EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, July 20, 2012

Ujenzi wa mji mpya wa Kigamboni: Dkt. Ndugulle asema NITAPAMBANA

Mbunge wa Kigamboni, Dkt. Faustine Ndugulile, amesema kuwa licha ya kusimamishwa kuhudhuria vikao vitatu Bungeni kwa ajili ya kuwatetea wananchi wa Kigamboni, ataendelea kupambana kuhakikisha haki inatendeka kwa wakazi wa Kigamboni.

Akizungumza katika mahojiano maalum na gazeti la TANZANIA DAIMA, mbunge huyo alisema hapingi kuanzishwa kwa mji mpya wa Kigamboni, bali anapinga taratibu zilizotumiwa na serikali kutekeleza mradi huo.

Alisema suala la uendelezaji wa Mji Mpya unatawaliwa na Sheria ya Mipango Miji Na.8 ya 2007 ambapo sheria hii inaelezea kwa ufasaha taratibu zinazopaswa kuchukuliwa tangu hatua ya kutangaza kwa mradi hadi utengenezaji wa mpango kamili.

Kwa mujibu wa sheria hii, mchakato huu unapaswa kushirikisha wananchi katika kila hatua. Aidha, kifungu 24 (2) kinatamka bayana kuwa Mamlaka ya Kupanga Mji (Planning Authority) inaweza kusimamisha uendelezaji na ujenzi kwenye eneo la mradi kwa kipindi kisichozidi miaka miwili ili kutoa nafasi ya kuandaa mpango kamili.

Akizungumzia hali ilivyo, mbunge huyo alisema takriban miaka minne sasa tangu kutangazwa kwa kusudio la kujenga Mji Mpya wa Kigamboni. Serikali imeshindwa kukamilisha mpango kamili ndani ya miaka miwili kwa mujibu wa sheria.

“Kwa vipindi tofauti, mawaziri na watendaji wa Wizara ya Ardhi, Makazi na Maendeleo ya Nyumba wameshindwa kutoa majibu kamili kuhusu lini mradi huu unaanza; maeneo ambayo mradi utaanzia; viwango vya fidia na hatma ya waathirika wa mradi huu. Vile vile, wananchi hawajashirikishwa kikamilifu katika mchakato wa mradi huu kama Sheria ya Mipango Miji inavyotaka,” alisema Dkt. Ndugulile.

Akizungumzia madhara ya kuchelewa kwa mradi huo, Dkt. Ndugulile alisema umewaathiri kisaikolojia, kiuchumi na kisiasa kwa wakazi wa Kigamboni.

Alizitaja athari hizo kuwa ni pamoja na wananchi kushindwa kujenga na kukarabati nyumba zao, kushindwa kuuza nyumba na ardhi yao na kushindwa kukopesheka kwenye mabenki.

“Manispaa ya Temeke nayo imeathirika katika maeneo yafuatayo. Kushuka kwa mapato ya kodi za majengo, baadhi ya wananchi wameacha kulipa kodi za majengo na vile vile viwango vya tozo za kodi vimepungua baada ya kushuka kwa thamani za nyumba kutokana na uchakavu na kutokarabatiwa,” alisema mbunge huyo.

Katika hatua nyingine Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai, amedaiwa kukiuka Kanuni za Kudumu za Bunge kifungu (71) (2) (3) na (4) wakati alipomwadhibu Dkt. Ndugulile, asihudhurie vikao vitatu mfululizo baada ya kushindwa kuthibitisha tuhuma kwamba madiwani wa Halmashauri ya Manispaa Temeke walihongwa ili kuukubali Mradi wa Mji Mpya wa Kigamboni.

Ndugai alitumia kifungu cha 73 (3) ambacho kinampa mamlaka ya kumwadhibu mbunge aliyeshindwa kuthibitisha tuhuma alizozitoa, huku pia akiwa amekaidi kufuta kauli yake kuhusiana na tuhuma hizo.

Baadhi ya wanasheria na wabunge waliozungumza na gazeti hili walisema Ndugai alitumia jazba katika kufikia uamuzi huo na hivyo kukiuka utaratibu mzima wa kanuni za Bunge unaotumika kushughulikia malalamiko ya mtu asiye mbunge.

Ndugai alipaswa kutumia kifungu cha 71(2) na (3) katika kushughulikia sakata hilo la Dkt. Ndugulile na madiwani kwa kuwasilisha malalamiko hayo kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge ili kuyatafakari na kulishauri Bunge. Adhabu ya mbunge huyo inamalizika leo.

via TanzaniaDaima

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate