TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
DC Korogwe awajibishwe kwa udhalilishaji
Mtandao
  wa Jinsia Tanzania (TGNP), tumesikitishwa sana na kauli iliyotolewa na
  Mkuu wa Wilaya ya Korogwe Mkoani Tanga Ndugu Mrisho Gambo, kwa  mwanasheria
  wa Halmashauri hiyo Bi. Najum Tekka, kuhusu uhalali wa shahada  
aliyonayo hususan kuihusisha shahada hiyo na vitendo vya ngono! Kama  
ilivyoripotiwa na vyombo vya habari ikiwepo gazeti la Majira Augosti 29,2012 Uk.3
Kauli
  hii ni udhalilishaji na ukiukwaji mkubwa wa haki za wanawake na 
inaenda  kinyume na misingi ya kuzingatia usawa sanjari na Katiba ya 
nchi ;  Uwezeshaji wa wanawake na utekelezaji wa Maazimio ya Haki na  Usawa katika ngazi za Kimataifa Kikanda na Nchini Tanzania.
Aidha kauli hii, inalenga kupotosha na kukatisha tamaa juhudi kubwa wanazofanya wanawake na wasichana katika  kupata
  elimu na mafanikio mbalimbali nchini Tanzania. Zaidi ya hapo, kauli 
hii  inadhalilisha na kushusha hadhi ya vyuo vya elimu ya juu 
vinavyofanya  kazi kubwa ya kutoa elimu kwa Watanzania.
Kutokana na kauli hiyo  DC  amekiuka
  maadili ya uongozi wa umma na kukidhalilisha kiti cha ukuu wa wilaya 
na  kiongozi Mkuu wa nchi aliyemteua kushika wadhifa huo. Aidha kauli ya
  kiongozi huyo ya kutimia  mahakama kutetea hoja yake , kunaashiria ubabe , ujeuri, vitisho, kiburi na dharau  ya  kutaka kuingilia uhuru wa mahakama na ajenda binafsi isiyokuwa na maslahi kwa wanawake na umma wa Watanzania
Kutokana na kauli hiyo ya udhalilishwaji ,sisi  wanaharakati  wa ukombozi wa wanawake Kimapinduzi, usawa wa kijinsia, haki za kibinadamu demokrasia tunalaani vikali kauli za DC na kutoa  Rai ifuatayo:
1.      Mkuu wa Wilaya  Ndugu Mrisho: amwombe radhi Mwanasheria Bi.  Najum Tekka, kwa kosa la  kumdhalilisha kijinsia
2.      Tume
  ya maadili ya utumishi wa umma, na Mamlaka nyingine za kinidhamu  
zimchukulie hatua za kinidhamu Ndugu Gambo kwa kutumia lugha ya  
kudhalilisha watumishi kinyume na maadili. 
3.      Wanawake  wote, wanaume, vijana wa kike na kiume kuendelea na mapambano dhidi ya  mfumo dume na mifumo yote kandamizi, kushikamana katika kudai misingi ya kisheria,  uwajibikaji  inayozingatia usawa na haki na kukataa kudhalilishwa katika ngazi binasfi na za umma !.
Imetolewa  Dar es salaam leo 31/08/2012 na: 
Usu Mallya
Mkrugenzi Mtendaji TGNP
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment