EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, July 21, 2012

BI. HARUSI AFA BWANA HARUSI APONA


Stori:Mwandishi Wetu
HUKU majonzi yakiwa bado yametawala miongoni mwa Watanzania kufuatia vifo vya watu waliokuwa ndani ya meli ya MV Skagit ambayo ilipinduka na kuzama Julai 18, 2012 karibu na Kisiwa cha Chumbe, Zanzibar mambo mengi yameibuka.

Nje ya ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadik siku ya Jumatano (juzi) ambako serikali ilikuwa ikitoa ripoti ya maendeleo ya uokoaji, baadhi ya watu walikuwa katika hali ya majonzi kufuatia ndugu zao kutojulikanna walipo.
Hamis, aliyedai ni mfanyakazi wa Kampuni ya Azam ya tajiri Said Salim Bakheressa alisema mdogo wake, Khalfan na mchumba wake, Zaina Ally walikuwa ndani ya meli hiyo kwenda Zanzibar kufunga ndoa Alhamisi (juzi) kama maandalizi ya kuukaribisha Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan, lakini mpaka siku hiyo mdogo wake aliokolewa, ila Zaina hajulikani alipo.

Hamis alisema: “Naamini shemeji yangu amefariki dunia, kwani katika watu wote waliokolewa hayupo, maskini mdogo wangu (Khalfan), alikuwa akafunge ndoa ili wakati wa swaumu mkewe awe halali kumpikia chakula.”
Akaongeza: “mbaya zaidi, mpaka muda huu (saa saba mchana Alhamisi) serikali imetangaza kupatikana kwa miili mingine nane, lakini pia shemeji yangu hayupo.”
Hamis aliongeza kuwa ndoa hiyo ilikuwa ifungwe jijini Dar wiki iliyopita, lakini wazazi wa Zaina ambao wote wanafanya kazi serikalini Zanzibar waliomba ikafungwe visiwani humo.

MENGINE YA KUSHANGAZA
Mtu mwingine ambaye hakutaja jina lake, alisema siku ya tukio, yeye alimsindikiza mdogo wake mpaka bandarini, akiwa anapanda meli hiyo, yeye akaondoka kuendelea na shughuli zake.
“Sasa niliposikia meli imezama, nikampigia simu, hakupatikana, nikajua tayari. Nilituma habari kwa ndugu mbalimbali tayari kwa maandalizi ya msiba.

“Lakini ilipofika saa kumi na mbili jioni akanipigia simu akiniuliza kama nimesikia kuna meli imezama. Nilishtuka, nikahisi naongea na mzimu, nilipomuuliza ameponaje akasema alighairi akapanda meli nyingine, alipofika Zanzibar simu yake ikazima kwa sababu ya kuishiwa chaji.”
Naye mzee Fasha Abduel, mkazi wa Magomeni, jijini Dar, alisema siku hiyo ya tukio, asubuhi alimpeleka bandarini mtoto wa mdogo wake aitwaye Shaban na alimkatia tiketi kwenye meli hiyo, lakini kijana huyo alikuwa hataki kwenda Zanzibar ambako ndiko aliko baba yake mzazi.

“Kumbe nilipoondoka kwenda kazini kwangu (Manispaa ya Temeke) na yeye akageuza kurudi nyumbani. Ajali ilipotokea nilishtuka sana, nikampigia simu mdogo wangu kule Zanzibar, akaanza kilio. Nilipompigia mke wangu kumjulisha, akasema mbona Shaban alirudi muda uleule wa asubuhi na amejaa tele nyumbani,” alisema mzee huyo.

Mzee Hassan, mkazi wa Kariakoo, jijini Dar, yeye alikuwa akipeleka magunia matupu Zanzibar, lakini asubuhi wakati akijiandaa, mwanaye wa kiume, Ally anayesoma Shule ya Msingi Makurumla, Dar aliugua ghafla, hivyo ikabidi yeye akatume magunia hayo kwenye meli hiyo na kumtaarifu mtu wa kuyapokea Bandari ya Malindi, Zanzibar ikawa salama yake.

HALI HALISI
Mpaka tunakwenda mitamboni, maiti zilizopatikana kufuatia ajali hiyo ni 31 huku 146 wakiwa wameokolewa na 117 hawajulikani walipo.

MELI YAFIKA MITA 47
Habari zaidi zisema kuwa, meli hiyo ambayo ilizama jumla jioni ya Jumatano, ilifika kina cha mita 47 kwenda chini wakati uwezo wa wazamiaji waliokuwa kwenye eneo la tukio ni mita 30 tu.

SPIKA WA BUNGE AWARUHUSU WABUNGE KWENDA MISIBANI
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Anna Makinda, Julai 19, aliahirisha bunge na kuwataka waheshimiwa waende misibani kuungana na Watanzania wengine katika kipindi hiki kigumu.

SIKU 3 ZA MAOMBOLEZO ZAISHA LEO
Wakati serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) ikitangaza siku tatu za maombolezo ambapo bendera hupepea nusu mlingoti, juzi Alhamisi, Serikali ya Jamhuri ya Muungano nayo ikatangaza siku tatu za maombelezo kwa nchi nzima ambazo zinakwisha leo.

KWA NINI KUTOKA DAR?
Kumbukumbu za haraka zinaonesha kuwa, sehemu kubwa ya ajali za meli hutokea wakati wa kutoka Dar kwenda Unguja au Pemba.
Miezi kumi iliyopita, Meli ya MV Spice Islanders ilipata ajali ikiwa inatoka Dar, kupitia Unguja kwenda Pemba.
Baadhi ya wananchi waliozungumza na gazeti hili walisema hata meli nyingi zinazozima injini majini, nyingi huwa zinatoka Dar kwenda Unguja.
UITABIRI WA MAAFA KUONGEZEKA
Wakati hayo yakitokea, baadhi ya Watanzania wametabiri ajali zaidi za meli wakidai kuwa nyingi haziko vizuri kwa safari za majini.
“Kama serikali haitachukua hatua ya kukagua meli zetu, ajali nyingi mbele zinakuja kwani meli nyingi hazina sifa ya kufanya safari za majini kutokana na kuzeeka au kutofanyiwa matengenezo.
KUTOKA KWA MHARIRI
Mungu awatie nguvu na uvumilivu wale wote waliopoteza ndugu zao katika ajali hiyo. Tuliwapenda wapendwa wetu, lakini Mungu amewapenda zaidi. Amina.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate