EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, September 14, 2012

Zaidi ya Wanawake 500 wanabakwa na mashemeji zao


UTAFITI uliofanywa hivi karibuni umeonyesha kuwa zaidi ya wajane 544 wametendewa vitendo vya kikatili, ikiwamo kubakwa na mashemeji zao kuanzia Januari hadi Julai, mwaka huu.

Utafiti huo unaonyesha kuwa kati ya hao, wajane 18 walirithiwa na kutakaswa wakati nane walilazimishwa kuingiliwa kinyume cha maumbile kwa imani ya kusafisha mikosi katika ukoo.

Taarifa ya utafiti huo ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Msaada wa Sheria kwa Wanawake na Watoto (WLAC), Theodosi Muhulo. Alikuwa akitoa taarifa hiyo mbele ya waandishi wa habari, iliyolenga kukemea vitendo vya kikatili na kibaguzi vinavyoendelea dhidi ya wajane.

Muhulo alisema utafiti uliofanywa na kituo umebaini kuwa baadhi ya wajane wamekuwa wakiporwa ardhi na mali walizoachiwa na waume zao pindi wanapofariki. Alisema utafiti huo ulifanywa kupitia kikosi kazi cha kamati ya mkataba wa kimataifa wa kuondoa aina zote za ubaguzi dhidi ya wanawake (CEDAW).

Alisema idadi hiyo ni kutoka katika vituo vya Dar es Salaam, Muleba, Karagwe, Kasulu Kigoma, Mara, Shinyanga na Songea.

“Takwimu kutoka Mara zinaonyesha kuwa wajane 55 walinyang’anywa ardhi zao baada ya waume zao kufariki, 23 walipewa mirathi kidogo, wajane 41 walifukuzwa baada ya waume zao kufariki kwa maambukizi ya VVU. Takwimu hizi ambazo ni za kuanzia Januari mpaka Julai 2012, pia zilijumuisha mashauri 174 kutoka Kitengo cha Wasaidizi wa Sheria, kilichopo Songea, yanayohusu wajane kunyimwa haki zao,” alisema.

Kutokana na hali hiyo, aliitaka Serikali kufanya marekebisho ya sheria za mirathi kwa kuwa mfumo dume uliopo unabagua na kukandamiza wanawake na kuchangia ukandamizaji wa kiuchumi.

“Vile vile sheria hizi zinakinzana na sheria mama ambayo ipo katika Katiba ya mwaka 1977 ibara ya 12, 13 na 24 pamoja na mikataba mbalimbali ya Kimataifa, ambayo serikali yetu imeridhia. Mfumo huo wa mirathi unakiuka haki ya msingi ya usawa, umiliki wa mali na kuwa na maisha bora, familia na kutweza utu wa mwanamke, hususani wajane,” alisema.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Wanawake na Ustawi wa Mtoto (TWCWC), Edda Mariki, alitoa wito kwa jamii kuondokana na mila potofu dhidi ya wajane na kuwatendea haki badala ya kuwanyanyasa.

“Mashemeji waache kubaka wajane kwa kutumia mfumo wa kurithi wajane, aidha jamii iondokane na dhana ya kuona wajane ni wachawi na wengine kusababisha kupigwa na kuuawa,” alisema.

Alizitaka taasisi mbalimbali kuendelea kutoa elimu kwa Watanzania ili kuondokana na mila potofu kwa ustawi wa jamii, kwani hicho ndiyo chanzo.

via Mtanzania

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate