EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, August 31, 2012

Mahakama yawaachia huru Wanachuo 51 wa UDSM

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam imewaachia huru wanafunzi 51 wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) waliokuwa wakikabiliwa kwa pamoja na mashitaka ya kufanya mkusanyiko usio halali tarehe Novemba 11 mwaka 2011, eneo la Mlimani la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kusababisha uvunjifu wa amani eneo la chuo hicho.

Wanafunzi hao waliachiwa jana na Hakimu Walialwande Lema aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo baada ya upande wa mashitaka ulioongozwa na Wakili wa Serikali, Ladslaus  Komanya kushindwa kuleta mashahidi mahakamani huku wakitoa sababu mbalimbali. Komanya alidai kuwa  washtakiwa hao wakiwa kwenye mkusanyiko huo haramu kwa lengo la kufanya mgomo, askari wa Jeshi la Polisi waliwataka watawanyike, lakini hata hivyo wanafunzi hao walikaidi amri hiyo na kudai kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika.

Hata hivyo washitakiwa hao ambao walifikishwa mahakamani hapo chini ya ulinzi mkali wa jeshi la polisi, walikana mashtaka hayo na waliachiwa huru baada ya kukamilisha masharti ya dhamana ya kuwa na mdhamini mmoja wa kuaminika ambaye alisaini bondi ya Shilingi milioni moja.

Baada ya kuachwa huru, wanafunzi hao waliondoka mahakamani hapo kwa furaha huku wakikumbatiana na wengine wakisali.

Akitoa uamuzi huo jana, Hakimu Lema alisema kuwa anatupilia mbali maombi ya upande wa mashitaka yaliyokuwa yakiomba ahirisho la kesi hiyo kwa mara nyingine wakidai kuwa mashahidi wao ambao ni askari wako katika Sensa ya Watu na Makazi.

Lema alisema kuwa sensa ni muhimu kama ilivyo kesi hiyo, lakini maombi yao hayakufuata taratibu za sheria ambapo kwa mujibu wa kifungu cha sheria cha 225 (4) Sheria ya  Mwenendo wa Mashauri ya Jinai (CPA), sura ya 20 kwa sababu upande wa mashtaka ulishindwa kuliendesha shtaka hilo.

“Agosti 13 mwaka huu kulikuwa na ahirisho ambapo sababu ilikuwa hakuna mashahidi kwa sababu wako katika mgomo wa madaktari, leo tena mnaleta sababu kuwa wako katika sensa inaonesha mmedharau amri ya Mahakama,” alisema Hakimu.

Alisema amri ya mwisho aliyoitoa ilikuwa ahirisho la Agosti 13 mwaka huu hivyo upande wa mashitaka umedharau amri ya Mahakama na kwa maana hiyo anawaachia huru washitakiwa wote chini ya kifungu cha sheria ya Mwenendo wa makosa ya jinai kifungu cha 225 (5) sura ya 20.

Awali wakili wa upande wa mashitaka, Prosper Mwangamila alidai kuwa kesi ilikuja kwa ajili ya kusikilizwa akaomba iahirishwe hadi Jumatatu. Wakili wa washitakiwa hao, Reginard Martin akijibu hoja hiyo aliiomba Mahakama kutokubali ombi hilo na badala yake kesi ifutwe washitakiwa waachiwe huru.

Baadhi ya majina ya wanafunzi walioachwa huru ni Mwambapa Elias, Evarist Ambrose, Baraka Monas, Hellen Moshi, Alphonce Lusako, Matrona Babu, Rolanda Wilfred, Godfrey Deogratius, Moris Denis and Evon Gumbi.Others are Lugiko Mathias, Ndimbo Jabir, Evarist Wilson, Cornel Rwaga Mushi, Mlazi Kumbuka, Rehema Munuo, Glory Masawe, Happy Amulike, Elias Mpangala, Frida Timothy, Stella Mofe, Betwel Martin, Mmasi Stephen na Lugemalila Venance na wengineo.
 
Taarifa via HabariLeo na Mwananchi

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate