 
 
HUKU
 wadau wakiwa na shauku kubwa ya kumjua mshindi wa shindano hili la 
kumsaka staa wa kike mwenye mvuto ambaye hajaolewa 
‘The Ijumaa Sexiest 
Girl’, hatimaye kura za wasomaji zimeamua msanii wa filamu, Jackline 
Wolper kutoa mkono wa kwaheri.Mratibu wa shindano hili, Imelda Mtema
 alisema: 
“Mtifuano ulikuwa mkali sana na hii ilitokana na ukweli 
kwamba, wote waliobaki ni wakali kuanzia sura hadi maumbo yao.
 Wopler 
ametolewa na sasa kimbembe ni kati ya Wema na Agnes.”
 
 Kufuatia 
matokeo hayo ya Wolper kuchapa lapa, sasa wanabaki Wema na Agnes ambao 
watapigiwa kura kwa wiki mbili kabla ya kumpata mshindi. 
Ili kushiriki 
katika hatua hii muhimu ya kumpata mshindi, andika jina la mshiriki 
kisha litume kwenda namba 0786-799120.
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment