EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, April 15, 2013

SOME TEXT MISSING - 03

                                Chombezo na IRENE MWAMFUPE NDAUKA.
“Kwani kaka kasemaje?”
“Hakusikia kitu, alisikia zogo tu, nimemwambia nilikuwa namfokea msichana
wa kazi amekuwa mzembe sana siku hizi...
“Amekuelewa?”
“Amenielewa, si hakusikia kitu kabla.”
Shemeji alikuja akapiga magoti mbele yangu na kuanza kunishikashika
sehemu mbalimbali za mwili huku akiniangalia kwa macho yaliyojaa mwonekano wa
kulemewa na mahaba mazito.
Nilimsihi kuacha maana hali ya hatari ilishajitokeza...
“Hakuna hatari tene, nimeikabili sawasawa kama inavyotakiwa.”
Nilimuahidi shemeji anishikeshike baadaye badala ya muda ule, akanielewa
na kuniacha.

***
Nilikuwa chumbani nimelala, mlango ukasukumwa, akaingia shemeji...
“Shemeji amka ule, ukishakula oga tutatoka kama nilivyokwambia.”
Nilikurupuka, lakini shemeji wakati huo akawa ameshaondoka zake.
Niliamka, nikaenda kula sebuleni. Nilikula peke yangu, shemeji alikuwa na
mumewe chumbani. Nilipomaliza, nilirudi kulala. Nilikuja kushtuliwa saa tisa na
usingizi niliolala ulikuwa mzito sana...
“Sweet mbona leo unalalalala sana, una nini?” alisema shemeji akiwa
amepiga magoti chini na kunipapasa kifuani. Nilisikia raha sana, nikahisi kama
nipo ufukweni kwenye upepo mwanana.
“Nimechoka sana shemeji, si unajua asubuhi mara mbili?”
“Aah! Shemeji bwana, mbona mi’ bado mwenzio,  unajua siku nyingi sana sijacheza mchezo
mzuri kama huu.”
Nilicheka kwa mbali, lakini shemeji yeye hakucheka, aliendelea kuutembeza
mkono wake kwenye kifua changu. Nilihisi kusisimka mwili, nikaingia hatua
nyingine ya kutamani kucheza mechi...
“Shemeji,” niliita...
“Bee...”

“Nateseka mwenzio.”
“Na nini shemeji?”
“Si hivyo unavyo...”
“Ninavyofanya?”
“Ee...”
“Pole, unataka nini sasa?”
“Wewe unajua.”
“Hapana bwana, baadaye, amka uoge tuondoke sasa.”
Niliamka, nikaenda bafuni kuoga, niliporudi nilivaa, nikatoka.
Shemeji alikuwa kwenye gari tayari, alikuwa akimwangalia Bertha
anavyofuta vumbi hapa na pale.
“Uko tayari shemeji?” aliniuliza shemeji akiniangalia kwa macho yenye
matamanio makubwa.
“Eee shemeji.”
“Dada maliza sisi tunaondoka,” shemeji alimwambia msichana wake wa kazi
huku akianza kushika mlango. Nilizunguka gari nikaenda kuingia mbele kwa
abiria.
Shemeji aliliondoa gari polepole hadi nje, msichana wa kazi akafunga
geti, tukaondoka. Umbali wa kama dakika mbili tulikuwa kimya, shemeji ndiyo
akaanza...
“Sweetheart nitabidi nikakununulie simu.”
“Nitashukuru sana shemeji.”
“Unataka ya aini gani?”
“Yoyote ya kawaida lakini shemeji...”
“Ya kawaida? Hutaki yenye manjonjomanjonjo?”
“Hapana shemeji, nataka kama ya Gabriel...”
“Gabriel gani shemeji?”
“Yuko nyumbani, Dodoma ni jirani yetu.”
“Ooo...basi tukifika dukani utanionesha niijue.”
Tuliingia Kariakoo, shemeji akaegesha gari mahali, tukashuka na kutembea
kwa miguu hadi mahali fulani kwenye maduka mengi ya simu.
Tuliingia duka la kwanza tu, nikaiona simu inayofanana na ya Gabriel...
“Hii hapa shemeji.”
Shemeji alishtuka alipoiona simu hiyo...
“Ha! Shemeji, mbona hii simu ya bei rahisi sana, simu elfu thelathini na
tano!”
“Mimi ndiyo naitaka hii shemeji.”
Kwa kuwa mimi ndiyo nilikazania, shemeji alitoa elfu thelathini, akampa
muuzaji. Tulitoka hapo na kwenda kwa mtu mwenye meza ya mwanvuli tukanunua
laini ya mtandao wa simu, shemeji ndiye aliyenichagulia namba, zilifanana kwa
mbali na zake, akanikabidhi lakini akiniambia sitakiwi kutumia hadi ikae kwenye
chaja kwa masaa kadhaa.
“Sasa shemeji twende mahali tukanywe kidogo.”
“Wapi shemeji?”
“We twende tu, utapajua hapohapo.”
Tuliondoka Kariakoo, shemeji akaendesha hadi sehemu moja siikumbuki, pana
baa lakini pia pana kitimoto, akaegesha gari hapo, tukashuka na kukaa kwenye
meza ya pembeni ya wawili tu.
Mhudumu alipofika, mimi niliagiza bia, shemeji akaagiza bia kisha
akamuomba mtu wa jikoni aje atusikilize. Hapo sasa ndipo ambapo shemeji
aliongea mambo yake ya moyoni kuhusu uhusiano wangu na wake...
“Shemeji...” alianza kusema...
“Naam...”
“Sitaki tuachane, lakini pia sitaki tujulikane, lakini pale utakapoona
navuka mipaka ujue nina uhakika wa ninachokifanya, please usije unkanikatili...
“Mimi sina mwanaume mwingine, kaka yako kama vile, hawezi kwa sasa,
unadhani nitafanyaje ili nijikidhi hamu yangu kama mwanamke..?”
“Nimekuelewa shemeji...”
“Oke, kama umenielewa kuanzia sasa nataka nipate haki yangu kwa kuniita
sweet, baby, dear, mpenzi au darling, sawa darling..?”
“Sawa baby...”
“Hapo sawa sweet. Kingine nataka kila siku asubuhi na jioni niwe napata
haki yangu.”
“Hilo linawezekana dear.”
Sasa tulianza kulewa, kwani shemeji alifika mahali akawa ananinywesha bia
kwa kutumia kinywa chake bila kujali wateja waliokaa kwenye meza ya jirani.

***
Saa kumi na nusu tuliondoka tukiwa tupo bwii kwa pombe, shemeji
alinishika mkono hadi kwenye gari. Tukaondoka, lakini njiani shemeji akasema...
“Sweetheart, nataka twende hotelini tukafurahi kwa uhuru mkubwa.” 
Nilimwangalia shemeji kwa macho yenye mshangao, nikapitia maneno yake
tena...
“Sweetheart, nataka twende
hotelini tukafurahi kwa uhuru mkubwa.” 
“Vipi, mbona unaniangalia baby wangu?”
“Hata...”
“Hujanielewa?”
“Nimekuelewa sana...”
“Kwa hiyo umekubali au?”
“Kwa nini nisikubali dear?”
Nilimwona shemeji akiachia tabasamu huku akiniangalia mara moja na kukaza
macho mbele, barabarani.
Siijui hoteli hadi leo, lakini nakumba ilikuwa ya ghorofa mbili, shemeji
aliingiza gari ndani na geti kubwa, akaniambia tushuke.
Tulitembea kuelekea mapokezi wote huku akiwa amenishika mkono...
“Mh!” niliguna...
“Nini darling, mbona umeguna?”
“Umepajuaje hapa sweet?”
“Ooo, kuna rafiki yangu anaishi Arusha, alikuja kwenye harusi ya rafiki
yetu wote, akafikia hapa...vipi, unadhani nilikuja na mwanaume mwingine?”
“Eee, nilidhani hivyo...”
“Aaaa, baby acha wivu bwana...”
Tulifika mapokezi, mhudumu wa hapo alikuwa mwanamke, alipotuona
tumeshikana mikono alioenesha kushtuka, mimi nilijua ni kwanini.
Aliniona mimi ni kijana mdogo kuliko shemeji lakini tulikuwa kimahaba
zaidi...
“Karibuni sana, niwasaidie...”
“Tunaweza kupata chumba?”
“Vyumba vimeisha, jaribuni mtaa wa pili, kuna hoteli inaitwa City Villa,”
alisama mhudumu huku akimkazia macho shemeji zaidi...
“Oke, asante sana anti,” alisema shemeji akiwa bado amenishika mkono na
kugeuza.
Tulikwenda kwenye huo mtaa wa pili, tukaiona hiyo hoteli, shemeji
aliingiza gari ndani ambapo mlinzi wa getini alitufungulia.
Kama tulikotokea, shemeji alinishika mkono, tukaongozana hadi mapokezi
ambapo mhudumu wa hapa alikuwa mwanaume, kijana mdogo tu...
“Karibuni sana,” alitukaribisha, lakini nyuma yake, kuna ubao mkubwa
ambapo kulikuwa na misumari ya funguo, kwa pembeni kulikuwa na ubao
ulioandikwa; NAFASI ZIMEJAA.
“Mh! Tulikuwa tunataka chumba, lakini tunaona nafasi zimejaa,” alisema
shemeji kwa sauti ya chini na ya upole sana...
“Wiki hii tuna wageni kutoka Kenya, wamechukua vyumba vyote,” alisema
yule mhudumu huku akinikazia macho mimi zaidi.
Tuliondoka kuelekea kwenye gari, nilimwona shemeji anakosa amani ya
uso...
“Dear kama vipi si turudi nyumbani tu?” nilisema.
Badala ya kunijibu aliniangalia, uso wake ulikasirika mpaka nikajua...
“Nilisema leo nataka kwa uhuru zaidi, hukunielewa?”
“Nilikuelewa shemeji, basi tuzidi kuhangaika, tutafanikiwa.”
Wakati tunatoka kwenye hoteli hiyo, mbele yetu tuliona nyumba inna kibao
juu kimeandikwa; TULIZANA GUEST HOUSE...
“Eti sweet...” aliniita shemeji...
“Naam...”
“Kwanini tusiingie gesti tu, kwani lazima hoteli? Hoteli zenyewe kama
hivi,” hapo alinyoosha gari hadi nje ya gesti hiyo.
Ilikuwa gesti ya kawaida sana, haina milango ya chumba nje, mapokezi
tulimkuta mzee mmoja mwanaume ambaye alituchangamkia sana...
“Karibuni sana wajukuu zangu, mnataka chumba?”
“Ndiyo,” alikubali shemeji.
“Karibuni, vyumba vipo.”
“Vizuri?” alihoji shemeji...
“Kwa hadhi yetu ni vizuri. Vina majina nje ya miji mbalimbali...”
“Una maanisha nini?”
“Naamanisha utakutana na vyumba vinaitwa Nairobi Kenya, Kampala Uganda,
Cairo Misri, Djamena Chad na vingine vingi tu.”
“Mh! Sisi hatuhitaji majina ila chumba.”
“Sawa, mtapata.”
Shemeji alipewa daftari ajaze jina lake ambapo aliandika jina la uongo.
Aliandika hivi...
Jina kamili: Blandina Frank Mavumbi.
Unakotoka: Morogoro.
Unakokwenda: Dar es Salaam.
Kazi: Mfanyabiashara.
Mzee wa mapokezi alitupeleka chumbani huku akichekacheka kama mtu
mwenyewe maswali mengi lakini anashindwa kuyauliza...
“Hawajambo nyumbani lakini?” aliuliza yule mzee...
“Hivi we mzee mbona maneno mengi  sana, nyumbani kwetu kunakuhusu nini wewe?”
“Jamani! Mimi nawaona nyie kama wajuku zangu, sasa lazima nijue maendeleo
yenu, kama nimewakosea mnisamehe sana,” alisema mzee huyo huku akitufungulia
chumba na kutukaribisha.
“Mbona mtaulo?” alihoji shemeji...
“Naleta...”
“Ngoja, usiondoke kwanza. Hakuna kandambili...”
“Pia nakwenda kuleta...”
“Hamna sabuni...”
“Yaani nakwenda kuleta vyote...”
“Lete na tishu...”
“Sawasawa.”
Hatukufunga chumba kumsubiri yule mzee ambapo baada ya muda alikuja akiwa
na vitu vyote tulivyomuomba. Shemeji alivipokea, akafunga mlango kwa funguo.
Baada ya kuvimwaga kitandani vitu vyote, alinishika na kunisimamisha,
tukaangaliana kwa karibu zaidi kwa muda wa kama dakika tatu nzima. Aibu ilimjaa
machoni lakini akajikaza tu kuniangalia...
“Sweet...” aliita kwa sauti tamu na nzuri...
“Naam dear...”
“Nakupenda, nipe ulimi...”
Nilimnyooshea shingo, nikatoa ulimi. Naye akaudaka na kuumiliki kinywani
mwake kwa dakika kadhaa kabla hajautoa na kupiga magoti chini mimi nikiwa bado
nimesimama.
Alishika sehemu ya mbele ya suruali, akafanya jitihada za kupaweka wazi.
Sikujua alikusudia kufanya nini. Aliingiza mkono mfukoni na kutoa ‘maiki’ kisha
akaanza kuimba nyimbo nzuri za mapenzi.
Hali hiyo ilinipa wakati mgumu mimi, miguu ilikufa ganzi, nilitamani
kuanguka chini na kulala, lakini mkono wake mmoja ulinishika goti kwa hiyo
sikuweza kuanguka.
Alipomaliza kuimba, alinichojoa, akachojoa, akafanya kama mwanzo kushika
maiki na kuanza kuimba.
Mara simu yake ikaita, akaiangalia...
“Mh! Monica huyo, sijui anasemaje, ngona nimsikilize..haloo Monica..”
“Shemeji kapona nini, naona gari yake hapa Tulizana Guest House...”
“Alitoka nalo fundi, nadhani bado anatanulia,” shemeji alisema huku
akibinua midomo kama ishara ya kukejeli.
“Aaa, uko nyumbani?”
“Ndiyo.”
“Oke, nitapita hapo.”
“Muda gani?”
Kabla Monica hajajibu ni muda gani, simu ikakatika, shemeji kila
alipojaribu kumtwangia, simu hiyo haikuwa hewani tena...
“Loo, asije akaenda nyumbani sasa hivi, itakuwa balaa maana akifika kabla
yetu ina maana atamkuta kaka ‘ako, atamsimulia ameliona gari gesti wakati anajua
mimi ndiyo nimeondoka nalo,” shemeji aliniambia huku akionekana mwenye
wasiwasi.
Hakuna kilichoendelea, tuliondoka haraka sana eneo hilo, tukafika
nyumbani baada ya dakika chache tu.
“Dada.”
“Abee.”
“Monica alifika hapa?”
“Hapana, sijamuona.”
Mara, nje kulisikika mlio wa honi ya gari, shemeji akatoka haraka.
Baada ya muda nikamsikia shemeji akiingia na mtu huku akisema...
“Yaani sasa hivi ndiyo kalileta, kaondoka, hujapishana naye hapo kona?”
“Hapana, sijapishana na mtu,” nilimsikia huyo mtu akisema, nikajua ni
mwanamke na ndiye Monica.
Alimkaribisha, akaa kwenye kiti huku akinikazia macho mimi...
“Hujambo?”
“Sijambo shikamoo.”
“Marahaba.”
“Huyu shemeji yangu, anaishi Dodoma,” shemeji alitambulisha.
“Oke, sawa, karibu sana Dar es Salaam.”
Niliitikia asante, kisha wakaendelea na mazungumzo yao.
Mimi nilisimama, nikaenda nje ambako nilimkuta Bertha akiendelea na kazi
zake za kila siku...
“Mlikwenda wapi?”
“Lini?”
“Lini? Si leo...”
“Si tulikwenda mjini.”
“Kufanyaje?”
“Shemeji alikwenda kuninunulia simu.”
“Iko wapi?”
“Nini?”
“Hiyo simu ulionunuliwa.”
“Si iko kwenye chaji.”
Tuliongea mambo mengi na Bertha, lakini mwisho wa yote, aliniambia jambo
nikashtuka sana...
“Hivi unajua anachoumwa kaka ‘ako..?”
“Mbona kipo wazi sana.”
“Oo, kipo wazi, kumbe ukijui wewe...”
“We unajua nini?”
“Si nasikia ameathirika.”
“Mh!” niliguna kwanza. Nilimshika mkono na kutoka naye nje ambako
nilimuuliza vizuri...
“Mi ndivyo ninavyosikia.”
“Kwa nani?”
“Majirani.”
Niliinamisha kichwa kwa muda, lakini sauti ya shemeji na mgeni wake ndiyo
iliyonishtua, nikaondoka kabisa hapo nyumbani kuzunguka nyumba huku nikimwacha
Martha akiingia ndani...
“Wewe unazungunguka tu, kazi utafanya muda gani?” shemeji alimjia juu
Martha.
Niliizunguka nyumba kisha nikarudi, niliwakuta akina shemeji bado wanaongea
nje, lakini mwenzake tayari alikuwa ndani ya gari.
“Shemeji ulikuwa wapi?”
“Nyuma huko.”
“Kuna nin tena?”
“Kunyoosha miguu tu.”
“Haya, sawa.”
Niliingia ndani,nikafikia kwenye kochi. Nilianza kumfikiria shemeji
alivyo na kumfananisha kama kweli anaweza kuwa mwathirika kama alivyoniambia
Martha...
“Lakini inaweza kuwa kweli, ila Martha naye si mtu wa kuaminika, ana
maneno mengi...” niliwaza moyoni huku mapigo ya moyo yakinienda kwa kasi ya
ajabu.
Mara shemeji aliingia huku akisema...
“Leo mwili wangu sijui ukoje, nimechokachoka?”
Kisha nikasikia sauti masikioni mwangu ikisema...
“Halafu waathirika huwa wanakuwa hivyo, wanachokachoka sana.”
Nilijikuta kama nakurupuka, nikamkazia macho shemeji...
“Pole, itakuwa nini?”
“Nadhani malaria, juzijuzi nililala msibani kuna mbu wengi sana, nadhani
wameniletea madhara,” alisema shemeji huku akiniangalia kwa macho yenye hoja
lakini hakuisema.
Aliingia chumbani, alipotoka alikuwa ameshika gazeti, akanitupia nisome
kisha akaondoka kurudi chumbani, mara akarudi tena akiwa ameshika CD mpya maana
ilikuwa ndani ya nailoni...
“Hii CD ni filamu ya kivita, nzuri sana, nimeinunua lakini sijawahi
kuiangalia, hebu iweke.”
Niliichukua, nikaiweka kwenye deki na kuanza kuitazama, lakini cha ajabu
kumbe haikuwa filamu ya kivita bali mapenzi...
“Ha!” nilishtuka.
“Unashtuka nini tena?”  aliniuliza
shemeji huku akiachia tabasamu laini...
“Kumbe ni hii?”
Mara msichanha wa kazi alitokea, alikuwa akipita kutoka chumbani kwake
kwenda jikoni, akatupa macho na akapunguza mwendo kisha akasimama kabisa...
“Wewe, unataka nini kwetu?” shemeji alijia juu, Martha akaondoka kwa kasi
kuendelea na safari yake huku akisema...
“Mimi nilijua watu wanacheza muziki wa kizungu kumbe hao wahuni.”
“Martha,” aliita shemeji...
“Abee...”
“Rudi hapa.”
Martha alirudi, akasimama mbele ya shemeji, macho yake yalionesha dalili
ya kuishiwa nguvu ya kuangalia...
“Hivi unajua siku zako za kuishi humu ndani zinahesabika?”
“Kwa nini dada?”
“Kwanini dada? We huoni,” shemeji alisema akibana pua kuiiga sauti ya
Martha...
“Yaani hapa nakwambia unataka nini kusimama hapa,, unajibu mimi nilijua
watu wanacheza muziki wa kizungu kumbe haoo wahuni, ina maana na sisi
tunaoangalia ni wahuni, si ndiyo?”
“Dada ulimi ulitereza.”
“Ondoka, usirudie tena na lugha zako mbaya.”
CD iliendelea kuzunguka, shemeji aliweka sauti ya chini sana kiasi kwamba
hata sisi wenyewe tulikuwa hatuwasikii wale wahuni na kile walichokuwa
wakikifanya zaidi ya kuangalia matendo tu.
Mara, msichana wa kazi alipita tena, akasimama kama mwanzo na kusema...
“Lakini hawa si huwa wanalipwagwa kwa kufanya hivyo?”
Nilimwona shemeji akimwangalia kwa macho ya kicheko na mwishowe akacheka
kweli huku akiendelea kumkazia macho...
“Unajua shemeji huyu Bertha ana matatizo...” shemeji aliniambia...
“Tena makubwa shemeji, mimi nadhani anahitaji msaada wa mawazo na
kufundishwa maadili ili ajue anatakiwa kuishi vipi...”
“Ni kweli kabisa shemeji...”
“Mimi napita tu,” alisema Bertha akienda ndani.
Hata mimi mwenyewe kusema ule ukweli sikufahamu lengo hasa la Bertha
lilikuwa ni nini...
“Halafu dear, huyu Bertha lazima aondoke hapa nyumbani, mimi nakwambia,
tukimwacha huyu atatuletea matatizo makubwa,” alisema shemeji. Nilijua ameniita
dear kwa sababu Bertha alishapita zake.
Shemeji alinikumbusha kuhusu simu, nikamwambia ipo kwenye chaja...
“Kailete shemeji.”
Nilikwenda kuichukua, nikampa, akaniambia nikae kochi lilelile alilokaa
yeye ili anifundishe kuhusu simu ile...
“Shemeji nimeshawahi kuitumia, kwa hiyo siyo mgeni sana mimi.”
“Wewe, nani shemeji yako?” shemeji alikuja juu lakini huku akicheka
kiaina.
“Da! Samahani sana darling, nilijisahau...”
“Hapo sawa, mimi si shemeji yako, wewe ni mume wangu, kwani hujui baadhi
ya makabila hapa Tanzania, mke akifa anarithiwa na mdogo wake au kaka mtu?”
“Yapo, kwa hiyo na wewe ulipenda siku moja urithiwe na mimi?”
“Nani mwingine wa kunirithi sweet..?”
“Kabila letu haliamini hayo mambo...”
“Hakuna kabila lisilokuwa na utamaduni huo, ila maendeleo ya dunia na
kusambaa kwa magonjwa mengi ndiyo kumewafanya watu waachane na mila hiyo...”
“Kwa hiyo mimi na wewe tuko kwenye kundi gani shemeji..?”
“Kati ya..?”
“Kustaarabika ili kuachana na mila au bado kustaarabika...”
“Mimi nakupenda shemeji, tubaki kwenye kundi la wasiostaarabika...”
alisema shemeji, akanibusu na kuifungua simu kisha akachukua yake, akanitumia
muda wa hewani wa shilingi elfu tano huku akisema...
“Hiyo itakuwa kwa ajili ya kunisalimia kila siku asubuhi kabala hujatoka
kitandani...”
“Da! Nashukuru sana my love,” nilimwambia, nikambusu shavu la kulia,
kisha naye akanitegea la kushoto ili nimalizie...
“Mmm...waaa...”
“Asante she, halafu mbona leo wewe wa moto sana?” aliniuliza...
“Kweli?”
“Kweli tena, kwani wewe hujui sweethetart..?”
“Sijitambui...”
“Basi tambua.”
Shemeji alisevu namba za simu yangu kwenye simu yake, akaandika MY
HUZBAND.
“Shemeji una hatari wewe...”
“Kwani wewe si mume wangu, hata yeye anajua wewe ni mume wangu...”
“Ha! Kweli shemeji?”
“Kha! Kwani nilipokuwa nakuja nyumbani Dodoma nilikuwa nakusalimiaje?”
“Hujambo mume wangu?”
“Sasa, manake nini kwani? Mdogo au mkubwa wa mumeo ni kama mumeo tu”
“Aaaa, nilidhani kujua ile ya siri...”
“Ha! Haa! Haa! Haa!”
Baada ya kusevu namba yangu kwake akasevu pia yake kwenye simu yake kwa
kuandika SWEET WIFE...
“Angalia, umeipenda?” alisema akinionesha jina hilo linavyoonekana kwenye
simu yangu...
“Eee, hiyo tamu...”
“Sana ..?”
“Sana...”
“Kama nini..?”
“Kama pipi kifua...”
“Ha! Ha! Haaaa!”
Shemeji aliniaga akiniambia...
“Sweet, leo nataka kupika chakula kizuri sana, nataka ule ushibe mpaka
uvimbiwe...”
“Tena ni njaa shem, kama sijala mchana...”
“Kweli?”
“Kabisa...”
“Basi nipe nusu saa tu.”
Shemeji aliondoka, mimi nikaona uvivu kukaa pale, nikaenda chumbani
kwangu.
Nilijitupa kitandani kwa kulala mlalo wa kuangalia juu au kwa jina
lingine chali, nikawaza...
“Hivi maisha haya ndiyo raha au mauti mbele..?”
“Ni kwanini shemeji ananipenda kiasi hiki, kwema..?”
“Je, siku bro akijua nini kitafuatia?”
“Je, nikiamua kumkaushia shemeji anaweza kuja juu...lakini hapo jibu liko
wazi, lazima atanifanyia visa tu mpaka niondoka.”
Mara simu yangu ililia, sikujua kama ni meseji au ilipigwa kwani hata
wimbo shemeji ndiyo aliuseti.
Nilikuwa bado nimelala vilevile kwa hiyo nikachukua simu kwa kupeleka
mkono chini ya kisogo ilipokuwa na kuileta machoni, ilikuwa meseji...
“Vipi sweet, upo chumbani?” ilitoka kwa shemeji kwani kwenye inbox jina
lilisomekana SWEET WIFE...
Nilimjibu...
“Nimepumzika tu baby, vipi chakula?”
Naye akajibu...
“Chakula mume wangu nakuomba unipe dakika chache sana kitakuwa tayari, i
miss you.”
“I miss you too, nakupenda.”
Nadhani neno ‘nakupenda’ lilimsisimua shemeji kwani alinipigia
palepale,  nikapokea...
“Haloo...”
“Baby nimefurahi sana uliponiambia unanipenda sana, da! Nakupenda zaidi
mume wangu...”
“Hunishindi ninavyokupenda mimi dear...”
“Aaa, wapi! Mimi natamani niwe nawe kila sekunde, kila dakika na kila
saa...”
“Asante darling...”
“Poa basi baby, acha mimi nikuandalie chakula chako cha jioni,
mmm...mwaaa...”
“Mmm...mwaaa...” na mimi nilimbusu shemeji kwenye simu, kisha akakata
simu.
Nilihema kwa nguvu zote, nikaendelea kuwaza. Niliamini nipo kwenye penzi
zito na tamu la shemeji. Penzi ambalo zikuwahi kuhisi nitalipata siku moja
kutoka kwa mwanamke kama shemeji.
Nasema kama shemeji kwa sababu ni mwanamke aliyeumbwa akaumbika, kila
idara kwake ilikuwa sawasawa kuanzia unyayo hadi utosini.
“Mh! Ila shemeji kaumbwa jamani, kila kiuno, mamaa...halafu mi macho yake
sasa...yaani akikuangalia unasikia aibu mwenyewe. Hivi anajijua kama ameumbika
kupita wanawake wengine?”
Ile naendelea na mawazo yangu kitandani, mlango ukasukumwa, nikageuka kwa
kasi kumwangalia aliyeingia.
Bertha, msichana wa kazi ndiye aliyeingia akiwa anatabasamu...
“Wewe unasemaje?”
“Sisemi kitu. Hivi mnavyofanya na dada wewe unaona ni sawa kabisa?”
“Tumefanya nini?”
“Kwani hujui?”
“Si useme unachokijua wewe...”
“Yaani kama kweli hamna mapenzi kati yenu ni kwanini mnaangalia picha
mbaya mkiwa wote?”
“Kuangalia picha kuna ubaya gani kwani?”
“Hujui ee? Haya,” alisema akitoka nje.
Wakati anafungua mlango nilisonya kwa nguvu kwani nilikuwa nimekasirika.
Baadaye nilipitiwa na usingizi, nikalala. Sikumbuki nilichukua muda gani
kulala, lakini nilikuja kushtuka baada ya kuhisi joto zuri mgongoni kwangu..
“Ha!”
“Ha nini mpenzi wangu, hutaki nikupapase jamani?” alikuwa shemeji amepiga
magoti chini akiupapasa mgongo wangu, kuanzia kwenye shingo hadi kiunoni...
“Vipi dear, unajisikiaje nikifanya hivi?” shemeji aliniuliza kwa sauti
nyororo huku akiwa amenisogelea sikioni...
“Nasikia raha sana sweet...”
“Niendelee, niache?”
Nilimjibu kwa vitendo kwani nilijipinda nikaushika mkono wake uliokuwa
ukipapasa mgongo na kuukandamiza kuashiria kwamba nilikuwa nahitaji aendelee
kunipapasa.
Shemeji aliendelea, sasa akapeleka mkono hadi kwenye matundu ya masikio
yangu ambapo nilihisi kusisimkwa mwili wote. 
Nilijikuta nikigeuka na kulala chali badala ya kifudifudi kama mwanzo.
Naye akahamia kunipapasa kwenye tumbo sasa, kuanzia shingoni hadi kiunoni, kuna
wakati alijua ‘ananitesa’ kwani alipita kiuno mpaka kwenye makazi halisi ya
mimi ambapo nilijikuta nikitupatupa miguu huku na kule kwa ‘uraha’.
“Baby,” aliniita shemeji.
Nilishindwa kumjibu kwa sauti, nilitingisha kichwa tu huku nikimkodolea
macho malegevu.
Shemu alifika mahali akaiishika maiki yangu na kuanza kuisumbua kwa tabu
za hapa na pale mpaka ikakasirika.
Nilimshika shemeji nikamvuta, akasimama, nikamvuta tena kuja kitandani,
akapanda akiwa na nguo zake...
“Unajua chakula tayari?” aliniambia naye akionesha dalili za kulemewa na
mahaba...
“Si baadaye...”
“Njaa imepungua?”
“Iko palepale?”
“Sasa si ukale kwanza?”
“Nina njaa nyingine my love...”
“Ipi?” shemeji aliniuliza huku nikijua alikuwa akifahamu nini nilikuwa
nakitaka kwa muda huo.
Nilimshika khanga aliyokuwa amejifunga, nikamuonesha dalili kama nataka
kuivua...
“Mh! Utaweza na njaa baby?”
Nilikubali kwa kutingisha kichwa, nikamuona shemeji anajisevia kwa
kuchojoa khanga yake moja aliyokuwa amejifunga kukatiza kwenye ‘nido’ zake.
Alibaki kama siku alipoingia duniani kwa mara ya kwanza. Nilishikwa na
uchu wa ajabu, utadhani nilikuwa na miaka miwili sijakutana na mtu mwenye jinsi
yake. Nilivua nguo zangu kwa papara kama nilidhani atanikatalia baada ya
sekunde kumi.
Wakati navua na yeye akawa anazidi kunihasisha kwa kuendelea kucheza na
maiki hali iliyoniweka katika wakati mgumu sana kimapenzi...
“Inakuwaje?” aliniuliza shemeji kwa sauti tamu huku macho yake yakiwa
hayana nguvu ya kuona sawasawa. Nilijua na yeye yuko vibaya kamma nilivyokuwa
mimi, lakini ili kujiridhisha nilijifanya nabatilisha kukutana ili nikale
kwanza...
“Sweet...” niliita.
“Bee...”
“Ngoja nikale kwanza.”
“Haa! Noo baby, umenifikisha pabaya halafu unataka kuniacha, hamna kwenda
mpaka tumalize,” alisema akinivutia kwake kwa dalili zote kwamba alitaka mechi
ianze haraka.
Nilijipindua, nikaingia uwanjani na mpambano ulianzia hapo. Shemeji
hakubakiza kitu katika kujiachia, alipoona inafaa kulalamika alifanya hivyo,
alipoona inafaa kuzungumza hakujizuia, ilifika mahali sauti yake ikatawala
chumba hadi nikahofia kuwa inaweza kuvuka ukuta wa chumba. Niliamua kumziba
mdomo shemeji...
“Mmm...shemeji usinizibe mdomo bwana...”
“Unaongea sana sasa...”
“Sasa nijibane kwa ajili gani?”
Mara mlanngo uligongwa, nikamwacha shemeji, nikashuka kitandani
nikitetemeka.
Shemeji aliniita kwa ishara ya mkono, nikamfuata na kumwinamia...
“Naamini ni Bertha, kama ndiye mwambie hujui nilipo.”
“Mh,” niliguna kwanza...
“Unadhani hajasikia ulivyokuwa ukipiga mayowe yako?”
“Hata kama...”
“Ngo...ngo...ngo,” mlango uligongwa tena, nikaenda kufungua..
“Niitie dada nina shida naye mara moja.”
Moyo ulinilupika lip! Maneno ya Bertha yalimaanisha ana uhakika shemeji
yuko chumbani kwangu...
“Alikwambia yuko huku kwangu?”
“Bwana nini, kwani mwenyewe sijamsikia?”
Nilijua nikigeuka kumwangalia shemeji ili anipe mwongozo, Bertha angejua
namwangalia yeye, lakini pia nilijua shemeji naye pale kitandani alikuwa ana
shauku ya kuniambia kitu kwani maneno ya Bertha aliyasikia waziwazi...
“Huku hayupo wewe, ondoka bwana.”
“Au niingie kwa nguvu niongee naye mwenyewe..?”
“Kwani una shida naye gani?”
“Najua mimi...”
“Basi huingii kama hutaki kuniambia...” nilisema lakini nikajua
nimechemsha, kauli yangu iliashiria shemeji yumo ndani...
“Hamtaki eee, shauri zenu,” alisema huku akiondoka.
Nilifunga mlango nikageuka kumwangalia shemeji, alikuwa akishuka
kitandani huku akisema...
“Huyu mtoto ananitafuta sana, au unatembea naye nini?”
“Hamna baby...”
“Mbona anajiamini sana kwangu?”
“Huyu mtoto hamnazo sweet...”
“Kwangu anafikia mwisho leo, sidhani kama ataendelea kuwa hapa nyumbani
kwangu...” shemeji alisema akiwa anafungua mlango na kutoka.
Nilibaki natetemeka kwa mambo mawili. Kwanza, kukatishwa mechi wakati
ndiyo kwanza mpira ulianza kunoga. Pili, nilijua Bertha ataanika uovu wetu kwa
kaka. Nilibaki nasikilizia kwa mbali.
Dakika kumi zilipita nikiwa chumbani, mara simu yangu iliingia meseji,
nikaifungua kuisoma...
“Sweet njoo ule chakula kitapoa.”
Nilitoka hadi kwenye chumba cha kulia chakula, nilikuwa peke yangu,
nilikula chakula mpaka nikashiba, sikumwona shemeji wala Bertha.
Nilienda kukaa sebuleni, mara nikawaona wanaingia wote wakitokea nje...
“Jamani vipi?” nilimuuliza shemeji...
“Huyu mtoto shemeji ana matatizo, leo  ndiyo nimegundua...”
“Kafanyaje?”
“Twende chumbani kwako tukaongee shemeji.” Shemeji aliniambia huku
akimwangalia Bertha ambaye alikuwa akiangusha tabasamu laini...
“Dada bwana...” alisema Bertha bila kufafanua alichomaanisha kusema ‘dada
bwana’.
Nilisimama, tukaongozana na shemeji hadi chumbani kwangu...
“Kwani kuna nini baby, mbona wewe umakasirika lakini msichana wako
anaonekana amejaa amani na tabasamu..?”
“Shemeji...” shemeji alianza kwa kuita, nikashangaa kumsikia anaita
‘shemeji’ badala ya darling, dear, sweet, ba baby, honey au mpenzi...
“Naam shemeji...”
“Wewe, umeniitaje..?” shemeji alinijia juu huku akinioneshea kidole...
“Si nimekuita shemeji...”
“Kwanini, tulikubaliana nini mimi na wewe?”
“Mbona hata wewe umeniita hivyohivyo sweet?”
Shemeji aliachia tabasamu, nikamwelewa kwamba anakiri na yeye alikosea...
“Enhe, niambie, tatizo nini shemeji?”
“Unajua shemeji, Bertha bwana nahisi ana lengo la kutuharibia uhusiano
wetu na naamini yuko njiani kufanya hivyo ikibidi hata kutoroa atoroke...”
“Kivipi honey?”
“Nimemtoa nje, nikamuuliza alikuwa ananitafuta kwa ajili ya nini, akasema
nani kaniambia alikuwa ananitafuta...nikamwambia si ulikwenda chumbani kwa
shemeji, akasema mbona wewe ulikataa mimi sipo, umeniambia saa ngapi?”
“Du!” nilishtuka mimi, nikaendelea...
“Enhe, akasemaje?”
“Hakusema alichokuwa akiniitia...”
“Sasa sweet unadhani nini kifanyike ili kumzuia na lengo lake hilo.?”
Shemeji alijiinamia kwa muda, kisha akasema...
“Unajua mbaya zaidi ana simu ya kaka yako, nikisema nimfukuze atampigia
kumwambia kila kitu...
“Mh!” niliguna kwanza...
“Sasa dear tufanyaje?”
“Mimi nina wazo moja, lakini linaniuma sana...”
“Lipi hilo?”
Shemeji alikata shingo akaniangalia sana usoni huku macho yake yakionesha
dalili ya kuishiwa nguvu...
“Unajua nini honey..?”
“Sijui...”
“Mimi nakuhitaji kwa hiyo sipendi kukupoteza. Unajua nilichokigundua kwa
huyu msichana anakutaka...”
“Ah! Ananitaka mimi au..?”
“Wewe ndiyo...”
“Aaaa wapi! Hanipati hata afanyaje!”
“Kweli baby..?”
“Naapa, eee, hanipati! Weee, mimi niko makini ile mbaya.”
Nilimwona shemeji akicheka kisha akaniangalia tena  kwa macho yaliyojaa matamanio...
“Sikiliza shemeji...”
“Nakusikiliza...”
“Ili mambo yetu yaende sawasawa bila matatizo mimi naomba sana mtongoze
kisha ulale naye...”
“Haa! Shemeji, una maana gani sasa? Mimi na wewe basi?”
“Hapana, ila ndiyo salama yetu baby. Bila hivyo hatuwezi kuwa salama
atasema tu. Halafu jina la shemeji usilirudie tena kuliita.”
“Mh! Sweet  unajua ni mchafuchafu
sana yule...”
“Najua...najua, lakini hivyohivyo...”
“Je akikataa..?”
“Hana ubavu huo. Hata huko kutufuatafuata ni kwa ajili ya kukupenda
wewe...”
“Mh!”
“Usigune darling.”
“Duu! Nitajaribu baby...”
“Siyo utajaribu, nataka utende na hivi sasa natoka naenda mtaa wa pili
kwa rafiki yangu ili mpate uhuru, uhakikishe unamtongoza lakaini...”
“Sawa shemeji.”
 Shemeji alisimama kitandani,
akauendea mlango, akafungua na kutoka zake. Alionesha dalili za kuumia moyoni,
lakini hakuwa na namna, ilibidi amwachie Bertha naye achze na mimi.

****
Nikiwa katikatika ya mawazo, mlango wa chumbani kwangu uligongwa...
“Karibu ingia.”
Aliingia Bertha akiwa amejifunga khanga moja tu. Hapo ni dakika kumi
baada ya shemeji kuondoka...
“Wewe unataka nini?”
“Niazime kitana kidogo.”
“Nani amekwambia kipo kwangu?”
“Kama huna si useme tu...”
“Sina.”
“Haya, asante na pole kwa usumbufu,” aliseka akiushika mlango kutoka...
“Hebu njoo,” nilimwita. Akageuka na kuja, akasimama...
“Unasemaje?”
“Shemeji yupo wapi?”
“Kaenda kwa mama Chris...”
“Wapi?”
“Mtaa wa mbele huko.”
“Anarudi muda gani?”
“Mh! Akiendaga huwa anakaakaa sana.”
“Wewe una kazi gani?”
“Nafanya usafi.”
“Njoo tulale kidogo basi...”
“Aaah! Akijua je?”
“Hawezi bwana, njoo,” nilimvutia kwangu, akaelekea huku akisema...
“Mimi naogopa bwana, dada anaweza kujua ikawa shida.”
“Hamna bwana, hawezi, labda umwambie wewe.”
Bertha alisimama akaufuata mlango na kuufunga kwa kitasa kwani mara ya
kwanza aliufunga lakini bila kitasa, kisha alirudi.
Bila kutarajia, nilishangaa kumwona anasimama huku akivua nguo moja baada
ya nyingine...
“Lakini usije ukamwambia dada,”
Ukitaka usalama kwa kaka yako na mimi niburudishe,” alisema wakati
anamalizia nguo ya mwisho na kuitupa chini kwenye kapeti.
Alikuja kitandani, akapanda lakini huku akionekana kuogopaogopa wa mbali.
Kwa kutumia maelezo ya shemeji sikuwa na sababu ya kumchelewesha,
nilimpandisha kitandani kisha nikamwanzishia mechi ya ufunguzi.
Bertha hakuwa msichana wa kufundishwa jambo lolote kwani aliujua mchezo
wote na masharti yake. Mimi nilitarajia angekuwa akitumia sheria za mpira wa
kikapu kwenye mpira wa miguu, lakini sivyo. Alijua kila kitu, alijua akiwa
mbele peke yake atakuwa ameotea, atapigiwa filimbi, alijua kukaba na alijua
kutumbukiza magoli ulingoni.
Alicheza mechi na mimi hadi akanishinda kwa ‘ati triki’ kwa kufunga
magoli matatu.
Tulipomaliza, alisema amefurahi sana kuliko siku zote, lakini
akaniambia...
“Unajua najiamini kwa sababu dada ni mke wa mtu kwa hiyo hawezi kula
kotekote wakati sisi tupo na tuna njaa zetu.”
Nilijikuta nikimpenda Bertha ghafla kwani alikuwa ‘mzuri’ uwanjani kuliko
shemeji, alichokosa yeye ni uzuri wa kuumbwa tu. Lakini si kwamba alikuwa mbaya
saaana kama wengine, ila sopsop. Kwa hiyo kila mmoja alikuwa na kasoro yake.
Mara simu yangu iliingia meseji, shemeji alituma...
“Yaani hapa nilipo shemeji roho inaniuma mpaka basi, lakini inabidi iwe
hivyo ili tuwe salama, nakuhitaji sana shemeji.”
Nilikaa sawa kitandani, nikamjibu...
“Nakupenda sana wewe kuliko Bertha...”
“Asante sana honey, lakini vipi, anaujua mchezo kama mimi?”

“Aaa! Wapi! Wewe mkali baby...”
“Teh! Teh! Teh..!
“Huyo si katoka kijijini juzijuzi, hawezi kujua mambo mengi, lakini vipi,
si kama gogo?”
Nilihisi shemeji anatafuta kujiumiza mwenyewe kwani maswali yake mengi
yalikuwa ya kutaka kujua huku mimi nikifahamu kwamba Bertha alikuwa mkali
kupita yeye halafu mbaya zaidi mimi sikuwa mtu wa kukatakata kona kumridhisha
mtu na kitu ambacho hakipo...
“Kusema ule ukweli my dear huyu mtoto anajiweza kitandani, si gogo, anajua
kujizungusha kama pia, ila akijitahidi akawa msafimsafi, atakuwa tishio, maana
mambo yake huwezi kuyategemea, ni mkali f’lani.”
Meseji hii nilipomtumia shemeji, ilichukua dakika mbili nzima kurudisha
majibu, nikajua imemuumiza.
Mara majibu yaliingia, yalikuwa hivi...
“Mh! Ina maana wewe umemuona huyo anaweza kuliko mimi lakini hutaki
kuniambia siyo? Mara hii unanisaliti? Mimi sijapenda, huyo ni mtoto tu kwangu
hanifikii hata chembe ila...”
Meseji hiyo ilikatika halafu ghafla ikaingia nyingine...
“...some text missing...”
Sikuelewa maana ya neno hilo lakini ni meseji iliyotoka kwa shemeji,
nikashindwa kujibu, nikamtumia hii...
“Kwa hiyo baby umekasirika siyo?”
“Sijakasirika, kwani hujasoma meseji yangu mwisho huko..?”
“Nimesoma,” nilimjibu nikijua nilichosoma mwisho ni ‘so text missing...’
“Nikuulize swali sweet?” alinitumia shemeji muda huohuo, nikamjibu uliza
honey...
“Umekwenda mara ngapi kwa Bertha?”
Lilikuwa swali rahisi sana kwangu, nikamjibu mara moja tu...
“Na babo yupo chumbani kwako?”
Niliamini nikisema katoka, si ajabu yeye anaingia ndani muda huo, ingawa
pia nilijua nikisema yupo ataumia, nikajipa moyo, nikamjibu ukweli...
“Amejaa tele, anasema anapumzika kwanza...”
“He! Huyo mtoto vipi, amepewa lifti anataka kupiga na honi? Mtimue haraka
sana  mi nakuja, nitakuweka vibao
nikimkuta...”
“Mbona unatuma sana meseji, unamtumia nani?” aliniuliza Bertha kwa uso
mkavu...
“Kuna mtu...”
“Wa wapi?”
“Nyumbani...”
“Dodoma..?”
“Eee...sasa sikiliza, wewe ungeondoka...”
“Niende wapi?”
“Kaendelee na kazi zako, shemeji anaweza kuja...”
“Hamna, nilikwambia akiendaga kwa huyo rafiki yake huwa anachelewa
kurudi. Mi namjua,” alisema Bertha akipeleka mkono wake wa kulia kwenye ‘makao
makuu’ yangu, nikashtuka, akaachia tabasamu huku akisema...
“Nini sasa jamani, yaani kuguswa kidogo tu, je ingekuwa hivi..?” hapo
aliishika maiki, nikajikuta nikiishiwa nguvu kabisa, nikamlalia.
Bertha alijigeuza na kulala chali, mimi nikawa ubavuni kwake. Hakutaka
kuchelewesha mechi nadhani alijua shemeji anaweza kutokea muda wowote,
alinivutia kwake na kunikaribisha ambapo nilimkuta ameshajiandaa tayari kwa
kuingia uwanjani.
Mechi hii ya dakika za nyongeza ilikuwa nzuri, kila mchezaji alionesha
uwezo wake awapo uwanjani, mpira ulikuwa hautulii upande mmoja wa uwanja.
Baada ya dakika tano, Bertha alibahatika kutumbukiza mpira golini,
tukaanza upya katikati ya uwanja, mpira ukaenda kwake, ukarudi kwangu, mara
akataka kufunga la pili, lakini nikamzuia ili na mimi niandike goli la
kusawazisha, ikawa hivyo, lakini katika hali ya kushangaza mpira ulipoanza
tena, Bertha alinifunga goli la tatu katika dakika za mwanzo na mpira ukaisha
kwa matokeo hayo.
“Sasa nenda,” nilimwambia.
Alitoka kitandani na kutua chini huku akichekacheka, alichonishangaza
Bertha aliweza hata kusema asante.
Alipoondoka, nilichukua simu ili kusoma meseji mbili ambazo ziliingia
wakati sisi tupo uwanjani...
“Vipi, ameshaondoka baby?”
“Ndiyo honey, katimua zake.”
“Mimi nakuja muda si mrefu.”
“Poa.”

***
Baada ya nusu saa, mlango wa chumbani kwangu ulisukumwa, akaingia
shemeji...
“Dear, unajua umemsahau  kaka
yako?”
Shemeji aliniambia jambo ambalo liligonga kichwani mwangu, nikatoka
kitandani na kusimama...
“Hivi kweli shemeji?”
“Ee, leo umeonana naye mara ngapi?”
“Mara moja asubuhi...”
“Sasa hebu fikiria, umekuja kwa ajili yake halafu hamuonani, twende
bwana, nitajua jinsi ya kumtuliza kama atakuwa anshangaa.”
Tulitoka kwangu na shemeji akiwa amenishika mkono mmoja hadi chumbani kwa
kaka, akanikalishha kwenye kiti jirani kabisa na kitanda...
“E bwana vipi, nilijua umekwenda kutembea saa hizi, maana vijana nyie
bwana,” alisema kaka.
“Yupo, anasema kichwa kina mgongagonga,” shemeji alinitetea.
“Oo, pole sana. Umekunywa dawa sasa?”
“Nimekunywa kaka, kidogo najisikia hata unafuu.”
Shemeji aliondoka, nikabaki na kaka tukiendelea kuzungumza mambo
mbalimbali kuhusu maisha, lakini akafika mahali akaniambia...
“Mdogo wangu...”
“Naam kama...”
“Unajua kuwepo kwako hapa mimi kwangu ni faraja kubwa sana...sidhani kama
unalitambua hilo?”
“Nalitambua kaka.”
“Enhee, nasema hivi kwa sababu, unajua kwa hali yangu hii hata kumtimizia
shemeji yako hitaji lake la mwili siwezi...”
Kaka alipofika hapo nilihisi anataka kunipa ruksa kutembea na shemeji ili
nimpe hitaji lake la mwili. Yaani niliamini kwamba kwake ilikuwa bora mimi na
mkewe tutembee kuliko atoke nje ya nyumba, akaendelea...
“Kwa hiyo hakikisha unambana sana, asiwe mtu wa kutokatoka nje ya
nyumbani peke yake. Ukimwona anataka kwenda wapi sijui, mwambie muongozane
wote.”
Mara shemeji aliingia, lakini hakusema neno zaidi ya kusikiliza kutika
kwetu...
“Hata akitaka kwenda kwenye harusi au kitchen party naomba uende naye,
utakuwa ndani ya gari hadi atakapomaliza ili mrudi wote, sawa mdogo wangu?”
“Sawa kaka.”
“Yaani ulinzi wote huo napewa mimi?” alihoji shemeji huku
akichekacheka...
“Nani mwingine?” alidakia kaka...
“Mimi sina wasiwasi, najiamini. Kama nitakuwa na mlinzi ambaye ni shemeji
yangu nashukuru zaidi, kujiamini kutaongezeka,” alisema shemeji kwa sauti yenye
furaha, moyoni nilimwambia kaka...
“Ungejua...”
Shemeji aliniangalia, tulipokutana macho akasema kwa ishara ya kupanua
midomo...
“Nakupenda sana.”
Nilimtupia macho kaka ambapo alikuwa amelala kuangalia ukutani, kwa hiyo
hakuona kitendo cha mkewe...
“Hata mimi,” nilimjibu shemeji kwa staili ileile aliyoitumia yeye
kuniambia ananipenda...
“Mume wangu unakumbuka jana nilikwambia saa mbili usiku leo nitakwenda
kwenye kitchen party ya Dorothea?” shemeji aliongea na mumewe, mimi nikashtuka
kwani hakuwahi kunidokeza kuhusu kutoka nyumbani usiku huo...
“Nakumbuka, nenda,” kaka alimjibu shemeji bila kusema anataka aende na
mimi.
Mimi niliaga nikaondoka kuelekea chumbani kwangu huku nikiamini kuwa,
shemeji alitaka kwenda kwa mwanaume wa nje ndiyo maana hakuniambia kuhusu
safari hiyo.

***
Usiku wa siku hiyo ulikuwa wa mawazo kwangu, toka nilipojitupa kitandani
nilikuwa nawaza mambo mengi kuhusu shemeji na msichana wake, Bertha.
Niliamini Bertha yeye anajijua ni mwizi kwa shemeji lakini hakujua kama
shemeji huyohuyo ndiye aliyeridhia mimi na yeye tufanye mambo machafu kama
yale.
Aidha, niliendelea kuamini kuwa shemeji muda huo wa usiku alikuwa tayari
kwa mwanaume mwingine ndiyo maana hata meseji hakunitumia wala kuja chumbani
kwangu kama mazoea yake. Niliminya simu ikatoa mwanga, nikaangalia muda,
ilikuwa saa tatu kasoro robo.
Nikiwa nautafuta usingizi, mara nikasikia kitasa cha mlango kikishikwa na
kuzungushwa, nikashtuka na kutupia macho mlangoni ingawa kulikuwa giza...
“Nani?” niliuliza, lakini ilionesha aliyeshika kitasa hicho hakutaka
kutoa sauti kwani aliendelea kukizungusha tu bila mpangilio.
Nilitoka kitandani kwenda kufungua mlango nikiamini ni Bertha...
“Huyu mtoto hachoki tu..?” nilisema moyoni.
Aliyesimama mbele yangu baada ya kufungua mlango ni shemeji. Alikuwa
ananukia sana pafyumu, alivaa gauni zuri lililomfika juu kidogo ya magoti...
“Vipi baby?” aliniuliza huku akinipiga kofi dogo la shavu la kushoto
kwangu, akaingia ndani na kuwasha taa...
“Tulale chapchap shemeji, nitakuwa na wewe hadi saa saba usiku wa leo
ndiyo nitarudi chumbani kwa kaka yako...”
“Kaka je?”
“Si nilimwambia nakwenda kwenye kitchen party, wewe hukujua maana yangu
nini?”
“Sasa ukirudi si atataka kusikia mlio wa gari?”
“Gari liko nje, nikitoka hapa natoka nje kwanza kisha najifanya ndiyo
ninarudi...”
“Mh! Nje pana usalama kweli?”
“Huku hakuna wezi, wala usiwe na wasiwasi na hilo,” alisema shemeji.
Kusema ule ukweli alipendeza sana usiku huo, alionekana kama malaika kwa
uzuri wa sura na ngozi yake na zaidi ya kupendeza alivutia na kutamanisha kwa
mwanaume yeyote rijali.
Shemeji alivua lile gauni mbele yangu huku akiniangalia kwa macho
yaliyojaa uchu...
“Sweet nimekwambia chapchap tulale, nataka kulala na wewe leo mpaka saa
saba usiku huu.”
Mimi sikuwa na sababu ya kuvua nguo kwani nilipopanda kitandani kulala
mara ya kwanza nilikuwa na bukta tu. Kwa hiyo alipomaliza yeye na kupanda
kitandani na mimi nilimfuata.
Shemeji alinishikashika, akanikumbatia kwa nguvu zake huku akinitwanga
mabusu ya kufa mtu.
Hapo tulikuwa tumeshazima taa. Kwa hiyo mambo yote ya kushikanashikana na
kupapasana yalikuwa yakifanyika kwenye giza nene lakini papo kwa papo.
Tulitembezeana mikono kwa muda mrefu, ikafika mahali kila mmoja akawa
tayari kwa mchezo. Shemeji alinivutia kwake na mimi nikaelekea na kuanza
mpambano.
Ulikuwa mpambano wa kukata na shoka kwani kila mmoja alionekana kutaka
kufurahi zaidi ya mwenzake. Shemeji alikuwa akicheza mchezo huo huku akiongea
yote ya kutoka moyoni mwake kuhusu mimi...mara aniambie nisimwache, mara aseme
hataki kusikia natembea tena na Bertha, mara adai atanipangishia chumba
niendelee kuishi Dar, kuna wakati alisema atahakikisha kila siku analala na
mimi usiku mpaka saa saba.
Lilipoisha hilo, akaingia hatua nyingine. Hii naweza kusema ni hatua ya
chumbani zaidi kuliko ile ya awali kwani sasa shemeji alipenda tuzungumzie kila
kitu kuhusu kile tulichokuwa tukikifanya wote, yaani mpambano.
Alikuwa akiniuliza maswali kwa sauti tamu na yenye mvuto ambapo mimi
nilimjibu.
Hali hiyo ilitufikisha mahali tukatangaza kufika juu ya mlima kwa pamoja
na tukafika kweli.
Tukiwa tumemaliza mpambano na tumepumzika huku tukiongea mawili matatu
kuhusu penzi letu, mara mlango ukagongwa kwa mbali...
“Ha! Atakuwa nani huyo?” nilimuuliza shemeji...
“Mh! Hakuna kuuliza, huyo ni Bertha...”
“Mh! Kweli?”
“Eee, huyu mtoto anataka kuchonga mzinga.”
Lakini kwa sauti tuliyokuwa tukiitumia kuongea mle chumbani haikuwa
rahisi aliyesimama nje kutusikia...
“Sasa nifanyeje dear?” nilimuuliza shemeji ambaye alikuwa ameniwekea
mkono kufuani...
“Nyamaza kwanza tuone.”
Tulinyamaza wote kwa dakika kama moja, mlango ukagongwa tena...
“Ngo ngo ngooo...”
“Huyu mtoto nikitoka hapa naweza kumpiga mpaka akazimia,” alisema shemeji
kwa sauti iliyojaa hasira.
Mara mlango ukaachwa kugongwa, kikazungushwa kitasa...
“Kwacha kwacha kwacha...”
Shemeji alinisogelea sikioni nikiamini anataka kuniambia jambo, lakini
cha ajabu akanibusu na kuomba ulimi wangu. Nilijua lengo lake kuu ni kumpuuza
msichana wake wa kazi....
“Kwacha kwachwa kwacha...” kitasa kilizungushwa tena na tena kwa
mfululizo...
“Toka muulize anachotaka, akisema anataka kuingia mwambie unaogopa mimi
nitakuja kuwafumania,” shemeji aliniambia.
Nilitii, nikatoka kitandani na kuufuata mlango. Nilifungua na kumkuta
Bertha amesimama katikati akiwa amejifunga khanga moja tu...
“Njoo huku nikwambie kitu,” alisema akinishika mkono na kunivuta,
nikatoka...
“Twende chumbani kwangu nikakwambie jambo zito sana, sidhani kama utaweza
kulipokea moyoni mwako,” aliniambia Bertha akiendelea kunishika na kunivuta,
tulikwenda hadi chumbani kwake.
Aliwasha taa akaniambia...
“Kaa hapo kwanza...”
“Niambie unachotaka kuniambia...” nilimjia juu nikiwa nimesimama.
Cha ajabu, Bertha aliniparamia kwa nguvu na kunikumbatia huku akisema...
“Nimekumisi sana mwenzio, njoo tulale wote bwana ah!”
Nilijitahidi kumtoa mwilini mwangu ikashindikana, akanilazimisha nimpe
ulimi kwa yeye kupanua kinywa chake mbele ya midomo yangu, lakini nikazuia.
Kujiondoa kwake sikushindwa ila nilijua ingetokea vurugu kiasi cha kaka kusikia
maana vyumba vyao vilipakana...
“Hutaki ee...hutaki siyo?” aliniuliza kwa sauti ya vitisho..
“Sitaki ndiyo, we unasemaje sasa?”
“Nitamwambia dada ulinitongoza nikakukatalia...”
“Mwambie,” nilimjibu nikianza kutoka, lakini kabla sijafika mlangoni alinishika
tena na kunivutia kwake, nikarudi kwa kasi, akanikumbatia, shemeji akasukuma
mlango na kuingia...
“Baby mnafanya nini humu chumbani?” shemeji aliniuliza akiwa amesimama,
uso wake ulijaa hasira, lakini hofu pia alikuwa nayo...
“Baby, huyu msichana wako wa kazi siye, amenifuata chumbani akanishika
mkono, akaniambia nije huku aniambie kitu, kufika akasema anataka alale na
mimi, si ndiyo nikawa natoka, akanishika kwa nguvu...”
“Martha...”
“Abee...”
“Ni kweli...”
“Mh! Muulize vizuri huyohuyo baby wako, si nyie ni mababy...”
“Martha unajua naweza kukuumiza...”
“Sasa dada mimi niseme nini, nyie mababy mmeulizana wenyewe, mimi yangu
masikio tu.”
Shemeji alinishika mkono na kunivutia nje. Tukarudi chumbani kwangu.
Nilijua alikuwa mpole kwa sababu muda huo mumewe alijua yupo kwenye kitchen
party, sasa endapo angelianzisha na akabainika yumo ndani ingekuwa tabu kwake.
“Sweet unajua imefika mahali Martha lazima aondoke hapa nyumbani...”
“Umeona ee?” nilimkubalia shemeji...
“Ndiyo, atatuletea matatizo lazima. Mi namjua huyu binti, dalili
zinaonesha anataka makubwa zaidi ya hapa.”
“Ni kweli mama.”
Shemeji alishaingia woga, akasema hajisikii kuendelea kuwa na mimi
chumbani kwangu...
“Sasa sikia, mimi itabidi nitoke, naingiza gari najifanya shughuli
imeisha mapena, nina wasiwasi huyu binti anaweza kwenda kumgongea kaka’ako
akasema yote...”
“Kwani anajua uko chumbani kwangu?” nilimuuliza shemeji...
“Atakuwa anajua tu, mi namfahamu huyu mtoto, mpekepeke sana.”
Niliwaza na kuwazua nikakubaliana na yeye, nikamkubalia aondoke. Wakati
anaondoka, shemeji alinipiga mabusu kama matatu, akaomba denda kwa karibu
dakika moja, akanitakia usiku mwema na kuondoka.
Nilipanda kitandani kulala nikiwa na ghadhabu na Martha kwani niliamini
ananiwekea kiwingu cha penzi langu kwa shemeji...
“Ngo...ngo...ngo,” mlango uligongwa.
Nilijua ni Martha kwani kama ni shemeji asingegonga, angeingia maana
alitoka muda huohuo. Nilitoka kitandani kwenda kufungua mlango...
“Nimemuona dada akitoka humu kwako naomba niingie mimi sasa, hawezi
kuja,” alisema Martha akijipenyeza na kuingia.
Nilimwachia, kwani hata mimi niliamini shemeji hawezi kurejea tena, pia
kwenye mechi yangu na shemeji niliishia njiani kwa hiyo ujio wa Martha kwa
namna moja au nyingine ulikuwa wa kunimalizia kiu yangu.
Nilifunga mlango kwa funguo, nikarudi kitandani ambapo Martha alishapanda
siku nyingi na alikuwa amejivua khanga moja aliyokuja nayo.
Nilimmiliki Martha, akamilikika, mechi ikaanza kwa kishindo huku
mashambulizi yakiwa sawa kwa sawa, mpira ulipoanza kwake ulifika mpaka golini
kwangu, nilipookoa hatari ya goli niliupeleka hadi golini kwake.
“Mimi nataka uachane na dada ubaki na mimi tu, nakupenda sana mwenzio,”
aliniambia Martha akiwa anendelea kuokoa hatari kadhaa za magoli...
“Nitamwacha, hata mimi simtaki, kwanza mkubwa sana kwangu, nitaonekana
kiserengeti boi...”
“Si unaona, afadhali mimi ni saizi yako, si eti ee?”
“Eee.”
Mazungumzo yangu na Martha yalihitimika kwa yeye kuhubiri kupasua dafu,
nikamruhusu, lakini sijui ilikuwaje wakati anapasua na mimi nikapasua langu.
Kwa mara nyingine tena nilikiri kwamba Martha alikuwa anaujua mchezo
kuliko shemeji. Kwanza hakuwa na papara, pili alijua nini ninataka, ndiyo maana
kila alipovunja dafu na mimi nilifuatia.
Martha aliniomba tupumzike kidogo kisha tuingie dakika za nyongeza kabla
ya mechi kumalizika akiamini atapatikana mshindi baada ya droo ya mwanzo...
“Sawa, tulale kidogo basi,” nilimjibu, tukalala kwa yeye kugeukia
ukutani, mimi mlangoni, lakini usingizi ukatupitia na kulala moja kwa moja.
Mimi nilishtuka baada ya kitasa cha mlango kuzungushwazungushwa kwa fujo.
Niliminya simu na kuangalia saa. Ilikuwa saa kumi na moja na nusu...
“Mh! Huyo atakuwa shemeji tu,” nilisema moyoni. Nilimshtua Martha huku
mapigo ya moyo yakinienda kwa kasi...
“Nini bwana, mi nasikia usingizi,” alisema Martha bila kujua kuna soo...
“Amka, shemeji amekuja.”
Aliamka, akakaa kitandani...
“Yuko wapi?”
“Chakachaka, chaka...”
“Unasikia kitasa hicho, ni yeye tu,” nilimwambia Martha kwa sauti ya
chini sana...
“Mungu wangu, kwani kumekucha tayari?”
“Ee, saa kumi na moja na nusu sasa.”
“Mungu wangu, sasa itakuwaje?”
“Sijui, kimekunuka tayari,” nilimwambia nikitaka kutoka kitandani.
Mawazo yaliniambia nikafungue mlango, shemeji aingia, atakachokiona
ataamua mwenyewe, lakini akili nyingine iliniambia kitakachofuata ni mimi
kurudishwa Dodoma kuendelea kuuza genge langu ambalo mtaji wake ulikuwa kama
elfu sitini na tano tu.
Nilipata wazo, nilimrudia Martha kitandani, nikamwambia...
“Vaa khanga yako ingia chini ya kitanda.”
Naye bila kuuliza alitii, aliinyakua khanga iliyokuwa chini, akaingia
nayo chini ya kitanda bila kuivaa.
“Kwacha kwacha kwacha...” kitasa kiliendelea kuzungushwa. Ilionekana
mzungushaji alikuwa makini ili watu wengine mle ndani wasisikie.
Kabla sijafungua mlango lakini nikiwa naufuata, akili yangu ikawa na
maswali mawili. Je, shemeji alipitia chumbani kwa Martha na kukuta hayupo au
alikuja moja kwa moja kwangu..?”
Nilifungua mlango huku nikiwa sina majibu ya maswali yangu yote  mawili...
“Vipi sweetheart...” shemeji alinisalimia. Kauli hiyo ilinifanya nipate
majibu yangu. Nilijua hajaenda kwani kama angeenda angeingia na kauli hii...
“Yuko wapi huyu malaya?”
“Poa baby, nimekumisi sana.”
Shemeji alipoingia alinipiga kikumbo, nikaangukia kitandani huku na yeye
akifuata na kusema...
“Nataka mechi ya asubuhi kwa ajili ya kushinda fiti mchana kutwa wa leo,
lakini huyu Martha baby lazima nimkate sikio moja siku mbili hizihizi...”
Martha kule chini ya kitanda alikuwa akitetemeka kiasi cha kutokwa jasho
kwa wingi kama mtu aliyejimwagia maji wakati wa joto kali...
“Ina maana huyu dada amepania kunitia kilema siyo? Sitakubali,” Martha
alisema moyoni huku akishindwa kulala vizuri kutoka na uvungu wa kitanda kuwa
mdogo...
“Sweet mbona kama una mawazo?”
“Hata, wala sina...”
“Au umemmisi Martha?”
Nilipata wakati mgumu sana kulijibu hilo kwani nilijua nikisema wala
sijammisi, Martha kule chini ya kitanda angemaindi sana wakati ukweli ni kwamba
kutoka moyoni nilimpenda Martha kwa uwezo wake mkubwa kitandani kuliko shemeji.
Kwa hiyo sikumjibu lolote, akendelea...
“Lakini dear hebu niambie, mimi na Martha nani zaidi, please nijibu..”
“Kwenye nini?”
“Kitandani...”
“Ha! Ha! Ha! Sweetheart bwana...” nilisema ili kuzuga...
“Sweetheart nini, nimekuuliza nataka jibu sasa hivi kabla hatujaanza
mechi ya asubuhi niliyokuomba...”
Shemeji alinipa wakati mgumu sana, Martha kule chini alikuwa hakohoi,
akili zake zote zilikuwa kwetu, hasa kusikia nini tunaongea...
“Kwani wewe darling unaweza kujifananisha na msichana mdogo kama Martha
kweli?”
Niliposema hivyo, shemeji alinikumbatia, akanivutia kwake na kunipiga
busu.
Najua aliamini maneno yangu yalikuwa ya kumsifia yeye. Niliposema ‘kwani
wewe darling unaweza kujifananisha na msichana mdogo kama Martha kweli’ alijua
yeye ni zaidi. Lakini mwenzake lengo langu lilikuwa, yeye ni mtu mzima, Martha
ni msichana kwa hiyo kama ‘ufiti’ wa kitandani, alikuwa mzuri zaidi yake kwa
kuwa ana damu changa.
Shemeji aliendelea kunipiga mabusu, mwisho wa yote akaniomba denda. Hapo
kwenye denda sasa! Tulidumu kwa muda wa dakika karibu tano, alikuwa akigugumia
na mimi nikiguna kimahaba zaidi.
Huku nikijua kuwa Martha alikuwa katika wakati mgumu zaidi kule chini ya
kitanda, shemeji alizidi kusisimka kimahaba. Kilio chake sasa kilikuwa hakina
mpaka kwa mle chumbani, mbaya zaidi akawa anaongezea na maneno...
“Sweet...baby...yeees...oke...oke...”
Mimi niliyekuwa naye kitandani nilisisimka sana, je yeye aliyekuwa
akisikilizia masikioni?
Nilipenda kumwambia shemeji apunguze kelele, lakini akasema nimwache
ajiachie kwa raha zake...
“Ba...baby nia...che nijimwa...gemwage kwa...kwa raha zangu.”
Kuna wakati alizidisha spidi ya kuzunguka keep left nikajua sasa anakaribia
kufika juu ya Mlima Kilimanjaro...
“Sweet...” aliita shemeji, sikuitika nikijua nitakuwa nampa kichwa au
kiburi hivyo angesema maneno mengi ambayo yangezidi kumpa wakati mgumu
Martha...
“Kohokoho,” kule chini Martha alikohoa bwana.
Shemeji alishtuka kidogo, akapunguza kasi ya mzunguko wa keep left...
“Kama nimesikia mtu akikohoa dirishani...”
“Hata mimi, lakini atakuwa mpita njia,” nilimjibu.
Ili kuonesha nilichokuwa nakisema mimi hata yeye amekiunga mkono, shemeji
aliongeza spidi, safari hii ilikuwa kali kuliko ya awali...
“D...”
“M...”
“Nikikuita mume wangu si sawa tu...?”
“Sawasawa...”
“Basi na wewe niite mke wangu...”
“Haya mke wangu.”
Nilimwona shemeji akiachia tabasamu lenye mahaba licha ya kwamba tulikuwa
‘kazini’.
Shem akatangaza kuvunja dafu, tukaenda sambamba huku mimi nikisema moyoni
afadhali maana kule kukohoa kwa Martha kulinipunguza spidi na makeke. Niliamini
anaweza hata kujitokeza na kusema chochote maana akili zake zinajulikana.

***
Shemeji alipumzika kwangu kama dakika tano baada ya mechi, akaniaga kwa
kunibusu huku akisema siku hiyo jioni atanitoa ‘out’ nikaoshe macho,
nikamwambia poa.
Baada ya kutoka, nilimtoa chini Martha nikimwambia aondoke kwani nilijua
safari ya shemeji ingeenda kukwamia chumbani kwake na kama asingemkuta ingekuwa
tabu...
“Sitaki, na mimi nataka kidogo, unadhani kule chini nilikuwa na hali
gani?” alisema Martha...
“Haitawezekana, ujue shemeji anakwenda chumbani kwako na kumekucha
tayari,” nilisema nikamsukuma...
“Halafu nyie si mlikuwa mnajifanya siyo wapenzi, leo imekuwaje?” alisema
Martha huku akitoka kwa hasira. Hilo mimi sikulijali ilimradi alitoka kama
nilivyotaka.
Nilitoka hadi kwenye kona moja ndani, nikasimama kwa kusikilizia, nilijua
shemeji angesikika, au akimwita kwa jina Martha, au akiuliza aliko baada ya
kumkosa chumbani mwake...
“We dada...”
“Abee...” niliwasikia...
“Hivi tangu umeamka umefanya kazi gani, mbona usafi bado?”
“Nimechelewa kuamka dada...”
“Kwa nini?”
“Usingizi, usiku sikulala, nimekuja kulala muda huuhuu...”
“Kwa nini, wewe ni mwanga?”


“Hapana dada, mimi si mwanga, kuna mambo yananiumiza kichwa...”
“Yapi hayo?”
“Yanahusu mapenzi...”
“Mapenzi, una akili wewe? Yaani mawazo yako kuhusu mapenzi ndiyo uniletee
nyumbani kwangu mimi na kuharibu kazi?”
Sikumsikia Martha alichojibu, ila nilimsikia shemeji akisema kwa sauti ya
chini...
“Sasa ndiyo unataka kutumia nafasi hiyo kuniharibia au?”
Baada ya hapo nikasikia ukimya wa hali ya juu. Nilirudi chumbani kwangu
na kujitupa kitandani nikiendelea kuwaza...
“Hivi mimi napendwa au kwa sababu humu ndani ni mwanaume peke yangu?”
“Shemeji atoke chumbani kwake hadi kwangu kulala, Martha naye ndiyo
hivyo, amefikia hatua ya kuning’ang’ania, lakini si mbaya ilimradi wote
nawaridhisha bwana.”
“Ngo ngo ngo...”
“Nani?”
“Maji ya kuoga tayari,” ilikuwa sauti ya Martha...
“Oke nakuja.”
Nilijifunga taulo nikaenda bafuni kuoga. Tofauti na siku zote, nilikuta
maji ya moto, matamu sana kwa kuoga...
“Mh! Leo shemeji amezidisha mapenzi, kanitengea maji ya moto...”
“Naona ameamua kuongeza mapenzi zaidi ili aninase vizuri, anahisi
atapinduliwa na Martha...” nilisema moyoni huku nikiwa na furaha ya kupitiliza.
Ile najimwagia maji makopo mawili tu, mlango wa bafuni ambao niliuacha
wazi, ukasukumwa...
Chombezo na Irene Mwamfupe Ndauka tukutane tena hapa ndani ya Blog muda wote..

3 comments:

  1. jamani watamuua huyu kijana hawampi nafasi

    ReplyDelete
  2. Sasa yale mameno ya kuambiwa na Martha kuwa Kaka yake ameathirika ni ya kweli au maana hata hayawazii kabisa.

    ReplyDelete
  3. duh kama kakake ameatirika itakua wameathirika woteeeee, ila kijana apate mambo yetu yaleeee ya huku kwetu visiwaniii, mambo ya kitu cha miks supu ya pwezzzaaaa ili anagalau ajirudi na haliii adhawayz watamuuaa

    ReplyDelete

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate