JUKWAA la Waandishi wa Habari wa Kiislamu Tanzania (NAMJOF)
litazinduliwa rasmi jijini Dar es Salaam, wiki ijayo, Mratibu wa Jukwaa
hilo, Hemed Adam Kimwanga alisema jana.
Kimwanga aliongeza kuwa, mahali na siku rasmi ya uzinduzi huo vitatangazwa wakati wowote na amewaomba waandishi wa habari wa Kiislamu kuwa tayari kujumuika kwa ajili ya kulizindua jukwaa hilo.
“Kwa hakika kwa sasa lazima jukwaa hili lianze rasmi kufanya kazi zake”, alisema Kimwanga ambaye ameasisi nia hiyo tangu mwaka 2007 mara baada ya kumaliza mkataba wake wa kikazi kwenye Baraza Kuu la Waislamu wa Tanzania (BAKWATA) akiwa Meneja Uhusiano na Msaidizi wa Katibu Mkuu wa Baraza hilo.
Amesisitiza kuwa matukio ya hivi sasa ya vurugu za Kiislamu nchini yamesababisha kuwepo umuhimu mkubwa na wa haraka wa kuwepo NAMJOF ili kuipeusha jamii ya Kiislamu na jamii nyingine na migongano isiyokuwa ya lazima.
Amesema kwamba madhumuni makubwa ya jukwaa hilo ni kuwawezesha waandishi wa habari wa Kiislamu kuijua vyema dini yao na fikra zake sahihi ili kuandika kwa usahihi mambo yote yanayoihusu dini ya Kiislamu kinyume cha ilivyo sasa ambapo inaonekana kuna mvurugano mkubwa wwnyw malengo ya kimaslahi ya kibinadaamu zaidi kuliko ya dini yenyewe.
“Tusipoliangalia hili litatugharimu wote huko mbele ya safari”, amesema Kimwanga na kusisitiza kuwa ni NAMJOF imara ndiyo itakayosaidia kuepusha uvunjifu wa amani ya nchi unaonekana dhahiri kulijongelea Taifa hivi sasa, “Huwezi kumng’oa Mifti iwapo wewe humo ndani ya ulingo wa uongozi rasmi wa BAKWATA”, alisema Kimwanga na kuongeza, “Mufti anaondolewa na vikao rasmi ndani ya Baraza hilo”.
Amesema chini ya katiba ya BAKWATA, Mufti anang’olewa baada ya kikao cha masheikh waTanzania nzima kijulikanacho kama ‘Tume ya Dini’ wanaotambulika na Baraza hilo kumjadili na kupeleka mapendekezo yao kwenye Mkutano Mkuu ambao utaidhinisha au kupinga mapebndekezo ya Tume ya Dini kwa zaidi ya robo tatu ya kura zote za wajumbe halali, “Kinyume cha hapo utakuwa ni uhaini mkubwa ambao hauwezi kuvumiliwa na wapenda amani wakiwemo Waislamu na wasiokuwa waislamu”, alisisitiza.
Alisema waandishi watakapoelewa dini yao, katiba ya BAKWATA na katiba mama ya nchi, hapana shaka utulivu utatopea nchini na hivyo kuongeza ustawi wa kizazi kilichopo na kijacho cha Kiislamu na ksichokuwa cha Kiislamu hapa nchini na nje ya nchi, “Kwa kitendo cha kuwavuruga na kuwapotosha waumini wa dini ya Kiislamu kuhusu sensa na hiki cha sasa cha kutaka kumng’oa Mufti kutoka madarakani ni ushahidi mkubwa kuwa waumini wa dini ya Kiislamu wanatakiwa wapewe elimu sahihi ya dini yao na kanzu zake zinazoizunguka na hilo ndilo jukumu la NAMJOF”, alisIsitiza Kimwanga.
RasImu ya NAMJOF tayari imetayarishwa na Kimwanga alisema moja ya mambo makuu yatakAyojadiliwa ni kuipitia rasmi hiyo ili ikipita isajiliwe kwa kulihuisha rasmi jukwaa hilo kisheria za za nchi.
Alisema tayari kuna taasisi zimeonesha utayari wa kutoa semina za kidii, kiutawala na uongozi kwa waandishi wa habari wa Kiislamu chini ya NAMJOF ili jukwa hilo lifanye kazi zake kwa usahihi na maendeleo chanya ya dini ya Kiislamu na jumuia nyingine hapa nchini na nje ya nchi.
Bila kuzitaja taasisi hizo, Kimwanga alisema NAMJOF pia itakuwa na Idara mbalimbali na kamati rasmi za masheikh, kinamama, vijana na nyingine na kwamba kutakuwa na idara za kidini na kidunia kwa faida ya waandishi wa habari wa Kiislamu na Taifa zima, “Tutakuwa na kamati ya Masheikh sita ambao watakuwa mhimili mkubwa wa jukwaa letu katika kutafsiri mienendo ya dini ya Kiislamu na saikolojia yake”, alisema Kimwanga.
Alipoulizwa kuhusu kadhia ya Mufti kung’olewa madarakani, Kiwamnga alisema, kwa niaba ya NAMJOF, anapinga vikali azma hiyo na kusema kuwa wanaotaka kufanya hivyo wanamkosea Mwenyezi Mungu aliyeamrisha waumini wa dini ya Kiislamu kumuheshimu na kumtii yeye kwanza, Mtume wake Muhammad (SAW) na wale wote walioko juu ya mamlaka ikiwemo serikali na viongozi wa dini.
Alisema kikatiba ya Baraza Kuu la Waislamu wa Tanzania (BAKWATA), Mheshimiwa Mufti bado hajavunja kipengele chochote ambacho kingehalalisha kuondolewa kwake. Chini ya katiba ya BAKWATA, Mufti anaondolewa iwapo atapoteza sifa kama vile kurukwa akili, kuwa mlevi, kuwa mzinzim, kuwa muongo na iwapo atabadili dini, “Hivyo hao wanaotaka kumng’oa Mufti madarakani wanafanya uhaini mkubwa wa mchana peuepe pee”, amesisistiza Kimwanga na kuishukuru serikali na vyombo vyote vya ulinzi na usalama kwa kumlinda Mufti na viongozi wengine wote wa BAKWATA wasipokwe madaraka yao waliyoyapata kikatiba.
Falsafa ya kuwa na chombo cha Waandishi wa Habari wa Kiislamu nchini iliasisiwa na mwandishi mkongwe nchini, Swalehe Msuya wa Daily News na baadaye Radio Tanzxania kwenye miaka ya themanini.
Baadaye mapema kwenye miaka ya 2000, mwandishi mwingine mkongwe na fundi mitambo wa Radio Tanzania Dar es Salaam, Athumani Mahanyu alijaribu kuanzisha chama cha aina hiyo lakini akaishia kuwa muasisi wa Radio Sauti ya Koran inayomilikiwa na BAKWATA kwa sasa,
Waandishi wote hao wawili Msuya na Mahanyu kwa sasa ni marehemu.
HabariMseto blog
Kimwanga aliongeza kuwa, mahali na siku rasmi ya uzinduzi huo vitatangazwa wakati wowote na amewaomba waandishi wa habari wa Kiislamu kuwa tayari kujumuika kwa ajili ya kulizindua jukwaa hilo.
“Kwa hakika kwa sasa lazima jukwaa hili lianze rasmi kufanya kazi zake”, alisema Kimwanga ambaye ameasisi nia hiyo tangu mwaka 2007 mara baada ya kumaliza mkataba wake wa kikazi kwenye Baraza Kuu la Waislamu wa Tanzania (BAKWATA) akiwa Meneja Uhusiano na Msaidizi wa Katibu Mkuu wa Baraza hilo.
Amesisitiza kuwa matukio ya hivi sasa ya vurugu za Kiislamu nchini yamesababisha kuwepo umuhimu mkubwa na wa haraka wa kuwepo NAMJOF ili kuipeusha jamii ya Kiislamu na jamii nyingine na migongano isiyokuwa ya lazima.
Amesema kwamba madhumuni makubwa ya jukwaa hilo ni kuwawezesha waandishi wa habari wa Kiislamu kuijua vyema dini yao na fikra zake sahihi ili kuandika kwa usahihi mambo yote yanayoihusu dini ya Kiislamu kinyume cha ilivyo sasa ambapo inaonekana kuna mvurugano mkubwa wwnyw malengo ya kimaslahi ya kibinadaamu zaidi kuliko ya dini yenyewe.
“Tusipoliangalia hili litatugharimu wote huko mbele ya safari”, amesema Kimwanga na kusisitiza kuwa ni NAMJOF imara ndiyo itakayosaidia kuepusha uvunjifu wa amani ya nchi unaonekana dhahiri kulijongelea Taifa hivi sasa, “Huwezi kumng’oa Mifti iwapo wewe humo ndani ya ulingo wa uongozi rasmi wa BAKWATA”, alisema Kimwanga na kuongeza, “Mufti anaondolewa na vikao rasmi ndani ya Baraza hilo”.
Amesema chini ya katiba ya BAKWATA, Mufti anang’olewa baada ya kikao cha masheikh waTanzania nzima kijulikanacho kama ‘Tume ya Dini’ wanaotambulika na Baraza hilo kumjadili na kupeleka mapendekezo yao kwenye Mkutano Mkuu ambao utaidhinisha au kupinga mapebndekezo ya Tume ya Dini kwa zaidi ya robo tatu ya kura zote za wajumbe halali, “Kinyume cha hapo utakuwa ni uhaini mkubwa ambao hauwezi kuvumiliwa na wapenda amani wakiwemo Waislamu na wasiokuwa waislamu”, alisisitiza.
Alisema waandishi watakapoelewa dini yao, katiba ya BAKWATA na katiba mama ya nchi, hapana shaka utulivu utatopea nchini na hivyo kuongeza ustawi wa kizazi kilichopo na kijacho cha Kiislamu na ksichokuwa cha Kiislamu hapa nchini na nje ya nchi, “Kwa kitendo cha kuwavuruga na kuwapotosha waumini wa dini ya Kiislamu kuhusu sensa na hiki cha sasa cha kutaka kumng’oa Mufti kutoka madarakani ni ushahidi mkubwa kuwa waumini wa dini ya Kiislamu wanatakiwa wapewe elimu sahihi ya dini yao na kanzu zake zinazoizunguka na hilo ndilo jukumu la NAMJOF”, alisIsitiza Kimwanga.
RasImu ya NAMJOF tayari imetayarishwa na Kimwanga alisema moja ya mambo makuu yatakAyojadiliwa ni kuipitia rasmi hiyo ili ikipita isajiliwe kwa kulihuisha rasmi jukwaa hilo kisheria za za nchi.
Alisema tayari kuna taasisi zimeonesha utayari wa kutoa semina za kidii, kiutawala na uongozi kwa waandishi wa habari wa Kiislamu chini ya NAMJOF ili jukwa hilo lifanye kazi zake kwa usahihi na maendeleo chanya ya dini ya Kiislamu na jumuia nyingine hapa nchini na nje ya nchi.
Bila kuzitaja taasisi hizo, Kimwanga alisema NAMJOF pia itakuwa na Idara mbalimbali na kamati rasmi za masheikh, kinamama, vijana na nyingine na kwamba kutakuwa na idara za kidini na kidunia kwa faida ya waandishi wa habari wa Kiislamu na Taifa zima, “Tutakuwa na kamati ya Masheikh sita ambao watakuwa mhimili mkubwa wa jukwaa letu katika kutafsiri mienendo ya dini ya Kiislamu na saikolojia yake”, alisema Kimwanga.
Alipoulizwa kuhusu kadhia ya Mufti kung’olewa madarakani, Kiwamnga alisema, kwa niaba ya NAMJOF, anapinga vikali azma hiyo na kusema kuwa wanaotaka kufanya hivyo wanamkosea Mwenyezi Mungu aliyeamrisha waumini wa dini ya Kiislamu kumuheshimu na kumtii yeye kwanza, Mtume wake Muhammad (SAW) na wale wote walioko juu ya mamlaka ikiwemo serikali na viongozi wa dini.
Alisema kikatiba ya Baraza Kuu la Waislamu wa Tanzania (BAKWATA), Mheshimiwa Mufti bado hajavunja kipengele chochote ambacho kingehalalisha kuondolewa kwake. Chini ya katiba ya BAKWATA, Mufti anaondolewa iwapo atapoteza sifa kama vile kurukwa akili, kuwa mlevi, kuwa mzinzim, kuwa muongo na iwapo atabadili dini, “Hivyo hao wanaotaka kumng’oa Mufti madarakani wanafanya uhaini mkubwa wa mchana peuepe pee”, amesisistiza Kimwanga na kuishukuru serikali na vyombo vyote vya ulinzi na usalama kwa kumlinda Mufti na viongozi wengine wote wa BAKWATA wasipokwe madaraka yao waliyoyapata kikatiba.
Falsafa ya kuwa na chombo cha Waandishi wa Habari wa Kiislamu nchini iliasisiwa na mwandishi mkongwe nchini, Swalehe Msuya wa Daily News na baadaye Radio Tanzxania kwenye miaka ya themanini.
Baadaye mapema kwenye miaka ya 2000, mwandishi mwingine mkongwe na fundi mitambo wa Radio Tanzania Dar es Salaam, Athumani Mahanyu alijaribu kuanzisha chama cha aina hiyo lakini akaishia kuwa muasisi wa Radio Sauti ya Koran inayomilikiwa na BAKWATA kwa sasa,
Waandishi wote hao wawili Msuya na Mahanyu kwa sasa ni marehemu.
HabariMseto blog
No comments:
Post a Comment