EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Sunday, September 23, 2012

Ajinyonga hadi kufa baada ya kupewa majibu ya kukutikana HIV+ve

MKAZI wa Kijiji cha Kasisa Kata ya Nyakasungu wilayani Sengerema, Shija Daudi (32) amejiua kwa kujinyonga na kamba hadi kufa usiku wa kuamkia jana baada ya kupima afya yake na kugundulika kuwa na Virusi Vya UKIMWI (VVU).Akizungumza na HabariLeo Jumapili jana akiwa nyumbani kwake mjini hapa, Isack Daudi alisema kuwa Daudi alikuwa amekwenda nyumbani kwake kuwasalimia lakini akiwa bado yuko nyumbani kwake alishikwa na maradhi ya kuumwa homa ya mara kwa mara iliyoambatana na malaria kwa muda wa wiki mbili.

Alisema baada ya kuona hali hiyo aliamua kumpeleka katika Zahanati ya Nyerere iliyoko Buswelu, lakini hali iliendelea kuwa mbaya na ndipo alipoamua kwenda kupima afya yake katika Hospitali ya Mkoa ya Sekou Toure ndipo alipogundulika kuwa na VVU, “Baada ya kubaini hayo, alijiunga na huduma ya tiba kwa kupewa ushauri nasaha na akawa anatumia dawa za kurefusha maisha za ARV kama kawaida,” alisema Isack.Alisema juzi akiwa anatoka kwenye mazishi ya jirani yake katika Mtaa wa Buswelu ghafla alikutana na watoto wake ambao walikuwa wanakimbia huku wakimueleza kuwa ndugu yake Shija alikuwa amejifungia ndani ya chumba, 

“Nilichukua pikipiki nikakimbia kwenda nyumbani nilipofika nilikuta yumo ndani amejifungia ndani na nilibisha hodi mara tatu bila kuniitikia ndipo nilipoamua kubomoa dirisha na nilipoingia ndani nilimkuta amening’inia, alikuwa amejiua na siku ile baada ya kumpima alisema haoni raha ya kuishi tena duniani, inaonekana alichukua maamuzi ya kujinyonga,” alisema Isack kwa masikitiko.



Anasema baada ya tukio hilo, aliamua kumpigia simu Balozi wa Mtaa wa Buswelu A, Turubuza Millinde na baada ya kufika alishauri apigiwe Mwenyekiti wa Mtaa, Meshack Budega ambaye alichukua jukumu la kumpigia simu Mkuu wa Kituo cha Polisi cha MwaTex kilichoko Nyakato, “Alikuja OCS na askari wenzake ambao walishuhudia tukio hilo na baadaye OCS alitushauri mwili upelekwe kituoni, kwake kwa ajili ya maelezo zaidi ikiwemo kufanyiwa uchunguzi zaidi na tunawashukuru polisi kwa ushirikiano waliotupatia kama familia na baada ya pale mwili ulipelekwa chumba cha kuhifadhia maiti Hospitali ya Rufaa ya Bugando,” alisema.

via HabariLeo



No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate