 
 
Waziri
 wa Uchukuzi Dkt. Harisson Mwakyembe amemsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu 
wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari-TPA-Ndugu Ephrahim Mgawe pamoja na 
wasaidizi wake wawili ili kupisha uchunguzi wa tuhuma zinazowakabili.
Wengine
 waliosimamishwa ni Meneja wa Mafuta ya Ndege Kurasini, Meneja wa JET na
 Meneja wa Oil Terminal kutokana na tuhuma za kupotea kwa mafuta na 
kuidanganya serikali kuhusu mafuta masafi na machafu.
Kutokana
 na kuwasimamisha kazi Wakurugenzi hao Dkt. Harisson Mwakyembe amemteua 
Injinia Madeni Kipange kukaimu nafasi ya Mkurugenzi Mkuu wa TPA.
Kufuatia
 tuhuma hizo zinazofanywa Bandarini Dkt. Mwakyembe ameunda Tume wa ya 
watu saba kufanya uchunguzi kwa wiki mbili na kumpelekea taarifa ofisini
 kwake ili kubaini ukweli wa tuhuma hizo zikiwemo za wizi.
Pia
 ameagiaza kufikia Septemba Mosi mwaka huu malipo yote yafanyike benki 
ili kuondoa rushwa na wizi unaofanyika ndani ya Mamlaka hiyo.
Waziri
 Mwakyembe anachukua hatua hizo kutokana na wwadao wengi sasa hawaitumii
 Bandari ya Dar es salaam kupitisha mizigo yao kutokana na kutokuwa na 
inami na watumishi wake hatua inayoifanya serikali kukosa mapato.
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment