Mkurugenzi
 wa Kitengo cha Biashara cha kampuni ya Precision Air, Patrick 
Ndekana(kushoto)akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na mkataba 
na Vodacom Tanzania ambapo wateja wataweza kulipia tiketi za usafiri 
kupitia huduma ya M-Pesa,kulia ni Mkuu wa kitengo cha huduma za fedha wa
 Vodacom Tanzania Bw. Innocent Ephraim.
*******
Kampuni
 ya usafiri wa anga ya Precision air hii leo imeingia kwenye mkataba na 
Vodacom Tanzania ambapo wateja wataweza kulipia tiketi za usafiri 
kupitia huduma ya M-Pesa.
Ili
 kufanya malipo mteja atatakiwa kupiga namba *150*00# na kuchagua malipo
 ya bili kupitia orodha ya M-pesa na kuingiza namba ya biashara ya 
Precision Air ambayo ni 333777  ikifuatiwa na namba ya malipo na kiasi 
cha fedha itakayolipwa.
Akizungumza
 wakati wa uzinduzi wa ushirikiano huo, Mkurugenzi wa Kitengo cha 
Biashara cha kampuni ya Precision Air, Patrick Ndekana, amesema kuwa 
njia hiyo ni ya haraka, rahisi na itaokoa muda kwa wateja.
 “Tunafurahi kuingia katika ushirikiano huu na Vodacom Tanzania, 
Tunawahimiza wateja wetu kutumia huduma hii ili kuokoa muda na kufanya 
malipo yao katika njia ambayo ni rahisi na ya haraka,” alisema Ndekana.
Kwa
 upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Huduma na Kifedha cha Vodacom 
Tanzania, Innocent Ephraim, alibainisha kuwa ushirikiano huo utatoa njia
 badala katika malipo ya tiketi, na kusisitiza kuwa huduma ya M- pesa ni
 salama, haraka na niya uhakika, kwa kuwa imeleta mapinduzi katika 
huduma mbalimbali za kifedha tangu kuanzishwa kwake miaka mimne 
iliyopita.
“Tunaamini
 kuwa tutatoa huduma bora kwa wateja wetu. Tunajivunia ushirikiano huu 
na tunatarajia utakuwa na mafanikio makubwa katika kukidhi mahitaji ya 
huduma kwa wateja wetu,” alisema Ephraim.
Huduma
 ya M-Pesa ya Vodacom Tanzania ina mawakala zaidi ya elfu 20,000 nchini 
kote, na ni pekee ambayo inaongoza, kwa usalama na ubora katika kukidhi 
mahitaji ya huduma za kifedha kwa Watatanzania walio wengi.
Kampuni ya Precision Air inatoa huduma zake katika mikoa mbalimbali ya Tanzania, na kufika katika maeneo mengi ya nchi kwa siku.
Sasa
 kampuni hiyo ina ndege tano zenye uwezo wa kubeba abiria sabini aina ya
 ATR 72-500, na ATR 42 yenye uwezo wa kubeba abiria arobaini na nane na 
ndege nyingine tatu aina ya Boeng 737. Na sasa iko katika mpango wa 
kuongeza ndege nyingine aina ya E- jets na ATR.
Mkuu
 wa kitengo cha huduma za fedha wa Vodacom Tanzania Bw. Innocent 
Ephraim,akionesha bango lenye maelekezo muhimu ya kufuatwa ambayo 
yatawafanya wateja wapate huduma ya kulipia tiketi za usafiri kupitia 
huduma ya M-Pesa kwa urahisi zaidi,kushoto ni Mkurugenzi wa Kitengo cha 
Biashara cha Precision Air, Patrick Ndekana.
 Baadhi
 ya wafanyakazi wa Precision Air wakifatilia kiumakini mkutano wa 
waandishi wa habari kuhusiana na mkataba wa Vodacom Tanzania na kampuni 
yao ambapo wateja wa Precision Air wataweza kulipia tiketi za usafiri 
kupitia huduma ya M-Pesa.
Waandishi
 wa habari wakiwa kazini wakati wa Precision Air na Vodacom Tanzania 
walipokuwa wakitangaza mkataba kuhusiana na wateja wa Precision Air 
kuweza kulipia tiketi za usafiri kupitia huduma ya M-Pesa.
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment