia kabla haijathibitishwa na kuwa na weledi katika yote wanayoyatenda;

c) Kwa watetezi wa haki za Binadamu:
- Kujenga na kuendeleza mshikamano wetu katika ngazi zote na kulaani vitendo vya ushambuliaji kama hivi.

d) Kwa Wataalamu wa Tiba:
- Kutokana na mazingira chokozi yaliyopo yanayoweza kuleta hali hasi, tunazidi kuwasihi wanataaluma wote wa afya kujizuia kutolumbana moja kwa moja kwa wakati huu bali kuendelea kufuatilia haki zao kwa kufuata utaratibu wa kisheria.

e) Kwa Wananchi /umma wa watanzania,
- Kuunga mkono shughuli zote zinazofanyika katika kutafuta haki zinazohusiana na tukio hili
- Kudai uwajibikaji na maboresho ya huduma za kijamii hasa hasa huduma za afya Tanzania.
- Kulaani vitendo vyote kama hivi vinavyokiuka haki za binadamu.

Hivyo basi, yote aliyotendewa Dr. Ulimboka ni mlolongo wa makosa ya jinai kwa waliotenda hivyo. Zaidi ya hapo tukio hili linaonyesha uvunjwaji wa haki za msingi uliofanywa na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama zinavyolindwa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya mwaka 1977 vifungu vifuatavyo: 12, 13, 14, 15,16,17,18, 20, 22,23 na 29.

Tunaamini kuwa vitendo kama hivi huwa vinafanywa kwa makusudi ili kunyamazisha na kuzuia kazi na juhudi za watetezi wa haki za binadamu. Havipaswi kurudiwa tena katika nchi hii iliyostaarabika tena ya kidemkrasia kwani hili ni tishio la wazi kwa watetezi wote wa haki za binadamu Tanzania.

Imetolewa Dar-es-salaam Tanzania leo tarehe 27 Juni 2012.

Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC)
Dr. Helen Kijo-Bisimba

 Mratibu Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRD-Coalition)
 Onesmo Olengurumwa

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate