

Mwenyekiti mpya wa Yanga, Yusuf Manji.
Na Saleh Ally
KWA mara ya kwanza, Mwenyekiti mpya wa Yanga, Yusuf Manji,
amezungumzia kipigo cha mabao 5-0 ambacho timu yake ilikipata kutoka kwa
watani wao, Simba, kabla ya yeye kuingia madarakani.
Simba ambao ni mabingwa wa Tanzania Bara, waliitandika Yanga kwa mabao 5-0 katika mechi ya mwisho ya kufunga msimu iliyochezwa Mei 6, mwaka huu, kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Simba ambao ni mabingwa wa Tanzania Bara, waliitandika Yanga kwa mabao 5-0 katika mechi ya mwisho ya kufunga msimu iliyochezwa Mei 6, mwaka huu, kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Akizungumza na Championi Ijumaa katika
mahojiano maalum, Manji alisema kipigo hicho kiliisambaratisha Yanga na
ndicho kilichangia yeye kugombea nafasi hiyo na akasisitiza inawezekana
kulipa kisasi.
“Kilikuwa kipigo kibaya na kilitusambaratisha, ilikuwa ni aibu, ndiyo maana uongozi wangu utafanya kazi kubwa ya kurudisha imani kwa Wanayanga. Hicho ni kitu muhimu sana.
“Hatuwezi kuacha kuizungumzia Simba kwa kuwa ni changamoto kwetu, kinachotakiwa kwa Yanga ni kuangalia mipango madhubuti ambayo siku ya mwisho itatufanya tuwe na timu imara.
“Kilikuwa kipigo kibaya na kilitusambaratisha, ilikuwa ni aibu, ndiyo maana uongozi wangu utafanya kazi kubwa ya kurudisha imani kwa Wanayanga. Hicho ni kitu muhimu sana.
“Hatuwezi kuacha kuizungumzia Simba kwa kuwa ni changamoto kwetu, kinachotakiwa kwa Yanga ni kuangalia mipango madhubuti ambayo siku ya mwisho itatufanya tuwe na timu imara.
“Kama tuna timu imara, kuifunga Simba au timu yoyote
mabao tano, hakitakuwa kitu kigumu. Kujipanga kwa mipango na programu za
uhakika, ndiyo kitu bora kuliko kukimbilia kulipa kisasi tu,” alisema
akionyesha kujiamini.
Manji alisisitiza kuwa wachezaji lazima wajue wana jukumu kubwa la kurejesha heshima ya Yanga na kocha atahusika katika kuhakikisha kikosi chake kinafanya kweli.
Manji alisisitiza kuwa wachezaji lazima wajue wana jukumu kubwa la kurejesha heshima ya Yanga na kocha atahusika katika kuhakikisha kikosi chake kinafanya kweli.
“Kama viongozi,
tutahakikisha mishahara, posho au kama kuna ahadi, kila kitu
kinapatikana kwa wakati mwafaka. Sasa wachezaji na makocha wahakikishe
tunafanya vizuri. Tunajua timu haiwezi kujengwa kwa siku mbili. Hatuwezi
kutimiza ahadi zetu kwenda katika mafanikio kama tutakuwa na timu
inayofungwa,” alisema Manji.
Kikosi cha Yanga kwa sasa kipo chini ya Kocha Mbelgiji, Tom Saintfiet na kimeanza michuano ya Kagame kwa kufungwa mabao 2-0 na Atletico ya Burundi kabla ya kuibuka na kuinyonya ‘damu’ Wau Salaam ya Sudan Kusini kwa mabao 7-1.
Kikosi cha Yanga kwa sasa kipo chini ya Kocha Mbelgiji, Tom Saintfiet na kimeanza michuano ya Kagame kwa kufungwa mabao 2-0 na Atletico ya Burundi kabla ya kuibuka na kuinyonya ‘damu’ Wau Salaam ya Sudan Kusini kwa mabao 7-1.
No comments:
Post a Comment